1Baada ya hayo, nilimwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa na uwezo mkuu, na dunia ikamulikwa na mng'ao wake.
1ܘܡܢ ܒܬܪ ܗܠܝܢ ܚܙܝܬ ܐܚܪܢܐ ܡܠܐܟܐ ܕܢܚܬ ܡܢ ܫܡܝܐ ܕܐܝܬ ܠܗ ܫܘܠܛܢܐ ܪܒܐ ܘܐܪܥܐ ܢܗܪܬ ܡܢ ܬܫܒܘܚܬܗ ܀
2Basi, akapaaza sauti kwa nguvu akisema, "Umeanguka; Babuloni mkuu umeanguka! Sasa umekuwa makao ya mashetani na pepo wachafu; umekuwa makao ya ndege wachafu na wa kuchukiza mno.
2ܘܩܥܐ ܒܩܠܐ ܪܒܐ ܢܦܠܬ ܢܦܠܬ ܒܒܝܠ ܪܒܬܐ ܘܗܘܬ ܡܥܡܪܐ ܠܫܐܕܐ ܘܢܛܘܪܬܐ ܠܟܠ ܪܘܚܐ ܠܐ ܕܟܝܬܐ ܘܤܢܝܬܐ ܀
3Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo."
3ܡܛܠ ܕܡܢ ܚܡܪܐ ܕܙܢܝܘܬܗ ܡܙܓܬ ܠܟܠܗܘܢ ܥܡܡܐ ܘܡܠܟܝܗ ܕܐܪܥܐ ܥܡܗ ܙܢܝܘ ܘܬܓܪܐ ܕܐܪܥܐ ܡܢ ܚܝܠܐ ܕܫܢܝܗ ܥܬܪܘ ܀
4Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema, "Watu wangu, ondokeni kwake, ili msishirikiane naye katika dhambi zake, msije mkaipata adhabu yake.
4ܘܫܡܥܬ ܐܚܪܢܐ ܩܠܐ ܡܢ ܫܡܝܐ ܕܐܡܪ ܦܘܩܘ ܡܢ ܓܘܗ ܥܡܝ ܕܠܐ ܬܫܬܘܬܦܘܢ ܒܚܛܗܝܗ ܕܠܡܐ ܬܤܒܘܢ ܡܢ ܡܚܘܬܗ ܀
5Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno, zimelundikana mpaka mbinguni, na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
5ܡܛܠ ܕܕܒܩܘ ܒܗ ܚܛܗܐ ܥܕܡܐ ܠܫܡܝܐ ܘܐܬܕܟܪ ܐܠܗܐ ܥܘܠܝܗ ܀
6Mtendeeni kama alivyowatendea ninyi; mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda. Jazeni kikombe chake kwa kinywaji kikali mara mbili zaidi ya kile alichowapeni.
6ܦܘܪܥܘܗ ܐܝܟܢܐ ܕܐܦ ܗܝ ܦܪܥܬ ܘܥܘܦܘ ܠܗ ܐܥܦܐ ܥܠ ܥܒܕܝܗ ܒܟܤܐ ܗܘ ܕܡܙܓܬ ܡܙܘܓܘ ܠܗ ܐܥܦܐ ܀
7Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!
7ܥܠ ܡܕܡ ܕܫܒܚܬ ܢܦܫܗ ܘܐܫܬܥܠܝܬ ܕܐܝܟ ܗܟܢ ܫܘܢܩܐ ܘܐܒܠܐ ܡܛܠ ܕܒܠܒܗ ܐܡܪܐ ܕܝܬܒܐ ܐܢܐ ܡܠܟܬܐ ܘܐܪܡܠܬܐ ܠܝܬܝ ܘܐܒܠܐ ܠܐ ܐܚܙܐ ܀
8Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja: ugonjwa, huzuni na njaa. Atachomwa moto, maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ni Mwenye Uwezo."
8ܡܛܠܗܢܐ ܒܚܕ ܝܘܡܐ ܢܐܬܝܢ ܥܠܝܗ ܡܚܘܬܐ ܡܘܬܐ ܘܐܒܠܐ ܘܟܦܢܐ ܘܒܢܘܪܐ ܬܐܩܕ ܡܛܠ ܕܚܝܠܬܢ ܡܪܝܐ ܕܕܢܗ ܀
9Wafalme wa Dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.
9ܘܢܒܟܘܢܗ ܘܢܪܩܕܘܢ ܥܠܝܗ ܡܠܟܝܗ ܕܐܪܥܐ ܗܢܘܢ ܕܙܢܝܘ ܥܡܗ ܘܐܫܬܥܠܝܘ ܡܐ ܕܚܙܝܢ ܬܢܢܐ ܕܝܩܕܢܗ ܀
10Wanasimama kwa mbali kwa sababu ya kuogopa mateso yake, na kusema, "Ole! Ole kwako Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata."
