Swahili: New Testament

Syriac: NT

Colossians

4

1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
1ܡܪܝܐ ܥܒܕܘ ܫܘܝܘܬܐ ܘܟܐܢܘܬܐ ܠܘܬ ܥܒܕܝܟܘܢ ܘܗܘܝܬܘܢ ܝܕܥܝܢ ܕܐܦ ܠܟܘܢ ܐܝܬ ܗܘ ܡܪܐ ܒܫܡܝܐ ܀
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
2ܒܨܠܘܬܐ ܐܬܐܡܢܘ ܘܗܘܝܬܘܢ ܥܝܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܗ ܘܡܘܕܝܢ ܀
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
3ܘܡܨܠܝܢ ܐܦ ܥܠܝܢ ܕܐܠܗܐ ܢܦܬܚ ܠܢ ܬܪܥܐ ܕܡܠܬܐ ܠܡܡܠܠܘ ܐܪܙܐ ܕܡܫܝܚܐ ܕܡܛܠܬܗ ܐܤܝܪ ܐܢܐ ܀
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
4ܕܐܓܠܝܘܗܝ ܘܐܡܠܠܝܘܗܝ ܐܝܟܢܐ ܕܘܠܐ ܠܝ ܀
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
5ܒܚܟܡܬܐ ܗܠܟܘ ܠܘܬ ܒܪܝܐ ܘܙܒܢܘ ܩܐܪܤܟܘܢ ܀
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
6ܘܡܠܬܟܘܢ ܒܟܠܙܒܢ ܒܛܝܒܘܬܐ ܐܝܟ ܕܒܡܠܚܐ ܬܗܘܐ ܡܡܕܟܐ ܘܗܘܝܬܘܢ ܝܕܥܝܢ ܠܐܢܫ ܐܢܫ ܐܝܟܢܐ ܘܠܐ ܠܟܘܢ ܠܡܬܒܘ ܦܬܓܡܐ ܀
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
7ܡܕܡ ܕܠܘܬܝ ܕܝܢ ܢܘܕܥܟܘܢ ܛܘܟܝܩܘܤ ܐܚܐ ܚܒܝܒܐ ܘܡܫܡܫܢܐ ܡܗܝܡܢܐ ܘܟܢܬܢ ܒܡܪܝܐ ܀
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
8ܗܢܐ ܕܫܕܪܬ ܠܘܬܟܘܢ ܥܠܝܗ ܥܠ ܗܕܐ ܕܢܕܥ ܡܐ ܕܠܘܬܟܘܢ ܘܢܒܝܐ ܠܒܘܬܟܘܢ ܀
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
9ܥܡ ܐܢܤܝܡܘܤ ܐܚܐ ܡܗܝܡܢܐ ܘܚܒܝܒܐ ܗܘ ܕܐܝܬܘܗܝ ܡܢܟܘܢ ܗܢܘܢ ܢܘܕܥܘܢܟܘܢ ܡܕܡ ܕܠܘܬܢ ܀
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
10ܫܐܠ ܒܫܠܡܟܘܢ ܐܪܤܛܪܟܘܤ ܫܒܝܐ ܕܥܡܝ ܘܡܪܩܘܤ ܒܪ ܕܕܗ ܕܒܪܢܒܐ ܗܘ ܕܐܬܦܩܕܬܘܢ ܥܠܘܗܝ ܕܐܢ ܐܬܐ ܠܘܬܟܘܢ ܬܩܒܠܘܢܝܗܝ ܀
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
11ܘܝܫܘܥ ܗܘ ܕܡܬܩܪܐ ܝܘܤܛܘܤ ܗܠܝܢ ܕܐܝܬܝܗܘܢ ܡܢ ܓܙܘܪܬܐ ܘܗܢܘܢ ܒܠܚܘܕ ܥܕܪܘܢܝ ܒܡܠܟܘܬܗ ܕܐܠܗܐ ܘܗܢܘܢ ܗܘܘ ܠܝ ܒܘܝܐܐ ܀
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
12ܫܐܠ ܒܫܠܡܟܘܢ ܐܦܦܪܐ ܗܘ ܕܡܢܟܘܢ ܥܒܕܐ ܕܡܫܝܚܐ ܟܕ ܒܟܠܙܒܢ ܥܡܠ ܚܠܦܝܟܘܢ ܒܨܠܘܬܐ ܕܬܩܘܡܘܢ ܓܡܝܪܐ ܘܡܫܡܠܝܐ ܒܟܠܗ ܨܒܝܢܗ ܕܐܠܗܐ ܀
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
13ܤܗܕ ܐܢܐ ܓܝܪ ܥܠܘܗܝ ܕܛܢܢܐ ܤܓܝܐܐ ܐܝܬ ܠܗ ܚܠܦܝܟܘܢ ܘܚܠܦ ܗܢܘܢ ܕܒܠܕܝܩܝܐ ܘܕܒܐܝܪܦܘܠܝܤ ܀
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
14ܫܐܠ ܒܫܠܡܟܘܢ ܠܘܩܐ ܐܤܝܐ ܚܒܝܒܢ ܘܕܡܐ ܀
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
15ܫܐܠܘ ܒܫܠܡܐ ܕܐܚܐ ܕܒܠܕܝܩܝܐ ܘܕܢܘܡܦܐ ܘܕܥܕܬܐ ܕܒܒܝܬܗ ܀
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
16ܘܡܐ ܕܐܬܩܪܝܬ ܐܓܪܬܐ ܗܕܐ ܠܘܬܟܘܢ ܥܒܕܘ ܕܐܦ ܒܥܕܬܐ ܕܠܕܝܩܝܐ ܬܬܩܪܐ ܘܗܝ ܕܐܬܟܬܒܬ ܡܢ ܠܕܝܩܝܐ ܩܪܐܘܗ ܐܢܬܘܢ ܀
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
17ܘܐܡܪܘ ܠܐܪܟܝܦܘܤ ܕܐܙܕܗܪ ܒܬܫܡܫܬܐ ܗܝ ܕܩܒܠܬ ܒܡܪܢ ܕܬܗܘܐ ܡܫܡܠܐ ܠܗ ܀
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.
18ܫܠܡܐ ܗܢܐ ܒܐܝܕܐ ܕܝܠܝ ܕܦܘܠܘܤ ܗܘܝܬܘܢ ܥܗܕܝܢ ܠܐܤܘܪܝ ܛܝܒܘܬܐ ܥܡܟܘܢ ܐܡܝܢ ܀