1Mungu alituahidia kwamba tutaweza kupata pumziko hilo alilosema. Basi, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo.
1ܢܕܚܠ ܗܟܝܠ ܕܠܡܐ ܟܕ ܩܝܡ ܡܘܠܟܢܐ ܕܡܥܠܬܐ ܕܠܢܝܚܬܗ ܢܫܬܟܚ ܐܢܫ ܡܢܟܘܢ ܕܦܐܫ ܡܢ ܕܠܡܥܠ ܀
2Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
2ܐܦ ܚܢܢ ܓܝܪ ܐܤܬܒܪܢ ܐܝܟ ܕܐܦ ܗܢܘܢ ܐܠܐ ܠܐ ܐܘܬܪܬ ܐܢܘܢ ܠܗܢܘܢ ܡܠܬܐ ܕܫܡܥܘ ܡܛܠ ܕܠܐ ܡܡܙܓܐ ܗܘܬ ܒܗܝܡܢܘܬܐ ܠܗܢܘܢ ܕܫܡܥܘܗ ܀
3Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: "Nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko." Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
3ܥܐܠܝܢܢ ܕܝܢ ܠܢܝܚܬܐ ܚܢܢ ܐܝܠܝܢ ܕܗܝܡܢܢ ܐܝܟܢܐ ܕܝܢ ܐܡܪ ܐܝܟ ܕܝܡܝܬ ܒܪܘܓܙܝ ܕܠܐ ܢܥܠܘܢ ܠܢܝܚܬܝ ܕܗܐ ܥܒܕܘܗܝ ܕܐܠܗܐ ܡܢ ܫܘܪܝܗ ܕܥܠܡܐ ܗܘܘ ܀
4Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: "Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote."
4ܐܝܟ ܕܐܡܪ ܥܠ ܫܒܬܐ ܕܐܬܢܝܚ ܐܠܗܐ ܒܝܘܡܐ ܫܒܝܥܝܐ ܡܢ ܥܒܕܘܗܝ ܟܠܗܘܢ ܀
5Tena jambo hili lasemwa pia: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
5ܘܗܪܟܐ ܬܘܒ ܐܡܪ ܕܠܐ ܢܥܠܘܢ ܠܢܝܚܬܝ ܀
6Wale waliotangulia kuhubiriwa Habari Njema hawakupata pumziko hilo kwa sababu hawakuamini. Wapo, basi, wengine ambao wangejaliwa kulipata.
6ܡܛܠ ܗܟܝܠ ܕܐܝܬ ܗܘܐ ܐܬܪܐ ܕܐܢܫ ܐܢܫ ܢܥܘܠ ܠܗ ܘܗܢܘܢ ܕܐܤܬܒܪܘ ܩܕܡܝܐ ܠܐ ܥܠܘ ܒܕܠܐ ܐܬܛܦܝܤܘ ܀
7Jambo hili ni wazi, kwani Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa "Leo". Miaka mingi baadaye Mungu alisema juu ya hiyo siku kwa maneno ya Daudi katika Maandiko yaliyokwisha tajwa: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu."
7ܬܘܒ ܝܘܡܐ ܐܚܪܢܐ ܤܐܡ ܡܢ ܒܬܪ ܙܒܢܐ ܤܓܝܐܐ ܐܝܟܢܐ ܕܡܢ ܠܥܠ ܟܬܝܒ ܕܐܡܪ ܕܘܝܕ ܕܝܘܡܢܐ ܐܢ ܒܩܠܗ ܬܫܡܥܘܢ ܠܐ ܬܩܫܘܢ ܠܒܘܬܟܘܢ ܀
8Kama Yoshua angaliwapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.
8ܐܠܘ ܓܝܪ ܝܫܘܥ ܒܪ ܢܘܢ ܐܢܝܚ ܗܘܐ ܐܢܘܢ ܠܐ ܐܡܪ ܗܘܐ ܡܢ ܒܬܪܟܢ ܥܠ ܝܘܡܐ ܐܚܪܢܐ ܀
9Kwa hiyo, basi, bado lipo pumziko kwa watu wa Mungu kama kule kupumzika kwake Mungu siku ya saba.
