1Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
1ܦܛܪܘܤ ܫܠܝܚܐ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܠܓܒܝܐ ܘܬܘܬܒܐ ܕܙܪܝܥܝܢ ܒܦܢܛܘܤ ܘܒܓܠܛܝܐ ܘܒܩܦܘܕܩܝܐ ܘܒܐܤܝܐ ܘܒܒܝܬܘܢܝܐ ܀
2Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
2ܐܝܠܝܢ ܕܐܬܓܒܝܘ ܒܡܩܕܡܘܬ ܝܕܥܬܗ ܕܐܠܗܐ ܐܒܐ ܒܩܕܝܫܘܬܐ ܕܪܘܚܐ ܕܢܗܘܘܢ ܠܡܫܡܥܬܐ ܘܠܪܤܤ ܕܡܗ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܛܝܒܘܬܐ ܘܫܠܡܐ ܢܤܓܐ ܠܘܬܟܘܢ ܀
3Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
3ܡܒܪܟ ܗܘ ܐܠܗܐ ܐܒܘܗܝ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܗܘ ܕܒܚܢܢܗ ܤܓܝܐܐ ܐܘܠܕܢ ܡܢ ܕܪܝܫ ܒܩܝܡܬܗ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܠܤܒܪܐ ܕܚܝܐ ܀
4na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
4ܘܠܝܪܬܘܬܐ ܕܠܐ ܡܬܚܒܠܐ ܘܠܐ ܡܬܛܢܦܐ ܘܠܐ ܚܡܝܐ ܗܝ ܕܡܛܝܒܐ ܠܟܘܢ ܒܫܡܝܐ ܀
5Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
5ܟܕ ܢܛܝܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܚܝܠܐ ܕܐܠܗܐ ܘܒܗܝܡܢܘܬܐ ܠܚܝܐ ܕܡܛܝܒܝܢ ܕܢܬܓܠܘܢ ܠܙܒܢܐ ܐܚܪܝܐ ܀
6Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
6ܕܒܗܘܢ ܬܚܕܘܢ ܠܥܠܡ ܐܦܢ ܒܗܢܐ ܙܒܢܐ ܩܠܝܠ ܡܬܬܥܝܩܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܢܤܝܘܢܐ ܡܫܚܠܦܐ ܕܥܕܝܢ ܥܠܝܟܘܢ ܀
7Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
7ܐܝܟܢܐ ܕܒܘܚܪܢܐ ܕܗܝܡܢܘܬܟܘܢ ܢܬܚܙܐ ܕܡܝܬܪ ܡܢ ܕܗܒܐ ܤܢܝܢܐ ܕܐܬܒܩܝ ܒܢܘܪܐ ܠܬܫܒܘܚܬܐ ܘܠܐܝܩܪܐ ܘܠܩܘܠܤܐ ܒܓܠܝܢܗ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
8Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
8ܗܘ ܕܠܐ ܚܙܝܬܘܢܝܗܝ ܘܡܚܒܝܢ ܐܢܬܘܢ ܠܗ ܘܒܗܝܡܢܘܬܗ ܪܘܙܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܚܕܘܬܐ ܡܫܒܚܬܐ ܕܠܐ ܡܬܡܠܠܐ ܀
9kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
9ܕܬܩܒܠܘܢ ܦܘܪܥܢܐ ܕܗܝܡܢܘܬܟܘܢ ܚܝܐ ܕܢܦܫܬܟܘܢ ܀
10Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
10ܗܢܘܢ ܚܝܐ ܕܥܩܒܘ ܗܘܘ ܥܠܝܗܘܢ ܢܒܝܐ ܟܕ ܐܬܢܒܝܘ ܥܠ ܛܝܒܘܬܐ ܕܥܬܝܕܐ ܗܘܬ ܕܬܬܝܗܒ ܠܟܘܢ ܀
11Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
11ܘܒܨܘ ܕܒܐܝܢܐ ܙܒܢܐ ܡܚܘܝܐ ܘܡܤܗܕܐ ܪܘܚܗ ܕܡܫܝܚܐ ܕܥܡܪܐ ܒܗܘܢ ܕܥܬܝܕܝܢ ܚܫܘܗܝ ܕܡܫܝܚܐ ܘܬܫܒܘܚܬܗ ܕܡܢ ܒܬܪܟܢ ܀
12Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
12ܘܐܬܓܠܝ ܠܗܘܢ ܟܠ ܕܒܨܝܢ ܗܘܘ ܡܛܠ ܕܠܘ ܠܢܦܫܗܘܢ ܒܥܝܢ ܗܘܘ ܐܠܐ ܠܢ ܕܝܠܢ ܡܬܢܒܝܢ ܗܘܘ ܐܝܠܝܢ ܕܗܫܐ ܐܬܓܠܝ ܠܟܘܢ ܒܝܕ ܐܝܠܝܢ ܕܤܒܪܢܟܘܢ ܒܪܘܚܐ ܕܩܘܕܫܐ ܕܐܫܬܕܪ ܡܢ ܫܡܝܐ ܕܒܗܝܢ ܒܗܠܝܢ ܡܬܪܓܪܓܝܢ ܐܦ ܡܠܐܟܐ ܕܢܕܝܩܘܢ ܀
13Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
13ܡܛܠ ܗܢܐ ܚܙܘܩܘ ܚܨܐ ܕܬܪܥܝܬܟܘܢ ܘܐܬܬܥܝܪܘ ܓܡܝܪܐܝܬ ܘܤܒܪܘ ܥܠ ܚܕܘܬܐ ܕܐܬܝܐ ܠܟܘܢ ܒܓܠܝܢܗ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
14Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
14ܐܝܟ ܒܢܝܐ ܡܫܬܡܥܢܐ ܘܠܐ ܬܫܬܘܬܦܘܢ ܬܘܒ ܠܪܓܝܓܬܟܘܢ ܩܕܡܝܬܐ ܐܝܠܝܢ ܕܪܓܝܢ ܗܘܝܬܘܢ ܕܠܐ ܒܝܕܥܬܐ ܀
15Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
15ܐܠܐ ܗܘܘ ܩܕܝܫܝܢ ܒܟܠܗܘܢ ܗܘܦܟܝܟܘܢ ܐܝܟ ܕܩܕܝܫ ܗܘ ܡܢ ܕܩܪܟܘܢ ܀
16Maandiko yasema: "Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu."
