Swahili: New Testament

Paite

John

5

1Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu.
1Huai thil nungin Judate ankuangluina a om a; Jesu Jerusalem khua ah a hoh tou a.
2Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao.
2Huan, Jerusalem ah belam kongkhak kiangah dil a oma, huai tuh Hebru pauin Bethsaida a chi ua, inlim nga neia.
3Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: vipofu, viwete na waliopooza. Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe,
3Huai ah damloute, mittawte, khebaite, jawte tampi a lum phengphung ua, tui hongtat ngakin.
4maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.
4Bang chiang hiamin huai dil ah angel a hoh suk a, tui a vatok a; huchiin, kuapeuh huai tui a kitoh khita valut masa penpen tuh, bangchibang natna nei hileh leng hihdamin a om jel hi.
5Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane.
5Huan, huaiah kum sawmthum leh giat damlou mi kuahiam a om a.
6Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo, akatambua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, "Je, wataka kupona?"
6Huan, Jesun a lum tuh a mu a, huchi bangin sawtpi a omta chih a thei a, a kiangah, Hihdam na ut hia? a chi a.
7Naye akajibu, "Mheshimiwa, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia."
7Huan, damloupan, Pu, tui kitohin dila honkoih ding mi ka neikei hi, ka hoh sungin mi dangin honmakhelh nak uh, achia, a dawng a.
8Yesu akamwambia, "Inuka, chukua mkeka wako utembee."
8Huan, Jesun a kiangah, Thou inla, na awngphah la inla, khein paita in, a chi a.
9Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.
9Huan, thakhatin huai mi tuh a dam pah a, a awngphah a la a, a paita hi.
10Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, "Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako."
10Huai ni tuh Khawlni ahi, Huchiin Judaten a dampa kiangah, Khawlni ei ve, na awngphah na lak a siang kei, a chi ua.
11Lakini yeye akawaambia, "Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: Chukua mkeka wako, tembea."
11Huan, aman a kiang uah, Honhihdampa ngeingeiin ka kiangah, Na awngphah la inla, khein paita in, honchi ahi, a chi a, a dawnga.
12Nao wakamwuliza, "Huyo mtu aliyekwambia: Chukua mkeka wako, tembea, ni nani?"
12Huan, amau a kiangah, Na awngphah la inla, khein paita in, na kianga chipa kua ahia? a chi ua, a dong ua.
13Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu.
13Himahleh, a dampan tuh kua ahia a hih a theikei a, huaia mipi a om jiak un Jesu a paimangta ngala.
14Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa Hekaluni, akamwambia, "Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi."
14Adenchiangin Jesun amah Pathian biakin ah a mu a, a kiangah, Ngaiin, na damta hi, khial nawnta ken, huchilou injaw thil hoihlou sem na tungah a hongom kha ding hi, a chi a.
15Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.
15Huan, huai mi tuh a vapai khia a, Judate kiangah a hihdampa Jesu ahi chih a hilh a.
16Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu.
16Huchiin, Khawlnia huai thil a hih jiakin Judaten Jesu a engbawl ua.
17Basi, Yesu akawaambia, "Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi."
17Himahleh, Jesun amau a houpiha, a kiang uah, Ka Pan tutan phain leng na asem jel hi, ken leng ka sem jel, a chi a.
18Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumwua Yesu: si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.
18Huchiin, Judaten hihlup a tum semsem ua, Khawlni a tanlouh jiak kia leng ahi keia, Pathian amah Paa a bawl a, Pathian toh ki kima a kibawl jiakin leng ahi.
19Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
19Huan, Jesun a kiang uah, Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Tapain amahin bangmah a hih theikei, Pa thil hih a muh kia lou ngal; thil a hih peuhmah, Tapain leng a hih sam jel ahi.
20Baba ampenda Mwana, na humwonyesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonyesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
20Pain Tapa a ita, a thilhih peuhmah a kiangah a musak a; hiaite sanga thilhih thupijaw a kiangah a musak ding, lamdang na sak ding un.
21Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uzima, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uzima wale anaopenda.
21Pain misite a a kithou a, hinna a piak bangin, Tapa inleng a utnana kiangah hinna a pia.
22Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,
22Pain kuamah vai a hawm sak ngei kei, vai tengteng Tapa a hawm sak zota;
23ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba ambaye amemtuma.
23mi tengtengin Pa zahna apiak bang un, Tapa leng zahna a piakna dingun. Kuapeuhmah Tapa zah lou ten jaw, Pa a sawlpa leng a zah kei uhi.
24"Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima.
24Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Kuapeuh ka thu ja a, honsawlpa gingtain, khantawna hinna a nei; siamlouhin a om keia, sihnaa kipan a pawta, hinna ah a lut zota ahi.
25Kweli nawaambieni, wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia, wataishi.
25Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, A hun a tung dekta, tuin leng a tung lellelta, huaihun chiangin misiten Pathian Tapa aw a za ding ua, a za peuhmah a hing ding uh.
26Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo pia alivyomjalia Mwanawe kuwa asili ya uhai.
26Pain amaha hinna a nei bangin, Tapa leng amaha hinna neidingin a peta hi.
27Tena amempa mamlaka ya kuhukumu kwa sababu yeye ni Mwana wa Mtu.
27Huan, Mihing Tapa a hih jiakin, a kiangah thukhenvaihawmna thu a pia hi.
28Msistaajabie jambo hili; maana wakati unakuja ambapo wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake,
28Hiai khawng lamdang sa kei un, a hun a tung dekta, huai hun chiangin han a om tengtengin a aw a za ding ua, a pawt vek ding uh;
29nao watafufuka: wale waliotenda mema watafufuka na kuishi, na wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa.
29thil hoih hihte tuh hinna tangin a thou nawn ding ua, thil gilou hihte tuh siam louh tangin a thou nawn ding uh.
30"Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi nina hukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma.
30Keimahin bangmah ka hih theikei; bila kajak bangbangin vai ka hawm jel; ka vaihawm tuh a dik ahi, keimah thu thuin om ka tum keia, honsawlpa thuthu ja ua om ka tup jel jiakin.
31Nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushahidi wangu hauwezi kukubaliwa kuwa wa kweli.
31Keimah tanchin theisak leng, ka thu theihsak a dik kei ding;
32Lakini yuko mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami najua kwamba yote anayosema juu yangu ni ya kweli.
32ka tanchin theisak mi dang ahi, aman ka tanchin a theihsak tuh a dik chih ka thei hi.
33Ninyi mlituma ujumbe kwa Yohane naye aliushuhudia ukweli.
33Nou Johan kiangah mi na sawl ua, huan, aman, thutak tanchin honna theisak hi.
34Si kwamba mimi nautegemea ushahidi wa wanadamu, lakini nasema mambo haya ili mpate kuokolewa.
34Thu theihsak ka san tuh mihing akipan ahi chihna ahi keia; himahleh na hinna ding un hiai thu tuh ka gen ahi.
35Yohane alikuwa kama taa iliyokuwa ikiwaka na kuangaza, nanyi mlikuwa tayari kufurahia mwanga huo kwa kitambo.
35Huai Johan tuh khawnvak kuangtak leh vak tak ahi, a vakah nuamsak tak dih na ut uh.
36Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma.
36Himahleh, theihsakna ka neihjaw Johan theihsakna thu sangin a thupi jaw ahi: Pain thil hih zoh dinga a honpiak, ka thil hih ngeiin Pain honsawl chih ka tanchin a theisak hi.
37Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake,
37Pa honsawlpan leng ka tanchin a theisakta. Nou chiklai mahin a aw na za ngei kei ua, a mel leng na mu ngei sam kei uh.
38na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.
38A thu leng noumau ah na pai kei uh, a sawlpa na gintak louh jiakun.
39Ninyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uzima wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia!
39Laisiangthou na phat sim ua, a sunga khantawna hinna oma na gintak jiakun: huai laisiangthou tuh ka tanchin theihpihna lah ahi ngala.
40Hata hivyo, ninyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima.
40Himahleh, hinna nei dingin ka kiangah na hong nuam ngal kei uh.
41"Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu.
41Mihing pahtawina ka sang kei.
42Lakini nawajua ninyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.
42Himahleh nou kon thei hi, Pathian itna noumau ah na neikei uhi.
43Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea.
43Ka Pa minin ka honga, nouten non kipahpih kei uh: mi dang amah minin hong leh, amah na kipahpih ding uhi.
44Mwawezaje kuamini, hali ninyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu ninyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu?
44Nou kipahtawi tuahna paktate aw, bangchin na gingta thei ding ua? Pathian tak kiaa pawt pahtawina lah na zong kei ua.
45Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye ninyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki.
45Ken Pa kianga nou kon hek ding gingta kei un: nou honhek khat a om, na muan uh Mosi ngei.
46Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia; maana Mose aliandika juu yangu.
46Mosi na gingta hile-uchin kei leng hongingta ta ding hi uchina; aman ka tanchin ahi a gelh.Himahleh, a thu gelh lah na gingta ngal kei ua, bangchin ka thu na gingta ding ua? a chi a.
47Lakini hamuyaamini yale aliyoandika, mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?"
47Himahleh, a thu gelh lah na gingta ngal kei ua, bangchin ka thu na gingta ding ua? a chi a.