1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
1Huan, unaute aw, Tanchin Hoih ka honhilh jaw ka honthei sak nawn ding a; huai Tanchin Hoih na nakipahpih ua, huaimah ah na ding ua;
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
2Kon thu hilh pen na mawk gintak uh a hih louha, pom kichian na hih uleh huai mahah hotdam lelin na om uhi.
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
3A masapenin ken ka muh sam tuh nou kon hilh sawna; huchia, Kris Laisiangthou bangbanga i khelhnate jiaka a siha,
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
4A vui ua, Laisiangthou bangbanga ni thum nia kaihthoha a oma,
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
5Kifa kianga a hongkilaka, huai khita sawm leh nihte kianga a kilak thute.
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
6Huai khitin unau za nga sanga tam kiangah a kilak nawna, huaite laka mi, a tam jaw tutanin leng a dam lai ua, khenkhat bel a ihmuta uhi.
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
7Huai khitin Jakob kiangah a kilak nawna; huai khitin sawltak tengteng kiangah.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
8Huan, a tawppenah, a hunlou banga piang, keimah kiangah leng a kilaka.
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
9Kei jaw sawltak laka neupen, Pathian saptuamte ka sawi jiaka sawltaka chihtuak louh ka hi ngala.
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
10Himahleh, Pathian hehpihna jiakin ka hihhih ka hita; huan, a hehpihna honpiak a thawnin a om keia, huchih naksangin, amau tengteng sangin ka sem gim jaw ahi; himahleh keimah kian ka sem keia, Pathian hehpihna ka kianga omin a sem jaw hi.
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
11Abang abang hitaleh, ken leng, amau leng, huchiin ka gen jel ua, huchiin nou leng na gingta uhi.
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
12Huan, Kris thu misi laka kipan kaihthohin a om chih a honhilh ngal uleh, bangchidan ahia na lak ua khenkhatin, Misi thohnawnna himhim a om kei, na chih uh?
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
13Misi thohnawnna himhim a omlou ahihleh, huai Kris leng kaihthohin a om kei ding hi.
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
14Huan huai Kris kaihthoha a om kei leh, i thugen uh bangmah lou ahi dinga, na gin uleng bangmah lou ahi ding hi.
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
15Ahi, Kris a kaithou chih Pathian i theihpih jiakin, Pathian lam thu ah theihpih juauthei leng i honghi ding hi, misite kaihthoha a om kei uleh, amah leng a kaithou kei dinga.
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
16Misite kaithoha a om kei un jaw, Kris leng kaihthohin a omta kei ding.
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
17Huan, Kris kaihthoha a om kei leh, na gin uh bangmah lou ahi dinga, na khelhna uah na om ni louhlouh uh ahi ding.
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
18Huai ahihleh, Krisa ihmu sate a mangthangte uh ahi ding hi.
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
19Tu damsung kiaa Kris tunga lametna i neih injaw mi tengteng dia mi hehpihhuai pen i hi ding hi.
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
20Himahleh, Kris misi laka kipan kaihthohin a om taktak ahi, ihmute laka kipan gahmasa a na hita hi.
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
21Mi khat jiaka sihna a hongom jiakin mi khat jiak mahin misi thohnawnna leng a hongomta ahi.
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
22Adam ah mi tengteng a si mahbang un, Kris ah mi tengteng hihhinin leng a om ding uhi.
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
23Himahleh, amau hun chiat jel ah: Kris tuh gah masapente ahia; huai khit chiangin a hongpainawnna ah Kris ate.
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
24Huai khit chiangin a tawp a hongtung ding; huai hun chiangin, vaihawmna tengteng leh, thuneihna leh thilhihtheihna tengteng a hihman nungin, Pathian kiangah, Pa kiang ngeingei ah gam tuh a pe ding hi.
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
25A melmate tengteng a khe nuaia a koih masiah aman vaihawm ding ahi ngala.
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
26Melma nanungpen a hihmanga om ding tuh sihna ahi.
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
27Aman a khe nuaiah bangkim a koih ngala, himahleh, A nuaiah bangkim koihin a om, a chihin, a nuaia bangkim koihpa a pang kha kei chih a kimugige ahi.
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
28Huan, a nuaia bangkim koiha a om hun chiangin, Tapa mahmah leng a nuaia koihin a om dinga, Pathian tuh bangkima bangkim a hih theihna dingin
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
29Huchi bang ahih kei in, misite adinga baptisma a tansak uh bang a chihna uh hi ding ahia? Misite kaihthoha a om louh hial ding uleh, bang achia amau adia baptisma tansak uh ahia?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
30Bangjiakin ahia, kei leng dak kal chiha lauthawnghuaia ka om?
