1Yesu alipokuwa anatoka Hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake alimwambia, "Mwalimu, tazama jinsi mawe haya na majengo haya yalivyo ya ajabu!"
1Huan, Pathian biakina kipan a pai khiak laiin, a nungjuite laka mi khatin a kiangah, Sinsakpa, en dih, a suang leh a in khawng thupi mahmah hi a, a chi a.
2Yesu akamwambia, "Je, unayaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitabomolewa."
2Huan, Jesun, a kiangah, Hiai in thupi tak na mu maw? hihchip louha, suang kichiang himhim hiaiah a om kei ding, a chi a.
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni akielekea Hekalu, Petro, Yakobo, Yohane na Andrea wakamwuliza kwa faragha,
3Huan, Oliv tanga Pathian biakin jawna a tut laiin, Peter, Jakob, Johan leh Andru ten a kiangah,
4"Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya karibu yatimizwe?"
4Huaite chikchiangin a hongom dia? huai tengteng a tunding chiangin chiamtehna bang a om dia: honhilh in, chiin a sim dot ua.
5Yesu akaanza kuwaambia, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5Huan, Jesun a kiang uah, Kuamahin honkhem louhna ding un, pilvang un.
6Maana wengi watakuja wakilitumia jina langu, wakisema, Mimi ndiye! nao watawapotosha watu wengi.
6Mi tampi, Kris tuh ka hi, chiin, keimah min louin a hong ding uh, mi tampi a khem ding uh.
7Mtakaposikia juu ya vita na fununu za vita, msifadhaike. Mambo hayo lazima yatokee, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7Huan, kidou thu leh kidou thuthang khawng na jak hun chiang un mangbang kei un; huaite hongtung ding him ahi uh; himahleh, tawpna jaw ahi nai ta-dih kei ding.
8Taifa moja litapigana na taifa lingine; utawala mmoja utapigana na utawala mwingine; kila mahali kutakuwa na mitetemeko ya ardhi na njaa. Mambo haya ni kama tu maumivu ya kwanza ya kujifungua mtoto.
8Nam tuam leh nam tuam a kidou ding ua, gam tuam leh gam tuam a kidou ding ua; mun tuamtuam ah jin a ling dia; kial a ke dia. Huai tuh nauvei kipatna ahi.
9"Lakini ninyi jihadharini. Maana watu watawapelekeni mahakamani, na kuwapigeni katika masunagogi. Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu ili mpate kunishuhudia kwao.
9Himahleh, pilvang un; vaihawmmite a honmansak ding ua; kikhopnain khawngah a honvo ding ua; keimah jiakin gam ukte leh kumpipate ma ah theihpihna pe ding na hongding ding uh.
10Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.
10Huan, Tanchin Hoih tuh nam tengteng kianga hilh masak ding ahi.
11Nao watakapowatieni nguvuni na kuwapeleka mahakamani, msiwe na wasiwasi juu ya yale mtakayosema; saa ile itakapofika, semeni chochote mtakachopewa, maana si ninyi mtakaosema, bali Roho Mtakatifu.
11Huan, a honpi ua, a honmatsak hun chiang un, Bang ka gen de aw? chiin, ngaihtuah khol kei un; a hun taka theihsaka naom peuh uh, huai ngeingei gen jaw un; a genpen jaw noumau na hi kei ding uhi, Kha Siangthou ahi zo ding.
12Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae; watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
12Huan, hihlup dingin unaupa leh unaupa a kimansak ding ua, pain leng tapa a mansak ding; taten leng a nu leh pate uh a dou ding uh, a hihlum sak ding uh.
13Watu wote watawachukieni ninyi kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.
13Keimah min jiakin mi tengteng huat na hi ding uh; himahleh, a tawp phaa thuakpa, huai mi mah tuh hotdamin a om ding.
14"Mtakapoona Chukizo Haribifu limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake!) Hapo watu walioko Yudea wakimbilie milimani.
14Himahleh, hihmangbangpa kihhuai a din louhna dinga ding na muh chiang un, (a sim peuhin a omdan thei heh) huai hun chiangin Judia gama omte tangsang ah taimang uheh;
15Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.
