Swahili: New Testament

Syriac: NT

Revelation

14

1Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
1ܘܚܙܝܬ ܘܗܐ ܐܡܪܐ ܩܐܡ ܥܠ ܛܘܪܐ ܕܨܗܝܘܢ ܘܥܡܗ ܡܐܐ ܘܐܪܒܥܝܢ ܘܐܪܒܥܐ ܐܠܦܝܢ ܕܐܝܬ ܥܠܝܗܘܢ ܫܡܗ ܘܫܡܐ ܕܐܒܘܗܝ ܟܬܝܒ ܥܠ ܒܝܬ ܥܝܢܝܗܘܢ ܀
2Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
2ܘܫܡܥܬ ܩܠܐ ܡܢ ܫܡܝܐ ܐܝܟ ܩܠܐ ܕܡܝܐ ܤܓܝܐܐ ܘܐܝܟ ܩܠܐ ܕܪܥܡܐ ܪܒܐ ܩܠܐ ܐܝܢܐ ܕܫܡܥܬ ܐܝܟ ܩܝܬܪܘܕܐ ܕܢܩܫ ܒܩܝܬܪܘܗܝ ܀
3Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
3ܘܡܫܒܚܝܢ ܐܝܟ ܬܫܒܘܚܬܐ ܚܕܬܐ ܩܕܡ ܟܘܪܤܝܐ ܘܩܕܡ ܐܪܒܥ ܚܝܘܢ ܘܩܕܡ ܩܫܝܫܐ ܘܠܐ ܐܢܫ ܐܬܡܨܝ ܠܡܐܠܦܗ ܠܬܫܒܘܚܬܐ ܐܠܐ ܐܢ ܡܐܐ ܘܐܪܒܥܝܢ ܘܐܪܒܥܐ ܐܠܦܝܢ ܙܒܝܢܝ ܡܢ ܐܪܥܐ ܀
4Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
4ܗܠܝܢ ܐܢܘܢ ܐܝܠܝܢ ܕܥܡ ܢܫܐ ܠܐ ܐܬܛܘܫܘ ܒܬܘܠܐ ܓܝܪ ܐܝܬܝܗܘܢ ܗܠܝܢ ܕܢܩܦܘܗܝ ܠܐܡܪܐ ܟܠ ܟܪ ܕܢܐܙܠ ܗܠܝܢ ܐܙܕܒܢܘ ܡܢ ܐܢܫܐ ܪܫܝܬܐ ܠܐܠܗܐ ܘܠܐܡܪܐ ܀
5Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
5ܕܒܦܘܡܗܘܢ ܠܐ ܐܫܬܟܚܬ ܕܓܠܘܬܐ ܕܠܐ ܡܘܡ ܓܝܪ ܐܢܘܢ ܀
6Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote.
6ܘܚܙܝܬ ܐܚܪܢܐ ܡܠܐܟܐ ܕܦܪܚ ܡܨܥܬ ܫܡܝܐ ܘܐܝܬ ܠܗ ܥܠܘܗܝ ܤܒܪܬܐ ܕܠܥܠܡ ܠܡܤܒܪܘ ܥܠ ܝܬܒܝ ܐܪܥܐ ܘܥܠ ܟܠ ܥܡ ܘܐܡܘܢ ܘܫܪܒܢ ܘܠܫܢ ܀
7Akasema kwa sauti kubwa, "Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji."
7ܠܡܐܡܪ ܒܩܠܐ ܪܒܐ ܕܚܠܘ ܡܢ ܐܠܗܐ ܘܗܒܘ ܠܗ ܬܫܒܘܚܬܐ ܡܛܠ ܕܐܬܬ ܫܥܬܐ ܕܕܝܢܗ ܘܤܓܘܕܘ ܠܕܥܒܕ ܫܡܝܐ ܘܐܪܥܐ ܘܝܡܐ ܘܥܝܢܬܐ ܕܡܝܐ ܀
8Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, "Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake--divai kali ya uzinzi wake!"
8ܘܐܚܪܢܐ ܕܬܪܝܢ ܢܩܝܦ ܗܘܐ ܠܗ ܘܐܡܪ ܢܦܠܬ ܢܦܠܬ ܒܒܝܠ ܪܒܬܐ ܐܝܕܐ ܕܡܢ ܚܡܬܐ ܕܙܢܝܘܬܗ ܐܫܩܝܬ ܠܟܠܗܘܢ ܥܡܡܐ ܀
9Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, "Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
9ܘܐܚܪܢܐ ܡܠܐܟܐ ܕܬܠܬܐ ܢܩܦ ܠܗܘܢ ܠܡܐܡܪ ܒܩܠܐ ܪܒܐ ܐܝܢܐ ܕܤܓܕ ܠܚܝܘܬܐ ܘܠܨܠܡܗ ܘܫܩܠ ܪܘܫܡܗ ܒܝܬ ܥܝܢܘܗܝ ܀
10yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
10ܐܦ ܗܘ ܢܫܬܐ ܡܢ ܚܡܪܐ ܕܚܡܬܗ ܕܡܪܝܐ ܕܡܙܝܓ ܕܠܐ ܚܠܛܐ ܒܟܤܐ ܕܪܘܓܙܗ ܘܢܫܬܢܩ ܒܢܘܪܐ ܘܟܒܪܝܬܐ ܩܕܡ ܡܠܐܟܐ ܩܕܝܫܐ ܘܩܕܡ ܐܡܪܐ ܀
11Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana."
11ܘܬܢܢܐ ܕܬܫܢܝܩܗܘܢ ܠܥܠܡ ܥܠܡܝܢ ܢܤܩ ܘܠܝܬ ܠܗܘܢ ܢܦܐܫܐ ܐܝܡܡܐ ܘܠܠܝܐ ܐܝܠܝܢ ܕܤܓܕܝܢ ܠܚܝܘܬܐ ܘܠܨܠܡܗ ܘܠܡܢ ܕܫܩܠ ܪܘܫܡܐ ܕܫܡܗ ܀
12Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
12ܗܪܟܐ ܐܝܬܝܗ ܡܤܝܒܪܢܘܬܐ ܕܩܕܝܫܐ ܐܝܠܝܢ ܕܢܛܪܘ ܦܘܩܕܢܘܗܝ ܕܐܠܗܐ ܘܗܝܡܢܘܬܗ ܕܝܫܘܥ ܀
13Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, "Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana." Naye Roho asema, "Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata."
13ܘܫܡܥܬ ܩܠܐ ܡܢ ܫܡܝܐ ܕܐܡܪ ܟܬܘܒ ܛܘܒܝܗܘܢ ܠܡܝܬܐ ܐܝܠܝܢ ܕܥܢܕܘ ܒܡܪܢ ܡܢ ܗܫܐ ܐܝܢ ܐܡܪ ܪܘܚܐ ܡܛܠ ܕܢܬܬܢܝܚܘܢ ܡܢ ܥܡܠܝܗܘܢ ܀
14Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
14ܘܗܐ ܥܢܢܐ ܚܘܪܬܐ ܘܥܠ ܥܢܢܐ ܝܬܒ ܕܡܘܬܐ ܕܒܪܢܫܐ ܘܐܝܬ ܠܗ ܥܠ ܪܫܗ ܟܠܝܠܐ ܕܕܗܒܐ ܘܥܠ ܐܝܕܗ ܡܓܠܬܐ ܚܪܝܦܬܐ ܀
15Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, "Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva."
15ܘܐܚܪܢܐ ܡܠܐܟܐ ܢܦܩ ܡܢ ܗܝܟܠܐ ܘܩܥܐ ܒܩܠܐ ܪܒܐ ܠܕܝܬܒ ܥܠ ܥܢܢܐ ܫܕܪ ܡܓܠܬܟ ܘܚܨܘܕ ܡܛܠ ܕܐܬܬ ܫܥܬܐ ܠܡܚܨܕ ܀
16Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
16ܘܐܪܡܝ ܗܘ ܕܝܬܒ ܥܠ ܥܢܢܐ ܡܓܠܬܗ ܥܠ ܐܪܥܐ ܘܐܬܚܨܕܬ ܐܪܥܐ ܀
17Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
17ܘܐܚܪܢܐ ܡܠܐܟܐ ܢܦܩ ܡܢ ܗܝܟܠܐ ܕܒܫܡܝܐ ܘܥܠܘܗܝ ܐܝܬ ܡܓܠܬܐ ܚܪܝܦܬܐ ܀
18Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, "Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!"
18ܘܐܚܪܢܐ ܡܠܐܟܐ ܢܦܩ ܡܢ ܡܕܒܚܐ ܕܐܝܬ ܠܗ ܫܘܠܛܢܐ ܥܠ ܢܘܪܐ ܘܩܥܐ ܒܩܠܐ ܪܒܐ ܠܕܐܝܬ ܠܗ ܡܓܠܬܐ ܚܪܝܦܬܐ ܫܕܪ ܐܢܬ ܡܓܠܬܟ ܚܪܝܦܬܐ ܘܩܛܘܦ ܠܤܓܘܠܐ ܕܟܪܡܗ ܕܐܪܥܐ ܡܛܠ ܕܪܒܝ ܥܢܒܘܗܝ ܀
19Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
19ܘܐܪܡܝ ܡܠܐܟܐ ܡܓܠܬܗ ܥܠ ܐܪܥܐ ܘܩܛܦ ܠܟܪܡܗ ܕܐܪܥܐ ܘܐܪܡܝ ܒܡܥܨܪܬܐ ܪܒܬܐ ܕܚܡܬܗ ܕܐܠܗܐ ܀
20Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.
20ܘܐܬܬܕܝܫܬ ܡܥܨܪܬܐ ܠܒܪ ܡܢ ܡܕܝܢܬܐ ܘܢܦܩ ܕܡܐ ܡܢ ܡܥܨܪܬܐ ܥܕܡܐ ܠܦܓܘܕܐ ܕܪܟܫܐ ܥܠ ܐܠܦ ܘܡܐܬܝܢ ܐܤܛܕܘܢ ܀