16ܡܛܠ ܕܟܬܝܒ ܕܗܘܝܬܘܢ ܩܕܝܫܝܢ ܐܝܟܢܐ ܕܐܦ ܐܢܐ ܩܕܝܫ ܐܢܐ ܀
17Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
17ܘܐܢ ܗܘ ܕܐܒܐ ܩܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܗܘ ܕܠܝܬ ܩܕܡܘܗܝ ܡܤܒ ܒܐܦܐ ܘܕܐܢ ܠܟܠܢܫ ܐܝܟ ܥܒܕܘܗܝ ܒܕܚܠܬܐ ܐܬܕܒܪܘ ܒܙܒܢܐ ܗܢܐ ܕܬܘܬܒܘܬܟܘܢ ܀
18Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
18ܟܕ ܝܕܥܝܢ ܐܢܬܘܢ ܕܠܐ ܒܟܤܦܐ ܕܒܠܐ ܘܠܐ ܒܕܗܒܐ ܐܬܦܪܩܬܘܢ ܡܢ ܥܒܕܝܟܘܢ ܤܪܝܩܐ ܗܢܘܢ ܕܩܒܠܬܘܢ ܡܢ ܐܒܗܝܟܘܢ ܀
19bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
19ܐܠܐ ܒܕܡܐ ܝܩܝܪܐ ܕܐܡܪܐ ܕܡܘܡܐ ܘܛܘܠܫܐ ܠܝܬ ܒܗ ܕܐܝܬܘܗܝ ܡܫܝܚܐ ܀
20Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
20ܗܘ ܕܡܩܕܡ ܗܘܐ ܦܪܝܫ ܠܗܕܐ ܡܢ ܩܕܡ ܬܪܡܝܬܗ ܕܥܠܡܐ ܘܐܬܓܠܝ ܒܐܚܪܝܬܗܘܢ ܕܙܒܢܐ ܡܛܠܬܟܘܢ ܀
21Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
21ܐܝܠܝܢ ܕܒܐܝܕܗ ܗܝܡܢܬܘܢ ܒܐܠܗܐ ܗܘ ܕܐܩܝܡܗ ܡܢ ܒܝܬ ܡܝܬܐ ܘܝܗܒ ܠܗ ܫܘܒܚܐ ܕܗܝܡܢܘܬܟܘܢ ܘܤܒܪܟܘܢ ܢܗܘܐ ܥܠ ܐܠܗܐ ܀
22Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
22ܟܕ ܢܗܘܝܢ ܩܕܝܫܢ ܢܦܫܬܟܘܢ ܒܡܫܬܡܥܢܘܬܗ ܕܫܪܪܐ ܘܢܗܘܝܢ ܡܠܝܢ ܚܘܒܐ ܕܠܐ ܡܤܒ ܒܐܦܐ ܕܡܢ ܠܒܐ ܕܟܝܐ ܘܓܡܝܪܐ ܬܗܘܘܢ ܡܚܒܝܢ ܚܕ ܠܚܕ ܀
23Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele.
23ܐܝܟ ܐܢܫܐ ܕܡܢ ܕܪܝܫ ܐܬܝܠܕܬܘܢ ܠܐ ܡܢ ܙܪܥܐ ܕܒܠܐ ܐܠܐ ܡܢ ܐܝܢܐ ܕܠܐ ܒܠܐ ܒܡܠܬܐ ܚܝܬܐ ܕܐܠܗܐ ܕܩܝܡܐ ܠܥܠܡ ܀
24Kama Maandiko yasemavyo: "Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
24ܡܛܠ ܕܟܠ ܒܤܪ ܥܡܝܪܐ ܘܟܠܗ ܝܐܝܘܬܗ ܐܝܟ ܥܘܦܝܐ ܕܚܩܠܐ ܝܒܫ ܥܡܝܪܐ ܘܚܡܐ ܥܘܦܝܐ ܀
25Lakini neno la Bwana hudumu milele." Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu.
25ܘܡܠܬܗ ܕܐܠܗܢ ܩܝܡܐ ܠܥܠܡܝܢ ܘܗܕܐ ܗܝ ܡܠܬܐ ܗܝ ܕܐܤܬܒܪܬܘܢ ܀