Swahili: New Testament

Paite

2 Corinthians

5

1Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono.
1I omna leia in pen hisiatin om mahleh, vanah, in, khutta lamlouh, khantawna om ding, pathian akipan in kip inei uh chih i thei ngal ua;
2Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
2Vana kipan i omna ding silhthuah ut mahmahin hiai in ah thum cihtakin i thum gige ngal ua;
3Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
3Huchibanga silhin om leng vuaktangin i omkei ding uhi.
4Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
4Eite hiai ina i om sungin gikpuain thum petmahin i thum ngala, silh loua i ut jiak ahi keia, silhthuaha om i ut jiak ahi jaw, sitheipen tuh hinna valh zoha a om theihna dingin.
5Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
5Huan, huaia mahmah dinga honsutuahpa Pathian ahi, khamna kha honpepa.
6Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
6Huchiin, pumpia i om laitengin Toupa kiangah i om kei chih theiin, muangtakin i om gige uhi.
7Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
7Mu theia pai louin, ginnain i pai zo jel uhi.
8Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
8Muangtakin i om, huan pumpia om loua Toupa kianga om i ut jaw hi.
9Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
9Huaijiakin, omin, om kei leng, amah kipahpih lam mi hih i tum chinten ahi.
10Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
10Mi chihin, pumpia thil hihte a sia a phain, i hih bangbanga i muh chiat theihna dingin, Kris thukhenna tutphah maah hihlatin i om vek ding uh ahi.
11Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
11Huchiin, Toupa kihtakna dan theiin mihingte ka zol jel uhi, Pathian kiangah bel latsakin ka om ua, na sia leh pha theihna uah leng latsaka ka om uh ka lamen ahi.
12Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
12Na kiang uah ka kigen hoih nawn uh ahi keia, lungtang lam hi loua, dinmun lam lel suangte, bang ahi hiam dawnna ding na neih theihna ding un kou lamah suan theihna honbawlin ka gen jaw uhi.
13Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
13Ka hai u leh, Pathian adin ahi a; ka pi u leh, noumau adin ahi ngala.
14Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
14Kris itnain honsawl teitei ahi; hichin ka ngaihtuah uh: Mi tengteng sih sikin mi khat a si a, huaijiakin mi tengteng a si uhi;
15Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
15A hingte leng amau adia a hin nonlouh ua, a sih sik ua sia thounawn adinga a hin jawkna ding uh ahi, mi tengteng sih sika a sih.
16Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
16Huchih ahih jiakin tuban kou jaw salamah kuamah ka thei nawngta kei ding uh; sa lamah Kris na theita mahle ung leng; tun jaw ka theita kei uhi.
17Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
17Huchih ahih jiakin, kuapeuh Krisa a om leh, thilsiam thak a honghi a; thil luite a mangta a; ngai un, a hongthakta uhi.
18Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
18Himahleh, bangkim Pathian kianga kipana pawt ahi a; aman Kris jiakin amah toh kituakin honbawla, kituahna nasepna a honpia hi;
19Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
19Huchiin, Pathianin Kris ah khovel amah toh kituaknawnin a bawla, a tatleknate uh tatleknaa seh sak louin, kituahnawnna thu a honkem sak ahi.
20Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
20Huaijiakin, Kris sika palai ka hi ua, Pathianin koute zangin a hon ngen ahi; Pathian toh kituakta un aw, chiin, Kris sikin ka hon ngen uhi.Amah ah Pathian diktatna i honghih theihna dingin, khelhna himhim theilou amah tuh Pathianin eite jiakin khelhnain a bawl hi.
21Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.
21Amah ah Pathian diktatna i honghih theihna dingin, khelhna himhim theilou amah tuh Pathianin eite jiakin khelhnain a bawl hi.