10ܟܕ ܩܝܡܝܢ ܡܢ ܩܒܘܠ ܡܢ ܕܚܠܬܐ ܕܬܫܢܝܩܗ ܘܢܐܡܪܘܢ ܘܝ ܘܝ ܘܝ ܡܕܝܢܬܐ ܪܒܬܐ ܒܒܝܠ ܡܕܝܢܬܐ ܥܫܝܢܬܐ ܡܛܠ ܕܒܚܕܐ ܫܥܐ ܐܬܐ ܕܝܢܟܝ ܀
11Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumfanyia matanga, maana hakuna mtu anayenunua tena bidhaa zao;
11ܘܬܓܪܐ ܕܐܪܥܐ ܢܒܟܘܢ ܘܢܬܐܒܠܘܢ ܥܠܝܗ ܘܡܘܒܠܗܘܢ ܠܝܬ ܕܙܒܢ ܬܘܒ ܀
12hakuna tena wa kununua dhahabu yao, fedha, mawe ya thamani na lulu, kitani na nguo za rangi ya zambarau, hariri na nguo nyekundu; vyombo vya kila aina ya miti ya pekee, vyombo vya pembe za ndovu, vya miti ya thamani kubwa, vya shaba, chuma na marmari;
12ܡܘܒܠܐ ܕܕܗܒܐ ܘܕܤܐܡܐ ܘܕܟܐܦܐ ܝܩܝܪܬܐ ܘܕܡܪܓܢܝܬܐ ܘܕܒܘܨܐ ܘܕܐܪܓܘܢܐ ܘܫܐܪܝܐ ܕܙܚܘܪܝܬܐ ܘܟܠ ܩܝܤ ܕܒܤܡܐ ܘܟܠ ܡܐܢ ܕܫܢܐ ܘܟܠ ܡܐܢ ܕܩܝܤܐ ܝܩܝܪܐ ܘܢܚܫܐ ܘܦܪܙܠܐ ܘܫܝܫܐ ܀
13mdalasini, viungo, ubani, manemane, udi, divai, mafuta, unga na ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari ya kukokotwa, watumwa wao na hata maisha ya watu.
13ܘܩܘܢܝܡܘܢ ܘܒܤܡܐ ܘܡܘܪܘܢ ܘܠܒܘܢܬܐ ܘܚܡܪܐ ܘܡܫܚܐ ܘܤܡܝܕܐ ܘܥܪܒܐ ܘܪܟܫܐ ܘܡܪܟܒܬܐ ܘܦܓܪܐ ܘܢܦܫܬܐ ܕܒܢܝܢܫܐ ܀
14Wafanyabiashara wanamwambia: "Faida yote uliyotazamia imetoweka, na utajiri na fahari vimekuponyoka; hutaweza kuvipata tena!"
14ܘܐܒܟܝ ܪܓܬܐ ܕܢܦܫܟܝ ܐܙܠ ܡܢܟܝ ܘܟܠ ܕܫܡܝܢ ܘܫܒܝܚ ܐܙܠ ܡܢܟܝ ܘܠܐ ܬܘܒ ܬܚܙܝܢ ܐܢܘܢ ܀
15Wafanya biashara waliotajirika kutokana na mji huo, watasimama mbali kwa sababu ya hofu ya mateso yake, watalalamika na kuomboleza,
15ܘܠܐ ܢܫܟܚܘܢ ܐܢܘܢ ܬܓܪܐ ܕܗܠܝܢ ܕܥܬܪܘ ܡܢܗ ܡܢ ܩܒܘܠ ܢܩܘܡܘܢ ܡܢ ܕܚܠܬܐ ܕܫܘܢܩܗ ܟܕ ܒܟܝܢ ܘܐܒܝܠܝܢ ܀
16wakisema, "Ole! Ole kwa mji huu mkuu. Ulizoea kuvalia nguo za kitani, za rangi ya zambarau na nyekundu, na kujipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu!
16ܘܐܡܪܝܢ ܘܝ ܘܝ ܡܕܝܢܬܐ ܪܒܬܐ ܕܡܥܛܦܐ ܒܘܨܐ ܘܐܪܓܘܢܐ ܘܙܚܘܪܝܬܐ ܕܡܕܗܒܢ ܒܕܗܒܐ ܘܟܐܦܐ ܝܩܝܪܬܐ ܘܡܪܓܢܝܬܐ ܀
17Kwa saa moja tu utajiri wako umetoweka!" Halafu manahodha wote na wasafiri wao, wanamaji na wote wanaofanya kazi baharini, walisimama kwa mbali,
17ܡܛܠ ܕܒܚܕܐ ܫܥܐ ܐܤܬܪܩ ܥܘܬܪܐ ܕܐܝܟ ܗܢܐ ܘܟܠ ܡܕܒܪܝ ܐܠܦܐ ܘܟܠ ܐܙܠܝ ܒܐܠܦܐ ܠܕܘܟܝܬܐ ܘܐܠܦܪܐ ܘܟܠ ܕܒܝܡܐ ܦܠܚܝܢ ܡܢ ܪܘܚܩܐ ܩܡܘ ܀
18na walipouona moshi wa moto ule uliouteketeza, wakalia kwa sauti: "Hakujapata kuwako mji kama mji huu mkuu!"