9ܡܕܝܢ ܩܝܡ ܗܘ ܠܡܫܒܬܘ ܠܥܡܗ ܕܐܠܗܐ ܀
10Maana, kila anayepata pumziko aliloahidi Mungu atapumzika baada ya kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika baada ya yake.
10ܐܝܢܐ ܓܝܪ ܕܥܠ ܠܢܝܚܬܗ ܐܬܬܢܝܚ ܐܦ ܗܘ ܡܢ ܥܒܕܘܗܝ ܐܝܟ ܕܐܠܗܐ ܡܢ ܕܝܠܗ ܀
11Basi, tujitahidi kupata pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwenu atakayeshindwa, kama walivyofanya wao kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.
11ܢܬܚܦܛ ܗܟܝܠ ܕܢܥܘܠ ܠܗܝ ܢܝܚܬܐ ܕܠܐ ܢܦܠ ܒܕܡܘܬܐ ܕܗܢܘܢ ܕܠܐ ܐܬܛܦܝܤܘ ܀
12Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali zaidi kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na mafuta. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
12ܚܝܐ ܗܝ ܓܝܪ ܡܠܬܗ ܕܐܠܗܐ ܘܟܠ ܤܥܪܐ ܘܚܪܝܦܐ ܛܒ ܡܢ ܤܦܤܪܐ ܕܬܪܝܢ ܦܘܡܝܗ ܘܥܐܠܐ ܥܕܡܐ ܠܦܘܪܫܢܐ ܕܢܦܫܐ ܘܕܪܘܚܐ ܘܕܫܪܝܬܐ ܘܕܡܘܚܐ ܘܕܓܪܡܐ ܘܕܝܢܐ ܡܚܫܒܬܐ ܘܬܪܥܝܬܐ ܕܠܒܐ ܀
13Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake. Kwake, sisi sote tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
13ܘܠܝܬ ܒܪܝܬܐ ܕܛܫܝܐ ܡܢ ܩܕܡܝܗ ܐܠܐ ܟܠ ܡܕܡ ܥܪܛܠ ܘܓܠܐ ܩܕܡ ܥܝܢܘܗܝ ܕܠܗ ܝܗܒܝܢܢ ܦܬܓܡܐ ܀
14Basi, tunapaswa kuzingatia kwa uthabiti imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka kwa Mungu mwenyewe--Yesu, Mwana wa Mungu.
14ܡܛܠ ܕܐܝܬ ܠܢ ܗܟܝܠ ܪܒ ܟܘܡܪܐ ܪܒܐ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܒܪܗ ܕܐܠܗܐ ܕܤܠܩ ܠܫܡܝܐ ܢܚܡܤܢ ܒܬܘܕܝܬܗ ܀
15Huyu Kuhani Mkuu wetu si mmoja ambaye hawezi kutuunga mkono katika unyonge wetu, ila ni Kuhani Mkuu ambaye alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
15ܠܐ ܓܝܪ ܐܝܬ ܠܢ ܪܒܟܘܡܪܐ ܕܠܐ ܡܨܐ ܕܢܚܫ ܥܡ ܟܪܝܗܘܬܢ ܐܠܐ ܕܡܢܤܝ ܒܟܠܡܕܡ ܐܟܘܬܢ ܤܛܪ ܡܢ ܚܛܝܬܐ ܀
16Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu, palipo na neema, ili tukajipatie huruma na neema ya kutusaidia wakati wa lazima.
16ܢܬܩܪܒ ܗܟܝܠ ܒܓܠܐ ܥܝܢ ܠܟܘܪܤܝܐ ܕܛܝܒܘܬܗ ܕܢܤܒ ܪܚܡܐ ܘܢܫܟܚ ܛܝܒܘܬܐ ܠܥܘܕܪܢܐ ܒܙܒܢܐ ܕܐܘܠܨܢܐ ܀