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
31Unaute aw, Kris Jesu i Toupaa ka honsuanna sialin, Ni tengin ka si, ka chi ahi.
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
32Mihing danin gen leng, Ephesa khua a gam sate kilaipih ka hih leh, kei din bang a phatuam ding? Misi kaihthoha a om kei ding uleh nein dawn leng ake, jingchianga si ding hi ve hangin.
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
33Khemin om kei un; Lawm gilouten omdan hoih a hihgawp nak uhi.
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
34Kizentakin halh unla, thil hihkhial kei un; khenkhatin Pa Pathian theihna himhim na neikei uh; huai tuh na zumna ding ua ka gen ahi.
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
35Himahleh, kuahiamkhatin, Misi bangchin kaihthoh ahi ding uh? Pumpi bangchi bang puin ahia a hongsuah ding? a chi ahi ding e.
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
36Nang mi hai, nangmah mahin na tuh leng, a sih phot keileh hihhinin a om sama.
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
37Huan, chi na tuhin a pumpi hongom ding pen ahi keia, a tang lel na tuh zo nak, buh tang hiam, chi dang tang hiam ahi thei hi.
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
38Himahleh, Pathianin amah deih bangbangin pumpi a pia hi, a tang chih kiangah amah pumpi chiat.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
39Sa tengteng sa chi khat ahi kei ua; mihing sa a tuama, gamsa sa a tuama, vasa sa a tuama, ngasa sa a tuam ahi.
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
40Vanlam pumpite leng a oma, leilam pumpite leng a om, himahleh vanlam pumpite thupina a tuama, leilam pumpite thupina a tuam,
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
41Ni thupina a tuam, kha thupina a tuama, aksite thupina a tuam; aksi leh aksi leng a thupina uh a tuam ngala.
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
42Misite thohnawnna leng tuabang ahi. Muattheia tuhin a oma, muattheiloua kaihthohin a om.
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
43Pahtawilouha tuhin a oma, thupitaka kaihthohin a om. Hatloua tuhin a oma, thilhihtheihna neia kaihthohin a om.
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
44Salam pumpi-a tuhin a oma, khalam pumi-a kaihthohin a om. Salam pumpi a om leh khalam pumpi leng a om.
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
45Huchiin, Mi masapen Adam tuh mihing a honghia, chi-a gelh ahi; Adam nanungpen bel hinna pepa kha a honghi a.
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
46Himahleh, khalam a om masa keia, sa lam a om jaw; huai zohin khalam pen a om hi.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
47Mihing masapen leia siam, leimi ahia; mihing nihna pen vanmi ahi.
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
48Leia siam mihing bang tuh, leia te leng ahi ua; vana mi bang tuh, vanate leng ahi uhi.
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
49Huan, leia siam batna pen i put bangin, vana batna pen leng i pu sam ding uhi.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
50Unaute aw, sa leh sisanin Pathian gam a luah theikei dinga; muat theiin muat theilou a luah sam kei ding, chih, ka gen ahi.
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
51Ngai un, thuguk ka honhilh ding hi: i vek un i ihmu khol kei dinga, himahleh i vek un pengkul nanungpen gin chiangin, sawtlou kalin,
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
52Mitphiat kal louin, hihlamdangin i om vekta ding; pengkul ging ding ahi ngala, huchiin, misite tuh muat theiloua kaihthohin a om ding ua, eite leng hihlamdanin i om ta ding hi.
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
53Hiai muat theiin muat theihlouhna a silh ding ahi a, hiai sitheiin leng sihtheihlouhna a silh sam ding ahi.
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
54Huchia, hiai muattheiin muatheihlouhna a silha, hiai sithein sihtheihlouhna a silh hun chiangin, huai hun ngeingeiin, zohnain sihnaa valh zouta, chih thugelh a hong tung ding.
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
55Aw sihna, na zohna koia omta ahia? Aw sihna na gu koia omta ahia?
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
56Sihna gu tuh khelhna ahia; khelhna thilhihtheihna tuh dan ahi.
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
57Himahleh, i Toupa Jesu Kris jiaka zohna honpepa Pathian kiangah kipahthu om hen.Huaijiakin, ka unau deihtakte aw, kip takin, hihlin vuallouhin, Toupa nasep phatuam ngai taka sem gigein om un, na sepgimna uh Toupa ah a thawn ngei kei chih na thei ngal ua.
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.
58Huaijiakin, ka unau deihtakte aw, kip takin, hihlin vuallouhin, Toupa nasep phatuam ngai taka sem gigein om un, na sepgimna uh Toupa ah a thawn ngei kei chih na thei ngal ua.