18ܘܒܟܐܘܗ ܟܕ ܚܙܝܢ ܬܢܢܐ ܕܝܩܕܢܗ ܘܐܡܪܝܢ ܡܢ ܗܝ ܕܕܡܝܐ ܠܡܕܝܢܬܐ ܪܒܬܐ ܀
19Wakajimwagia vumbi juu ya vichwa vyao wakilia kwa sauti na kuomboleza: "Ole! Ole kwako mji mkuu! Ni mji ambamo wote wenye meli zisafirizo baharini walitajirika kutokana na utajiri wake. Kwa muda wa saa moja tu umepoteza kila kitu!"
19ܘܐܪܡܝܘ ܥܦܪܐ ܥܠ ܪܝܫܝܗܘܢ ܘܩܥܘ ܟܕ ܒܟܝܢ ܘܐܒܝܠܝܢ ܘܐܡܪܝܢ ܘܝ ܘܝ ܡܕܝܢܬܐ ܪܒܬܐ ܐܝܕܐ ܕܒܗ ܥܬܪܘ ܐܝܠܝܢ ܕܐܝܬ ܠܗܘܢ ܐܠܦܐ ܒܝܡܐ ܡܢ ܐܝܩܪܗ ܕܒܚܕܐ ܫܥܐ ܚܪܒܬ ܀
20Furahi ee mbingu, kwa sababu ya uharibifu wake. Furahini watu wa Mungu, mitume na manabii! Kwa maana Mungu ameuhukumu kwa sababu ya mambo uliyowatenda ninyi!
20ܐܬܦܨܚܘ ܥܠܝܗ ܫܡܝܐ ܘܩܕܝܫܐ ܘܫܠܝܚܐ ܘܢܒܝܐ ܡܛܠ ܕܕܢ ܐܠܗܐ ܕܝܢܟܘܢ ܡܢܗ ܀
21Kisha malaika mmoja mwenye nguvu sana akainua jiwe mfano wa jiwe kubwa la kusagia, akalitupa baharini akisema, "Ndivyo, Babuloni atakavyotupwa na kupotea kabisa.
21ܘܫܩܠ ܚܕ ܡܢ ܡܠܐܟܐ ܚܝܠܬܢܐ ܟܐܦܐ ܪܒܬܐ ܐܝܟ ܪܚܝܐ ܘܐܪܡܝ ܒܝܡܐ ܘܐܡܪ ܗܟܢܐ ܒܚܐܦܐ ܬܫܬܕܐ ܒܒܝܠ ܡܕܝܢܬܐ ܪܒܬܐ ܘܠܐ ܬܫܟܚ ܬܘܒ ܀
22Sauti za vinubi za muziki, sauti za wapiga filimbi na tarumbeta hazitasikika tena ndani yako. Hakuna fundi wa namna yoyote ile atakayepatikana tena ndani yako; wala sauti ya jiwe la kusagia haitasikika tena ndani yako.
22ܘܩܠܐ ܕܩܝܬܪܐ ܘܕܫܝܦܘܪܐ ܘܕܙܢܝ ܙܡܪܐ ܘܕܡܙܥܘܩܐ ܠܐ ܢܫܬܡܥ ܒܟܝ ܬܘܒ ܀
23Mwanga wa taa hautaonekana tena ndani yako; sauti za bwana arusi na bibi arusi hazitasikika tena ndani yako. Wafanyabiashara wako walikuwa wakuu duniani, na kwa uchawi wako mataifa yote yalipotoshwa!"
23ܘܢܘܗܪܐ ܕܫܪܓܐ ܠܐ ܢܬܚܙܐ ܠܟܝ ܬܘܒ ܘܩܠܐ ܕܚܬܢܐ ܘܩܠܐ ܕܟܠܬܐ ܠܐ ܢܫܬܡܥ ܒܟܝ ܬܘܒ ܡܛܠ ܕܬܓܪܝܟܝ ܐܝܬ ܗܘܘ ܪܘܪܒܢܝܗ ܕܐܪܥܐ ܡܛܠ ܕܒܚܪܫܝܟܝ ܐܛܥܝܬܝ ܠܟܠܗܘܢ ܥܡܡܐ ܀
24Mji huo uliadhibiwa kwani humo mlipatikana damu ya manabii, damu ya watu wa Mungu na damu ya watu wote waliouawa duniani.
24ܘܒܗ ܐܫܬܟܚ ܕܡܐ ܕܢܒܝܐ ܘܩܕܝܫܐ ܕܩܛܝܠܝܢ ܥܠ ܐܪܥܐ ܀