Swahili: New Testament

Syriac: NT

Acts

23

1Paulo aliwakodolea macho wale wanabaraza, halafu akaanza kusema, "Ndugu zangu, mpaka hivi leo nimekuwa nikiishi na dhamiri njema mbele ya Mungu."
1ܘܟܕ ܚܪ ܦܘܠܘܤ ܒܟܢܫܗܘܢ ܐܡܪ ܓܒܪܐ ܐܚܝ ܐܢܐ ܒܟܠ ܬܐܪܬܐ ܛܒܬܐ ܐܬܕܒܪܬ ܩܕܡ ܐܠܗܐ ܥܕܡܐ ܠܝܘܡܢܐ ܀
2Hapo Kuhani Mkuu Anania akaamuru wale waliokuwa wamesimama karibu na Paulo wampige kofi mdomoni.
2ܘܚܢܢܝܐ ܟܗܢܐ ܦܩܕ ܠܗܢܘܢ ܕܩܝܡܝܢ ܥܠ ܓܒܗ ܕܢܡܚܘܢܗ ܠܦܘܠܘܤ ܥܠ ܦܘܡܗ ܀
3Basi, Paulo akamwambia, "Mungu mwenyewe atakupiga kofi wewe uliye kama ukuta uliopakwa chokaa! Unawezaje kukaa hapo ili unihukumu kisheria na huku wewe mwenyewe unaivunja Sheria kwa kuamuru nipigwe?"
3ܘܦܘܠܘܤ ܐܡܪ ܠܗ ܥܬܝܕ ܗܘ ܐܠܗܐ ܕܢܡܚܝܟ ܐܤܬܐ ܡܚܘܪܬܐ ܘܐܢܬ ܝܬܒ ܐܢܬ ܕܐܢ ܐܢܬ ܠܝ ܐܝܟ ܕܒܢܡܘܤܐ ܟܕ ܥܒܪ ܐܢܬ ܥܠ ܢܡܘܤܐ ܘܦܩܕ ܐܢܬ ܕܢܡܚܘܢܢܝ ܀
4Watu waliokuwa wamesimama pale wakamwambia Paulo, "Unamtukana Kuhani Mkuu wa Mungu!"
4ܘܐܝܠܝܢ ܕܩܝܡܝܢ ܗܘܘ ܬܡܢ ܐܡܪܝܢ ܠܗ ܠܟܗܢܐ ܕܐܠܗܐ ܡܨܚܐ ܐܢܬ ܀
5Paulo akajibu, "Ndugu zangu, sikujua kama yeye ni Kuhani Mkuu. Maana Maandiko yasema hivi: Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako."
5ܐܡܪ ܠܗܘܢ ܦܘܠܘܤ ܠܐ ܝܕܥ ܗܘܝܬ ܐܚܝ ܕܟܗܢܐ ܗܘ ܟܬܝܒ ܗܘ ܓܝܪ ܕܠܪܫܐ ܕܥܡܟ ܠܐ ܬܠܘܛ ܀
6Wakati huo Paulo alikwisha tambua kwamba sehemu moja ya wanabaraza wale ilikuwa ni Masadukayo na nyingine Mafarisayo. Basi, alipaaza sauti yake mbele ya Baraza: "Ndugu zangu, mimi ni Mfarisayo, mwana wa Mfarisayo. Mimi nimeletwa mahakamani kwa kuwa ninatumaini kwamba wafu watafufuka."
6ܘܟܕ ܝܕܥ ܦܘܠܘܤ ܕܡܢܗ ܕܥܡܐ ܐܝܬܘܗܝ ܕܙܕܘܩܝܐ ܘܡܢܗ ܕܦܪܝܫܐ ܩܥܐ ܗܘܐ ܒܟܢܫܐ ܓܒܪܐ ܐܚܝ ܐܢܐ ܦܪܝܫܐ ܐܢܐ ܒܪ ܦܪܝܫܐ ܘܥܠ ܤܒܪܐ ܕܩܝܡܬܐ ܕܡܝܬܐ ܡܬܕܝܢ ܐܢܐ ܀
7Baada ya kusema hivyo, mzozo mkali ulitokea kati ya Mafarisayo na Masadukayo na mkutano ukagawanyika sehemu mbili.
