1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
1ܗܢܐ ܕܝܢ ܡܠܟܝܙܕܩ ܐܝܬܘܗܝ ܡܠܟ ܫܠܝV ܟܘܡܪܐ ܕܐܠܗܐ ܡܪܝܡܐ ܘܗܘ ܐܪܥܗ ܠܐܒܪܗV ܟܕ ܗܦܟ ܡܢ ܚܪܒܐ ܕܡܠܟܐ ܘܒܪܟܗ ܀
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
2ܘܠܗ ܦܪܫ ܐܒܪܗV ܡܥܤܪܐ ܡܢ ܟܠܡܕV ܕܐܝܬ ܗܘܐ ܥܡܗ ܡܬܦܫܩ ܕܝܢ ܫܡܗ ܡܠܟܐ ܕܟܐܢܘܬܐ ܘܬܘܒ ܡܠܟ ܫܠܝV ܕܐܝܬܘܗܝ ܡܠܟܐ ܕܫܠܡܐ ܀
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
3ܕܠܐ ܐܒܘܗܝ ܘܠܐ ܐܡܗ ܐܬܟܬܒܘ ܒܫܪܒܬܐ ܘܠܐ ܪܝܫܝܬܐ ܕܝܘܡܘܗܝ ܘܠܐ ܫܘܠܡܐ ܕܚܝܘܗܝ ܐܠܐ ܒܕܡܘܬܐ ܕܒܪܗ ܕܐܠܗܐ ܡܩܘܝܐ ܟܘܡܪܘܬܗ ܠܥܠV ܀
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
4ܚܙܘ ܕܝܢ ܟܡܐ ܪܒ ܗܢܐ ܕܐܒܪܗV ܪܝܫ ܐܒܗܬܐ ܠܗ ܝܗܒ ܡܥܤܪܐ ܕܪܫܝܬܐ ܀
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
5ܐܝܠܝܢ ܓܝܪ ܡܢ ܒܢܝ ܠܘܝ ܕܡܩܒܠܝܢ ܗܘܘ ܟܘܡܪܘܬܐ ܦܘܩܕܢܐ ܐܝܬ ܗܘܐ ܠܗܘܢ ܕܢܡܘܤܐ ܕܢܤܒܘܢ ܡܥܤܪܐ ܡܢ ܥܡܐ ܗܢܘܢ ܡܢ ܐܚܝܗܘܢ ܟܕ ܐܦ ܗܢܘܢ ܡܢ ܚܨܗ ܕܐܒܪܗV ܢܦܩܘ ܀
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
6ܗܢܐ ܕܝܢ ܕܠܐ ܟܬܝܒ ܒܫܪܒܬܗܘܢ ܡܥܤܪܐ ܫܩܠ ܡܢ ܐܒܪܗV ܘܒܪܟܗ ܠܗܘ ܕܩܒܠ ܡܘܠܟܢܐ ܀
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
7ܕܠܐ ܚܪܝܢܐ ܕܝܢ ܗܘ ܕܒܨܝܪ ܡܬܒܪܟ ܡܢ ܗܘ ܕܡܝܬܪ ܡܢܗ ܀
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
8ܘܗܪܟܐ ܒܢܝܢܫܐ ܕܡܝܬܝܢ ܢܤܒܝܢ ܡܥܤܪܐ ܠܗܠ ܕܝܢ ܗܘ ܕܐܤܗܕ ܥܠܘܗܝ ܟܬܒܐ ܕܚܝ ܗܘ ܀
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
9ܘܐܝܟ ܐܢܫ ܢܐܡܪ ܒܝܕ ܐܒܪܗV ܐܦ ܠܘܝ ܗܘ ܕܡܥܤܪܐ ܢܤܒ ܗܘܐ ܐܦ ܗܘ ܐܬܥܤܪ ܀
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
10ܥܕܟܝܠ ܓܝܪ ܒܚܨܗ ܗܘܐ ܕܐܒܘܗܝ ܟܕ ܐܪܥܗ ܠܡܠܟܝܙܕܩ ܀
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
11ܐܠܘ ܗܟܝܠ ܓܡܝܪܘܬܐ ܒܝܕ ܟܘܡܪܘܬܐ ܕܠܘܝܐ ܐܝܬܝܗ ܗܘܬ ܕܒܗ ܤܝV ܢܡܘܤܐ ܠܥܡܐ ܠܡܢܐ ܡܬܒܥܐ ܗܘܐ ܟܘܡܪܐ ܐܚܪܢܐ ܕܢܩܘV ܒܕܡܘܬܗ ܕܡܠܟܝܙܕܩ ܐܡܪ ܕܝܢ ܕܒܕܡܘܬܗ ܕܐܗܪܘܢ ܢܗܘܐ ܀
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
12ܐܠܐ ܐܝܟܢܐ ܕܗܘܐ ܫܘܚܠܦܐ ܒܟܘܡܪܘܬܐ ܗܟܢܐ ܗܘܐ ܫܘܚܠܦܐ ܐܦ ܒܢܡܘܤܐ ܀
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
13ܗܘ ܓܝܪ ܕܐܬܐܡܪ ܥܠܘܗܝ ܗܠܝܢ ܡܢ ܫܪܒܬܐ ܗܘ ܐܚܪܬܐ ܐܬܝܠܕ ܕܐܢܫ ܡܡܬܘV ܡܢܗ ܠܐ ܫܡܫ ܒܡܕܒܚܐ ܀
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
