Swahili: New Testament

Syriac: NT

2 Timothy

3

1Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu.
1ܗܕܐ ܕܝܢ ܗܘܝܬ ܝܕܥ ܕܒܝܘܡܬܐ ܐܚܪܝܐ ܢܐܬܘܢ ܙܒܢܐ ܩܫܝܐ ܀
2watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu;
2ܘܢܗܘܘܢ ܒܢܝܢܫܐ ܪܚܡܝ ܢܦܫܗܘܢ ܘܪܚܡܝ ܟܤܦܐ ܫܒܗܪܢܐ ܪܡܐ ܡܓܕܦܢܐ ܕܠܐܢܫܝܗܘܢ ܠܐ ܡܬܛܦܝܤܝܢ ܟܦܪܝ ܒܛܝܒܘܬܐ ܪܫܝܥܐ ܀
3watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema;
3ܐܟܠܝ ܩܪܨܐ ܡܫܥܒܕܝ ܠܪܓܬܐ ܒܥܪܝܪܝܐ ܤܢܝܝ ܛܒܬܐ ܀
4watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
4ܡܫܠܡܢܐ ܡܤܪܗܒܐ ܚܬܝܪܐ ܪܚܡܝ ܪܓܝܓܬܐ ܛܒ ܡܢ ܚܘܒܗ ܕܐܠܗܐ ܀
5Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.
5ܕܐܝܬ ܠܗܘܢ ܐܤܟܡܐ ܕܕܚܠܬ ܐܠܗܐ ܘܡܢ ܚܝܠܗ ܪܚܝܩܝܢ ܐܝܠܝܢ ܕܗܟܢܐ ܐܢܘܢ ܕܚܘܩ ܐܢܘܢ ܡܢܟ ܀
6Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina;
6ܡܢܗܘܢ ܐܢܘܢ ܓܝܪ ܗܠܝܢ ܕܡܚܠܕܝܢ ܒܝܬ ܒܬܐ ܘܫܒܝܢ ܢܫܐ ܕܛܡܝܪܢ ܒܚܛܗܐ ܘܡܬܕܒܪܢ ܠܪܓܝܓܬܐ ܡܫܚܠܦܬܐ ܀
7wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli.
7ܕܒܟܠܙܒܢ ܝܠܦܢ ܘܡܡܬܘܡ ܠܝܕܥܬܐ ܕܫܪܪܐ ܠܡܐܬܐ ܠܐ ܡܫܟܚܝܢ ܀
8Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose.
8ܐܝܟܢܐ ܕܝܢ ܕܝܢܤ ܘܝܡܒܪܝܤ ܩܡܘ ܠܘܩܒܠ ܡܘܫܐ ܗܟܢܐ ܐܦ ܗܢܘܢ ܩܝܡܝܢ ܠܘܩܒܠ ܫܪܪܐ ܐܢܫܐ ܕܡܚܒܠ ܪܥܝܢܗܘܢ ܘܤܠܝܢ ܡܢ ܗܝܡܢܘܬܐ ܀
9Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre.
9ܐܠܐ ܠܐ ܢܐܬܘܢ ܠܩܕܡܝܗܘܢ ܫܛܝܘܬܗܘܢ ܓܝܪ ܡܬܝܕܥܐ ܗܝ ܠܟܠܢܫ ܐܝܟܢܐ ܕܐܦ ܕܗܢܘܢ ܐܬܝܕܥܬ ܀
10Wewe lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu,
10ܐܢܬ ܕܝܢ ܐܬܝܬ ܒܬܪ ܝܘܠܦܢܝ ܘܒܬܪ ܕܘܒܪܝ ܘܒܬܪ ܨܒܝܢܝ ܘܒܬܪ ܗܝܡܢܘܬܝ ܘܒܬܪ ܢܓܝܪܘܬ ܪܘܚܝ ܘܒܬܪ ܚܘܒܝ ܘܒܬܪ ܡܤܝܒܪܢܘܬܝ ܀
11udhalimu na mateso yangu. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.
11ܘܒܬܪ ܪܕܝܦܘܬܝ ܘܒܬܪ ܚܫܝ ܘܝܕܥ ܐܢܬ ܐܝܠܝܢ ܤܝܒܪܬ ܒܐܢܛܝܟܝܐ ܘܒܐܝܩܢܘܢ ܘܒܠܘܤܛܪܐ ܐܝܕܐ ܪܕܝܦܘܬܐ ܤܝܒܪܬ ܘܡܢ ܟܠܗܝܢ ܦܨܝܢܝ ܡܪܝ ܀
12Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe.
12ܘܟܠܗܘܢ ܕܝܢ ܐܝܠܝܢ ܕܨܒܝܢ ܒܕܚܠܬ ܐܠܗܐ ܕܢܚܘܢ ܒܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܡܬܪܕܦܝܢ ܀
13Watu waovu na wadanyanyifu watazidi kuwa waovu zaidi na zaidi kwa kuwadanganya wengine na kudanganyika wao wenyewe.
13ܒܢܝܢܫܐ ܕܝܢ ܒܝܫܐ ܘܡܛܥܝܢܐ ܢܘܤܦܘܢ ܥܠ ܒܝܫܘܬܗܘܢ ܟܕ ܛܥܝܢ ܘܡܛܥܝܢ ܀
14Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa, ukaukubali kabisa. Unawajua wale waliokuwa walimu wako.
14ܐܢܬ ܕܝܢ ܩܘܐ ܒܐܝܠܝܢ ܕܝܠܦܬ ܘܐܫܬܪܪܬ ܝܕܥ ܐܢܬ ܓܝܪ ܡܢ ܡܢܘ ܝܠܦܬ ܀
15Unakumbuka kwamba tangu utoto wako umeyajua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu.
15ܘܕܡܢ ܛܠܝܘܬܟ ܤܦܪܐ ܩܕܝܫܐ ܝܠܝܦ ܐܢܬ ܕܡܫܟܚܝܢ ܕܢܚܟܡܘܢܟ ܠܚܝܐ ܒܗܝܡܢܘܬܐ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
16Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
16ܟܠ ܟܬܒ ܕܒܪܘܚܐ ܐܬܟܬܒ ܡܘܬܪܢܐ ܗܘ ܠܝܘܠܦܢܐ ܘܠܟܘܘܢܐ ܘܠܬܘܪܨܐ ܘܠܡܪܕܘܬܐ ܕܒܟܐܢܘܬܐ ܀
17ili mtu anayemtumikia Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila tendo jema.
17ܕܢܗܘܐ ܓܡܝܪ ܒܪܢܫܐ ܕܐܠܗܐ ܘܠܟܠ ܥܒܕ ܛܒ ܡܫܠܡܢ ܀