7ܘܟܕ ܗܕܐ ܐܡܪ ܢܦܠܘ ܚܕ ܒܚܕ ܦܪܝܫܐ ܘܙܕܘܩܝܐ ܘܐܬܦܠܓ ܥܡܐ ܀
8Kisa chenyewe kilikuwa hiki: Masadukayo hushikilia kwamba wafu hawafufuki, hakuna malaika, na roho nazo hazipo. Lakini Mafarisayo husadiki hayo yote matatu.
8ܙܕܘܩܝܐ ܓܝܪ ܐܡܪܝܢ ܕܠܝܬ ܩܝܡܬܐ ܘܠܐ ܡܠܐܟܐ ܘܠܐ ܪܘܚܐ ܦܪܝܫܐ ܕܝܢ ܡܘܕܝܢ ܒܟܠܗܝܢ ܀
9Kelele ziliongezeka na baadhi ya walimu wa Sheria wa kikundi cha Mafarisayo walisimama na kutoa malalamiko yao kwa nguvu: "Hatuoni chochote kilicho kiovu katika mtu huyu; huenda ikawa kwamba roho au malaika ameongea naye."
9ܘܗܘܐ ܩܠܐ ܪܒܐ ܘܩܡܘ ܐܢܫܐ ܤܦܪܐ ܡܢ ܓܒܐ ܕܦܪܝܫܐ ܘܢܨܝܢ ܗܘܘ ܥܡܗܘܢ ܘܐܡܪܝܢ ܠܐ ܡܫܟܚܝܢܢ ܡܕܡ ܕܒܝܫ ܒܗܢܐ ܓܒܪܐ ܐܢ ܕܝܢ ܪܘܚܐ ܐܘ ܡܠܐܟܐ ܡܠܠ ܥܡܗ ܡܢܐ ܐܝܬ ܒܗ ܒܗܕܐ ܀
10Mzozo ulizidi kuwa mwingi hata mkuu wa jeshi akaogopa kwamba Paulo angeraruliwa vipandevipande. Kwa hiyo, aliwaamuru askari wake kuingia kati ya lile kundi, wamtoe Paulo na kumrudisha ndani ya ngome.
10ܘܟܕ ܗܘܐ ܫܓܘܫܝܐ ܪܒܐ ܒܝܢܬܗܘܢ ܕܚܠ ܗܘܐ ܟܠܝܪܟܐ ܕܠܡܐ ܢܦܫܚܘܢܗ ܠܦܘܠܘܤ ܘܫܠܚ ܠܪܗܘܡܝܐ ܕܢܐܬܘܢ ܢܚܛܦܘܢܗ ܡܢ ܡܨܥܬܗܘܢ ܘܢܥܠܘܢܗ ܠܡܫܪܝܬܐ ܀
11Usiku uliofuata, Bwana alisimama karibu na Paulo, akamwambia, "Jipe moyo! Umenishuhudia katika Yerusalemu, utafanya vivyo hivyo mjini Roma."
11ܘܟܕ ܗܘܐ ܠܠܝܐ ܐܬܚܙܝ ܠܗ ܡܪܢ ܠܦܘܠܘܤ ܘܐܡܪ ܠܗ ܐܬܚܝܠ ܡܛܠ ܕܐܝܟ ܕܐܤܗܕܬ ܥܠܝ ܒܐܘܪܫܠܡ ܗܟܢܐ ܥܬܝܕ ܐܢܬ ܕܐܦ ܒܪܗܘܡܐ ܬܤܗܕ ܀
12Kulipokucha, Wayahudi walifanya kikao cha faragha. Wakala kiapo: "Hatutakula wala kunywa mpaka tutakapokuwa tumekwisha muua Paulo."
12ܘܟܕ ܗܘܐ ܨܦܪܐ ܐܬܟܢܫܘ ܗܘܘ ܐܢܫܝܢ ܡܢ ܝܗܘܕܝܐ ܘܐܚܪܡܘ ܥܠܝܗܘܢ ܕܠܐ ܢܐܟܠܘܢ ܘܠܐ ܢܫܬܘܢ ܥܕܡܐ ܕܢܩܛܠܘܢܗ ܠܦܘܠܘܤ ܀
13Watu zaidi ya arobaini ndio waliokula njama kufanya hivyo.