14ܓܠܝܐ ܗܝ ܓܝܪ ܕܡܢ ܝܗܘܕܐ ܕܢܚ ܡܪܢ ܡܢ ܫܪܒܬܐ ܕܠܐ ܐܡܪ ܥܠܝܗ ܡܘܫܐ ܡܕV ܥܠ ܟܘܡܪܘܬܐ ܀
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
15ܘܝܬܝܪܐܝܬ ܬܘܒ ܝܕܝܥܐ ܒܗܝ ܕܐܡܪ ܕܒܕܡܘܬܗ ܕܡܠܟܝܙܕܩ ܩܐV ܟܘܡܪܐ ܐܚܪܢܐ ܀
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
16ܗܘ ܕܠܐ ܗܘܐ ܒܢܡܘܤܐ ܕܦܘܩܕܢܐ ܦܓܪܢܝܐ ܗܘܐ ܐܠܐ ܒܚܝܠܐ ܕܚܝܐ ܕܠܐ ܡܫܬܪܝܢ ܀
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
17ܡܤܗܕ ܓܝܪ ܥܠܘܗܝ ܕܐܢܬ ܗܘ ܟܘܡܪܐ ܠܥܠV ܒܕܡܘܬܗ ܕܡܠܟܝܙܕܩ ܀
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
18ܫܘܚܠܦܐ ܕܝܢ ܕܗܘܐ ܠܦܘܩܕܢܐ ܩܕܡܝܐ ܡܛܠ ܡܚܝܠܘܬܗ ܘܕܝܘܬܪܢ ܠܝܬ ܗܘܐ ܒܗ ܀
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
19ܡܕV ܓܝܪ ܠܐ ܓܡܪ ܢܡܘܤܐ ܥܠ ܕܝܢ ܚܠܦܘܗܝ ܤܒܪܐ ܕܡܝܬܪ ܡܢܗ ܕܒܗ ܡܬܩܪܒܝܢܢ ܠܐܠܗܐ ܀
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
20ܘܫܪܪܗ ܠܢ ܒܡܘܡܬܐ ܀
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
21ܗܢܘܢ ܓܝܪ ܕܠܐ ܡܘܡܬܐ ܗܘܘ ܟܘܡܪܐ ܗܢܐ ܕܝܢ ܒܡܘܡܬܐ ܐܝܟ ܕܐܡܪ ܠܗ ܒܝܕ ܕܘܝܕ ܕܝܡܐ ܡܪܝܐ ܘܠܐ ܢܕܓܠ ܕܐܢܬ ܗܘ ܟܘܡܪܐ ܠܥܠV ܒܕܡܘܬܗ ܕܡܠܟܝܙܕܩ ܀
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
22ܗܢܐ ܟܠܗ ܡܝܬܪܐ ܕܝܬܩܐ ܗܕܐ ܕܗܘܐ ܒܗ ܥܪܒܐ ܝܫܘܥ ܀
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
23ܘܗܢܘܢ ܗܘܘ ܟܘܡܪܐ ܤܓܝܐܐ ܡܛܠ ܕܡܝܬܝܢ ܗܘܘ ܘܠܐ ܡܫܬܒܩܝܢ ܗܘܘ ܕܢܩܘܘܢ ܀
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
24ܗܢܐ ܕܝܢ ܡܛܠ ܕܠܥܠV ܩܝV ܠܐ ܥܒܪܐ ܟܘܡܪܘܬܗ ܀
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
25ܘܡܫܟܚ ܠܡܚܝܘ ܠܥܠV ܠܐܝܠܝܢ ܕܡܬܩܪܒܝܢ ܒܐܝܕܗ ܠܐܠܗܐ ܚܝ ܗܘ ܓܝܪ ܒܟܠܙܒܢ ܘܡܤܩ ܨܠܘܬܐ ܚܠܦܝܗܘܢ ܀
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
26ܕܐܝܟ ܗܢܐ ܓܝܪ ܟܘܡܪܐ ܐܦ ܙܕܩ ܗܘܐ ܠܢ ܕܟܝܐ ܕܠܐ ܒܝܫܘ ܘܕܠܐ ܛܘܠܫܐ ܕܦܪܝܩ ܡܢ ܚܛܗܐ ܘܡܪܝV ܠܥܠ ܡܢ ܫܡܝܐ ܀
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
27ܘܠܝܬ ܠܗ ܐܘܠܨܢܐ ܟܠܝܘV ܐܝܟ ܪܒܝ ܟܘܡܪܐ ܕܠܘܩܕV ܚܠܦ ܚܛܗܘܗܝ ܢܩܪܒ ܕܒܚܐ ܘܗܝܕܝܢ ܚܠܦ ܥܡܐ ܗܕܐ ܓܝܪ ܥܒܕܗ ܚܕܐ ܙܒܢ ܒܢܦܫܗ ܕܩܪܒ ܀
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.
28ܢܡܘܤܐ ܓܝܪ ܒܢܝܢܫܐ ܗܘ ܟܪܝܗܐ ܡܩܝV ܟܘܡܪܐ ܡܠܬܐ ܕܝܢ ܕܡܘܡܬܐ ܕܗܘܬ ܒܬܪ ܢܡܘܤܐ ܒܪܐ ܓܡܝܪܐ ܠܥܠV ܀