15huan, in tunga om kum kei heh; a ina banghiam om tuh dingin zong lut sam kei heh;
16Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
16huan, lou-a om a puan tuh dingin kik nawn kei heh.
17Ole wao waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
17Huai niin gaite leh naunou pomte tung a gik ding.
18Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.
18Huan, huaite phalbia a hongtun louhna dingin thum un.
19Maana wakati huo kutakuwa na dhiki ambayo haijatokea tangu Mungu alipoumba ulimwengu mpaka leo, wala haitatokea tena.
19Huai nite banga gimthuakna thupi himhim Pathian bawl leilungpian tunga kipan tutanin a om ngei nai keia, chikchiangmahin a hongom ngei nawn kei ding hi.
20Kama Bwana asingepunguza siku hizo, hakuna binadamu ambaye angeokolewa. Lakini kwa ajili ya wateule wake, Bwana amezipunguza siku hizo.
20Huan, Toupan huai nite hihtom keileh mi hing himhim hingin a pawt kei ding uh; himahleh, mi tel, a sehte jiakin nite tuh a hih tom a.
21"Basi mtu akiwaambieni, Tazama, Kristo yupo hapa! au Yupo pale! msimsadiki.
21Huan, huai hun chiangin, kuapeuhin na kiang ua, En dih uh: Kris tuh hiailai ah a om, a hihkeileh, En dih uh: hua laiah, hiam a chih uh leh, um kei un;
22Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana.
22Kris takloute leh jawlnei takloute a hongpawt ding uh ahi ngala, huaiten, chiamtehna leh thillamdang a hih ding uh, hithei lehouh, telte nangawn a khem theihna ding un.
23Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.
23Nou jaw pilvang un, ngai dih uh, bangkim ka honhilh khol khin ahi.
24"Basi, siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza na mwezi hautaangaza.
24Himahleh, huai nitein, huai gimthuakna khitin, ni hihmialin a om dinga, kha a vak nawnta kei dia.
25Nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
25Van akipanin aksite a hongke ding ua, vana thilhihtheihna omte hihlinin a om ding uh.
26Hapo watamwona Mwana wa Mtu akija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu.
26Huai hun chiangin Mihing Tapa Thilhihtheihna leh thupina lianpi toh mei laka hongpai a mu ding uh.
27Kisha atawatuma malaika wake; atawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
27Huai hun chiangin angelte a sawl khe dia, a telte lei ningli a pat-lei tawp akipana van tawp pha in a khawm khawm ding uh.
28"Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
28Huchiin, theipi kungah a gentehna thu zil un: ahiang a hongnou a, a nah a hong selin nipi a nai chih na thei uh.
29Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo hayo yakitendeka, jueni kwamba Mwana wa Mtu yuko karibu sana.
29Huchi bangmahin, nou leng, huaite a hongtung na muh hun chiang un, amah a hongnaita a, kongkhak bul mahmah ah a om chih, thei un.
30Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
30Chihtaktakin ka honhilh ahi, huai tengteng a tunkim masiah tulai khangthakte a mang kei ding uh.
31Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
31Lei leh van a mang dia, ka thu a hihleh a mang kei ding.
32"Lakini hakuna mtu ajuaye siku au saa hiyo itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye.
32Himahleh, huai ni leh a dak thu Pa kia loungal kuamahin, vana angelten leng, Tapain leng a theikei uh.
33Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.
33Pilvang unla, kiging gigea omin thum un; a hun lah na thei ngal kei ua.
34Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia mlinzi wa mlango awe macho.
34Mi, a in pai sana, a sikhate thu nei saka, a nasep ding uh pe chiata, kongkhakveng leng kigin ding thu pe phota, gam danga vatam bang ahi.
35Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.
35Huaijiakin kiging gigein om un, inneipa hong ding hun, nitak lam hia, jan ah hia, akkhuanin hia, jingin hia hi ding chih na thei ngal kei ua;
36Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.
36Huchilou injaw, hongpai guih khaleh ihmuin a honmu khading.Huan, na kiang ua ka gen tuh mi tengteng kianga ka gen ahi, Kiging gigein om un, a chita a.
37Ninayowaambieni ninyi, nawaambia wote: Kesheni!"
37Huan, na kiang ua ka gen tuh mi tengteng kianga ka gen ahi, Kiging gigein om un, a chita a.