13ܗܘܝܢ ܗܘܘ ܕܝܢ ܗܢܘܢ ܕܐܩܝܡܘ ܒܡܘܡܬܐ ܗܢܐ ܩܝܡܐ ܝܬܝܪ ܡܢ ܐܪܒܥܝܢ ܓܒܪܝܢ ܀
14Basi, walikwenda kwa makuhani wakuu na wazee, wakasema, "Sisi tumeapa kwamba hatutaonja chochote kwa vinywa vyetu mpaka hapo tutakapokuwa tumemuua Paulo.
14ܘܐܬܩܪܒܘ ܠܘܬ ܟܗܢܐ ܘܠܘܬ ܩܫܝܫܐ ܘܐܡܪܝܢ ܗܘܘ ܕܚܪܡܐ ܐܚܪܡܢ ܥܠܝܢ ܕܡܕܡ ܠܐ ܢܛܥܡ ܥܕܡܐ ܕܢܩܛܘܠ ܠܦܘܠܘܤ ܀
15Sasa basi, ninyi pamoja na Baraza tumeni ujumbe kwa mkuu wa jeshi ili amlete Paulo kwenu mkijisingizia kwamba mnataka kupata habari kamili zaidi juu yake. Tuko tayari kumuua hata kabla hajafika karibu."
15ܘܗܫܐ ܒܥܘ ܐܢܬܘܢ ܘܪܫܐ ܕܟܢܘܫܬܐ ܡܢ ܟܠܝܪܟܐ ܕܢܝܬܝܘܗܝ ܠܘܬܟܘܢ ܐܝܟ ܒܥܝܢ ܐܢܬܘܢ ܕܬܒܨܘܢ ܫܪܝܪܐܝܬ ܤܘܥܪܢܗ ܘܚܢܢ ܡܛܝܒܝܢܢ ܕܢܩܛܠܝܘܗܝ ܥܕܠܐ ܢܡܛܐ ܠܘܬܟܘܢ ܀
16Lakini mtoto wa kiume wa dada yake Paulo alisikia juu ya mpango huo; hivyo akaenda ndani ya ngome, akamjulisha Paulo juu ya njama hiyo.
16ܘܫܡܥ ܗܘܐ ܒܪ ܚܬܗ ܕܦܘܠܘܤ ܐܦܪܤܢܐ ܗܢܐ ܘܥܠ ܠܡܫܪܝܬܐ ܘܒܕܩ ܠܦܘܠܘܤ ܀
17Hapo Paulo akamwita mmoja wa askari, akamwambia, "Mchukue kijana huyu kwa mkuu wa jeshi; ana kitu cha kumwambia."
17ܘܫܕܪ ܦܘܠܘܤ ܩܪܐ ܠܚܕ ܡܢ ܩܢܛܪܘܢܐ ܘܐܡܪ ܠܗ ܐܘܒܠ ܠܥܠܝܡܐ ܗܢܐ ܠܘܬ ܟܠܝܪܟܐ ܐܝܬ ܠܗ ܓܝܪ ܡܕܡ ܕܢܐܡܪ ܠܗ ܀
18Askari akamchukua huyo kijana, akamwongoza mpaka kwa mkuu wa jeshi, akasema, "Yule mfungwa Paulo ameniita akaniomba nimlete kijana huyu kwako kwa maana ana jambo la kukwambia."
18ܘܕܒܪܗ ܩܢܛܪܘܢܐ ܠܥܠܝܡܐ ܘܐܥܠܗ ܠܘܬ ܟܠܝܪܟܐ ܘܐܡܪ ܦܘܠܘܤ ܐܤܝܪܐ ܩܪܢܝ ܘܒܥܐ ܡܢܝ ܕܐܝܬܐ ܗܢܐ ܥܠܝܡܐ ܠܘܬܟ ܕܐܝܬ ܠܗ ܡܕܡ ܕܢܐܡܪ ܠܟ ܀
19Mkuu wa jeshi alimshika huyo kijana mkono, akampeleka mahali pa faragha, akamwuliza, "Una nini cha kuniambia?"
19ܘܐܚܕܗ ܒܐܝܕܗ ܟܠܝܪܟܐ ܠܥܠܝܡܐ ܘܢܓܕܗ ܠܚܕ ܓܒܐ ܘܡܫܐܠ ܗܘܐ ܠܗ ܕܡܢܐ ܐܝܬ ܠܟ ܕܬܐܡܪ ܠܝ ܀
20Yeye akasema, "Wayahudi wamepatana wakuombe umpeleke Paulo Barazani wakijisingizia kwamba Baraza lingependa kupata habari kamili zaidi juu yake.
