Swahili: New Testament

Syriac: NT

1 Timothy

4

1Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
1ܪܘܚܐ ܕܝܢ ܦܫܝܩܐܝܬ ܐܡܪܐ ܕܒܙܒܢܐ ܐܚܪܝܐ ܢܦܪܩܘܢ ܐܢܫ ܐܢܫ ܡܢ ܗܝܡܢܘܬܐ ܘܢܐܙܠܘܢ ܒܬܪ ܪܘܚܐ ܛܥܝܬܐ ܘܒܬܪ ܝܘܠܦܢܐ ܕܫܐܕܐ ܀
2Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
2ܗܠܝܢ ܕܒܐܤܟܡܐ ܕܓܠܐ ܡܛܥܝܢ ܘܡܡܠܠܝܢ ܟܕܒܘܬܐ ܘܟܘܝܢ ܒܬܐܪܬܗܘܢ ܀
3Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
3ܘܟܠܝܢ ܠܡܙܕܘܓܘ ܘܡܦܪܩܝܢ ܡܢ ܡܐܟܠܬܐ ܐܝܠܝܢ ܕܐܠܗܐ ܒܪܐ ܐܢܝܢ ܠܚܘܫܚܐ ܘܠܬܘܕܝܬܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܡܗܝܡܢܝܢ ܘܝܕܥܝܢ ܫܪܪܐ ܀
4Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
4ܡܛܠ ܕܟܠ ܕܒܪܐ ܠܐܠܗܐ ܫܦܝܪ ܗܘ ܘܠܝܬ ܡܕܡ ܕܡܤܠܝ ܐܢ ܒܬܘܕܝܬܐ ܢܬܢܤܒ ܀
5kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
5ܡܬܩܕܫ ܓܝܪ ܒܡܠܬܐ ܕܐܠܗܐ ܘܒܨܠܘܬܐ ܀
6Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
6ܗܠܝܢ ܐܢ ܬܗܘܐ ܡܠܦ ܠܐܚܝܟ ܡܫܡܫܢܐ ܛܒܐ ܬܗܘܐ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܟܕ ܡܬܪܒܐ ܐܢܬ ܒܡܠܐ ܕܗܝܡܢܘܬܐ ܘܒܝܘܠܦܢܐ ܛܒܐ ܕܝܠܝܦ ܐܢܬ ܀
7Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
7ܡܢ ܫܘܥܝܬܐ ܕܝܢ ܦܟܝܗܬܐ ܕܤܒܬܐ ܐܫܬܐܠ ܘܕܪܫ ܢܦܫܟ ܒܟܐܢܘܬܐ ܀
8Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
8ܕܘܪܫܐ ܓܝܪ ܕܦܓܪܐ ܙܒܢܐ ܗܘ ܙܥܘܪܐ ܡܘܬܪ ܟܐܢܘܬܐ ܕܝܢ ܒܟܠ ܡܕܡ ܡܘܬܪܐ ܘܐܝܬ ܠܗ ܫܘܘܕܝܐ ܕܚܝܐ ܕܙܒܢܐ ܗܢܐ ܘܕܥܬܝܕ ܀
9Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
9ܡܗܝܡܢܐ ܗܝ ܡܠܬܐ ܘܫܘܝܐ ܗܝ ܠܡܩܒܠܘܬܗ ܀
10Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
10ܡܛܠ ܗܕܐ ܗܘ ܓܝܪ ܠܐܝܢܢ ܘܡܬܚܤܕܝܢܢ ܕܡܤܒܪܝܢܢ ܒܐܠܗܐ ܚܝܐ ܕܐܝܬܘܗܝ ܡܚܝܢܐ ܕܒܢܝܢܫܐ ܟܠܗܘܢ ܝܬܝܪܐܝܬ ܕܡܗܝܡܢܐ ܀
11Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
11ܗܠܝܢ ܐܠܦ ܘܦܩܕ ܀
12Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
12ܘܠܐ ܐܢܫ ܢܒܤܐ ܥܠ ܛܠܝܘܬܟ ܐܠܐ ܗܘܝ ܕܡܘܬܐ ܠܡܗܝܡܢܐ ܒܡܠܬܐ ܘܒܗܘܦܟܐ ܘܒܚܘܒܐ ܘܒܗܝܡܢܘܬܐ ܘܒܕܟܝܘܬܐ ܀
13Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
13ܥܕ ܐܬܐ ܐܢܐ ܐܬܚܦܛ ܒܩܪܝܢܐ ܘܒܒܥܘܬܐ ܘܒܝܘܠܦܢܐ ܀
14Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
14ܘܠܐ ܬܒܤܐ ܒܡܘܗܒܬܐ ܕܐܝܬ ܒܟ ܗܝ ܕܐܬܝܗܒܬ ܠܟ ܒܢܒܝܘܬܐ ܘܒܤܝܡ ܐܝܕܐ ܕܩܫܝܫܘܬܐ ܀
15Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
15ܒܗܠܝܢ ܐܬܗܓܐ ܘܒܗܝܢ ܗܘܝ ܕܬܬܝܕܥ ܠܟܠܢܫ ܕܠܩܕܡܝܟ ܐܬܐ ܐܢܬ ܀
16Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.
16ܘܐܙܕܗܪ ܒܢܦܫܟ ܘܒܝܘܠܦܢܟ ܘܚܡܤܢ ܒܗܘܢ ܟܕ ܗܠܝܢ ܓܝܪ ܬܥܒܕ ܢܦܫܟ ܬܚܐ ܘܠܐܝܠܝܢ ܕܫܡܥܝܢ ܠܟ ܀