Swahili: New Testament

Paite

Luke

2

1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
1Huan, huai laiin hichi ahia, Kaisar Augusta in khovel tengteng min khum ding thu a pia a.
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
2Huai tuh Suria gama Kurinia gam ukpa a hih laia min khumna masapen ahi.
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
3Huchiin, mi tengteng a min uh khum dingin amau khua chiat uah a hoh ua.
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
4Huan, Joseph leng, David inkuante leh a suan a hih manin Galili gama Nazaret khua akipanin, Judia gama David khua Bethlehem kichi ah a hoh ta a.
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
5Mari a zikham gai san lai toh, min khum dingin.
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
6Huan, hichi ahia, huai laia a om lai un, a nauneih a honghunta a.
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
7Huan, a ta masain pasal a nei khe ta a; huan, puanin a tuama, khualbuka a tak louh jiak un gan an piakna ah a sial hi.
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
8Huan, huai gam mah ah belam chingmite a om ua, gamlak ah janin a belam uh a ching ua.
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
9Huan, Toupa angel khat a kiang uah a hongding a, Toupa thupinain a kim uh a tanvak a; huchiin a lauta mahmah ua.
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
10Huan, angelin a kiang uah, Lau kei unla, ngai un, mi chih adingin tanchin hoih kipahhuai mahmah ka hontut ahi.
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
11Tuniin nou adingin David khua ah Hondampa a piangta, amah Kris Toupa ahi.
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
12Huan, hiai nou adingin chiamtehna ding ahi; naungek puana tuam, gan an piakna kuanga lum na mu ding uh, a chi a.
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
13Huan, angel kiangah vana mipi hon a hongom khawm guih ua, Pathian a phat ua.
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
14Tungnungpen ah Pathian thupi henla, leitunga a kipahpih mahmah mihingte lakah lemthu leng hen, a chi uhi.
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
15Huan, hichi ahia, angelten vana a paisan tak un, belam chingmiten, Tun ah Bethlehem kho phain pai lehang, Toupan thu a honhilh hongtung tuh i en ding uh, a kichi ua.
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
16Huchiin, a pai mengmeng ua, Mari toh, Joseph toh, gan an piakna kuanga naungek lum toh a vamu ua.
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
17Huan, a vamuh un a naungek tanchin angelin a hilh tuh a gen thangta uh.
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
18Huan, a za peuhmahin belam chingmite thugen lamdang a sa mahmah uh.
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
19Mariin bel thugen tengteng a lungtangin a ngaihtuah a, a vom gige a.
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
20Huan, belam chingmiten angel hilh bang ngeia bangkim a muh ua a jak jiak un, Pathian pahtawi leh phat kawm jelin a kik nawnta ua.
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
21Huan, a zek sumna ding ni giat a hongchinin, a min din, sula a om ma hima angelin a saksa, Jesu a sa uh.
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
22Huan, Mosi dan banga a kisiansakna ni uh a hongtunin, Jerusalem khua ah amah a vatonpih tou ua, Toupa kianga amah lan dingin.
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
23(Toupa thu a, ta pasal sul hong peuhmah Toupa adinga seh a chi ding uh, chia gelh bangin),
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
24Toupa Dan thua gen banga vakhu kop khat hiam vapal nou nih hiam kithoihna lan dingin.
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
25Huan, ngai in, Jerusalem khua ah mi khat a min Sumeon a om a; huai mi tuh mi diktat tak leh Pathian limsak tak ahia, Israelte khamuanpa ding a ngak ngitnget a, a tungah Kha Siangthou a om hi.
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
26Huan, Toupa Kris a muh masiah jaw a si kei ding chih Kha Siangthouin a na thei sak him ahi.
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
27Huan, Kha theihsakin Pathian biakin ah a valuta; naungek Jesu tuh a nu leh a pan Dan ngeina banga a tunga hihsak dinga a honpi lut lai un,
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
28aman a na-angpoma, Pathian a phata,
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
29Toupa, tun ah na thu bang jelin, na sikha khamuang takin na pai sak dinga:
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
30Na hotdamna ka mitin a muhtak jiakin,
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
31Huai mi chih muha na bawltak tuh;
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
32Jentelte kianga kilakna vak leh na mi Israelte thupina ding, a chi hi.
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
33Huan, naungek thu a gen tuh a nu leh a pan lamdang a sa mahmah ua.
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
34Huan, Sumeonin amau a vual jawla, a nu Mari kiangah, Ngai in, hiai naupang Israel laka mi tampi pukna ding leh dinkhiakna dinga seh ahi, gensiata om chiamtehna hi dingin leng.
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
35(A hi, nang lungtang leng temsauin a dawt pailet ding a) huchia mi tampiin a lungtang ua a ngaihtuahte uh a latna dingin, a chi hi.
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
36Huan, mi khat, a min, Anna, jawlnei, Phanuel Tanu, Asher nama mi a oma; amah tuh tek tak ahi a, a nungak tawp nung siah a pasal kiangah kum sagih a oma,
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
37huan, kum sawmgiat leh kum li hial a methaia, aman tuh Pathian biakin pai san louin a sun a janin anngawl kawma thumin Pathian a be jel.
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
38Huan, huchihlaitakin amah a hongpaia, Pathian kiangah kipahthu a gena, Jerusalem tatna lamen peuhmahte kiangah Jesu tanchin a gen hi.
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
39Huan, Toupa dan jela thil tengteng a hih zoh un, Galili gama, amau khua Nazaret ah a kik nawnta uh.
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
40Huan, naungek a hongkhang lian deuhdeuha, a honghat hiaihiaia, pilnain a dimtaa, Pathian deihsakna tuh a tungah a omta hi.
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
41Huan, kum tengin, Paikan Ankuanglui hunin, a nu leh a pa Jerusalem khuaah a hoh jel ua.
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
42Huan, amah tuh kum sawm leh kum nih a hihin dan ngeinain a hoh tou ua.
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
43Huan, ankuanglui akikhita a kik nawn lai un, naupang Jesun Jerusalem khuaah a om san a. A nu leh pan a theikei ua,
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
44huchiin a pawl lak ua om hi nanteh a chi ua, ni khat lam a pai khin ua, a sanggamte uh leh a meltheihte uh lakah a zong uh.
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
45Huan, a muh louh jiak un zong kawmkawmin Jerusalem khuaah a kik nawnta ua.
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
46Huan, hichi ahi a, ni thum nungin, Pathian biakin ah, sinsakmite laka tu a, a thu uh na ngaikhiaa, amau thu dongin, a vamuta ua.
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
47Huan, a thu za peuhin a theihdan leh a dawndan lamdang a sa mahmah uh.
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
48Huan, a nu leh a pan amah a muh un, lamdang a sa mahmah ua: huan, a nun, a kiangah, Ta aw, bangdia hichibanga honhih na hia? Ngai in, na pa leh ken lungkham takin kon zong uh, a chi a.
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
49Huan, aman a kiang uah, Bangdia honzong na hi ua? ka Pa ina ka om ding na theikei ua hia? a chi a.
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
50Huan, a kiang ua a thugen tuh a theisiam kei uhi.
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
51Huan, amau a jui suka, Nazaret khua a hongtung a, a thu uh mangin a oma. Huan, a nun huai thil tengteng tuh a lungtang ah a vom gige a.Huan, Jesu tuh a pil deuhdeuha, a honglian hiaihiaia, Pathian leh mihing deihsakin a om deuhdeuhta.
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
52Huan, Jesu tuh a pil deuhdeuha, a honglian hiaihiaia, Pathian leh mihing deihsakin a om deuhdeuhta.