20ܘܐܡܪ ܠܗ ܥܠܝܡܐ ܝܗܘܕܝܐ ܐܬܚܫܒܘ ܕܢܒܥܘܢ ܡܢܟ ܕܬܚܬ ܠܦܘܠܘܤ ܡܚܪ ܠܟܢܫܗܘܢ ܐܝܟ ܨܒܝܢ ܡܕܡ ܝܬܝܪ ܕܢܐܠܦܘܢ ܡܢܗ ܀
21Lakini wewe usikubali kwa maana kuna watu zaidi ya arobaini walio tayari kumvamia. Wameapa kutokula wala kunywa mpaka watakapokuwa wamemuua. Sasa wako tayari, wanangojea tu uamuzi wako."
21ܐܢܬ ܗܟܝܠ ܠܐ ܬܬܛܦܝܤ ܠܗܘܢ ܗܐ ܓܝܪ ܝܬܝܪ ܡܢ ܐܪܒܥܝܢ ܓܒܪܝܢ ܡܢܗܘܢ ܢܛܪܝܢ ܠܗ ܒܟܡܐܢܐ ܘܐܚܪܡܘ ܥܠ ܢܦܫܗܘܢ ܕܠܐ ܢܐܟܠܘܢ ܘܠܐ ܢܫܬܘܢ ܥܕܡܐ ܕܢܩܛܠܘܢܗ ܘܗܐ ܡܛܝܒܝܢ ܘܡܩܘܝܢ ܠܫܘܘܕܝܟ ܀
22Mkuu wa jeshi alimwacha aende zake akimwonya asimwambie mtu yeyote kwamba amemletea habari hizo.
22ܘܫܪܝܗܝ ܟܠܝܪܟܐ ܠܥܠܝܡܐ ܟܕ ܦܩܕܗ ܕܐܢܫ ܠܐ ܢܕܥ ܕܗܠܝܢ ܒܕܩܬ ܠܝ ܀
23Basi, mkuu wa jeshi aliwaita askari wawili akawaambia, "Wekeni tayari askari mia mbili, wapanda farasi sabini na askari mia mbili wa mikuki, waende Kaisarea; muwe tayari kuondoka kabla ya saa tatu leo usiku.
23ܘܩܪܐ ܠܬܪܝܢ ܩܢܛܪܘܢܝܢ ܘܐܡܪ ܠܗܘܢ ܙܠܘ ܥܬܕܘ ܪܗܘܡܝܐ ܡܐܬܝܢ ܕܢܐܙܠܘܢ ܠܩܤܪܝܐ ܘܦܪܫܐ ܫܒܥܝܢ ܘܫܕܝܝ ܒܝܡܝܢܐ ܡܐܬܝܢ ܕܢܦܩܘܢ ܡܢ ܬܠܬ ܫܥܝܢ ܒܠܠܝܐ ܀
24Wekeni farasi kadhaa kwa ajili ya Paulo; mfikisheni salama kwa Felisi, mkuu wa mkoa."
24ܛܝܒܘ ܕܝܢ ܐܦ ܒܥܝܪܐ ܐܝܟ ܕܢܪܟܒܘܢ ܠܦܘܠܘܤ ܘܢܦܠܛܘܢܗ ܠܘܬ ܦܝܠܟܤ ܗܓܡܘܢܐ ܀
25Halafu mkuu huyo wa jeshi akaandika barua hivi:
25ܘܟܬܒ ܐܓܪܬܐ ܝܗܒ ܠܗܘܢ ܕܐܝܬ ܒܗ ܗܟܢܐ ܀
26"Mimi Klaudio Lusia ninakuandikia wewe Mheshimiwa Felisi, mkuu wa mkoa. Salamu!
26ܠܘܤܝܘܤ ܠܦܝܠܟܤ ܗܓܡܘܢܐ ܢܨܝܚܐ ܫܠܡ ܀
27"Wayahudi walimkamata mtu huyu na karibu wangemuua kama nisingalifahamishwa kwamba yeye ni raia wa Roma na hivyo nikaenda pamoja na askari nikamwokoa.
27ܠܓܒܪܐ ܗܢܐ ܐܚܕܘ ܝܗܘܕܝܐ ܐܝܟ ܕܢܩܛܠܘܢܗ ܘܩܡܬ ܐܢܐ ܥܡ ܪܗܘܡܝܐ ܘܦܪܩܬܗ ܟܕ ܝܠܦܬ ܕܪܗܘܡܝܐ ܗܘ ܀
28Nilimpeleka mbele ya Baraza lao kuu nikitaka kujua kisa cha mashtaka yao.
28ܘܟܕ ܒܥܐ ܗܘܝܬ ܠܡܕܥ ܥܠܬܐ ܕܡܛܠܬܗ ܪܫܝܢ ܗܘܘ ܠܗ ܐܚܬܬܗ ܠܟܢܫܗܘܢ ܀
29Niligundua kwamba mashtaka yenyewe yalihusu ubishi juu ya sehemu kadha wa kadha za Sheria yao na hivyo sikuona kwamba amefanya chochote kinachostahili auawe au afungwe gerezani.
29ܘܐܫܟܚܬ ܕܥܠ ܙܛܡܐ ܕܢܡܘܤܗܘܢ ܪܫܝܢ ܗܘܘ ܠܗ ܘܥܠܬܐ ܕܫܘܝܐ ܠܐܤܘܪܐ ܐܘ ܠܡܘܬܐ ܠܝܬ ܗܘܐ ܠܘܬܗ ܀
30Nilipofahamishwa kwamba Wayahudi walikuwa wamefanya njama za kumuua, niliamua kumleta kwako. Nikamwambia washtaki wake walete mashtaka yao mbele yako."
30ܘܟܕ ܐܬܒܕܩ ܠܝ ܢܟܠܐ ܒܟܡܐܢܐ ܕܥܒܕܘ ܥܠܘܗܝ ܝܗܘܕܝܐ ܡܚܕܐ ܫܕܪܬܗ ܠܘܬܟ ܘܦܩܕܬ ܠܩܛܓܪܢܘܗܝ ܕܢܐܬܘܢ ܘܢܐܡܪܘܢ ܥܡܗ ܩܕܡܝܟ ܗܘܝ ܚܠܝܡ ܀
31Basi, hao askari walimchukua Paulo kama walivyoamriwa; wakampeleka usiku uleule mpaka Antipatri.
31ܗܝܕܝܢ ܪܗܘܡܝܐ ܐܝܟ ܕܐܬܦܩܕܘ ܕܒܪܘܗܝ ܠܦܘܠܘܤ ܒܠܠܝܐ ܘܐܝܬܝܘܗܝ ܠܐܢܛܝܦܛܪܤ ܡܕܝܢܬܐ ܀
32Kesho yake askari wa miguu walirudi ngomeni, wakawaacha wale askari wapanda farasi waendelee na safari pamoja na Paulo.
32ܘܠܝܘܡܐ ܐܚܪܢܐ ܫܪܘ ܦܪܫܐ ܠܪܓܠܐ ܚܒܪܝܗܘܢ ܕܢܗܦܟܘܢ ܠܡܫܪܝܬܐ ܀
33Walipofika Kaisarea walimpa mkuu wa mkoa ile barua na kumweka Paulo chini ya mamlaka yake.
33ܘܐܝܬܝܘܗܝ ܠܩܤܪܝܐ ܘܝܗܒܘ ܐܓܪܬܐ ܠܗܓܡܘܢܐ ܘܐܩܝܡܘܗܝ ܩܕܡܘܗܝ ܠܦܘܠܘܤ ܀
34Felisi alipoisoma hiyo barua aliwauliza Paulo ametoka mkoa gani. Alipofahamishwa kwamba alikuwa ametoka mkoa wa Kilikia,
34ܘܟܕ ܩܪܐ ܐܓܪܬܐ ܡܫܐܠ ܗܘܐ ܠܗ ܕܡܢ ܐܝܕܐ ܗܘܦܪܟܝܐ ܐܝܬܘܗܝ ܘܟܕ ܝܠܦ ܕܡܢ ܩܝܠܝܩܝܐ ܀
35akasema, "Nitasikiliza kesi yako baada ya washtaki wako kufika." Kisha akaamuru Paulo awekwe chini ya ulinzi ndani ya ukumbi wa Herode.
35ܐܡܪ ܠܗ ܫܡܥ ܐܢܐ ܠܟ ܡܐ ܕܐܬܘ ܩܛܓܪܢܝܟ ܘܦܩܕ ܕܢܛܪܘܢܗ ܒܦܪܛܘܪܝܢ ܕܗܪܘܕܤ ܀