1Baada ya hayo nilitazama nikaona mlango umefunguliwa mbinguni. Na ile sauti niliyoisikia pale awali ambayo ilikuwa kama sauti ya tarumbeta, ikasema, "Njoo hapa juu nami nitakuonyesha mambo yatakayotukia baadaye."
1ܡܢ ܒܬܪ ܗܠܝܢ ܚܙܝܬ ܘܗܐ ܬܪܥܐ ܦܬܝܚܐ ܒܫܡܝܐ ܘܩܠܐ ܗܘ ܕܫܡܥܬ ܐܝܟ ܫܝܦܘܪܐ ܡܠܠ ܥܡܝ ܠܡܐܡܪ ܤܩ ܠܗܪܟܐ ܘܐܚܘܝܟ ܡܐ ܕܝܗܝܒ ܠܡܗܘܐ ܒܬܪ ܗܠܝܢ ܀
2Mara nikachukuliwa na Roho. Kumbe, huko mbinguni kuna kiti cha enzi na juu yake ameketi mmoja.
2ܘܡܚܕܐ ܗܘܝܬ ܒܪܘܚ ܘܗܐ ܟܘܪܤܝܐ ܤܝܡ ܒܫܡܝܐ ܘܥܠ ܟܘܪܤܝܐ ܝܬܒ ܀
3Huyo aliyeketi juu yake alikuwa kama almasi na jiwe zuri jekundu. Upinde wa mvua ulikuwa unang'aa kama zumaridi na ulikizunguka kiti cha enzi pande zote.
3ܘܕܝܬܒ ܐܝܟ ܕܡܘܬܐ ܕܚܙܘܐ ܕܟܐܦܐ ܕܝܫܦܗ ܘܕܤܪܕܘܢ ܘܩܫܬܐ ܕܥܢܢܐ ܕܚܕܪܘܗܝ ܕܟܘܪܤܝܐ ܕܡܘܬ ܚܙܘܐ ܕܙܡܪܓܕܐ ܀
4Kulikuwa na duara la viti ishirini na vinne kukizunguka kiti cha enzi, na juu ya viti hivyo wazee ishirini na wanne walikuwa wameketi wamevaa mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani.
4ܘܚܕܪ ܟܘܪܤܝܐ ܟܘܪܤܘܬܐ ܥܤܪܝܢ ܘܐܪܒܥܐ ܘܥܠܝܗܘܢ ܕܝܢ ܕܟܘܪܤܘܬܐ ܥܤܪܝܢ ܘܐܪܒܥܐ ܩܫܝܫܝܢ ܕܝܬܒܝܢ ܕܥܛܝܦܝܢ ܡܐܢܐ ܚܘܪܐ ܘܥܠ ܩܪܩܦܬܗܘܢ ܟܠܝܠܐ ܕܕܗܒܐ ܀
5Umeme, sauti na ngurumo, vilikuwa vinatoka kwenye hicho kiti cha enzi. Taa saba za moto zilikuwa zinawaka mbele ya hicho kiti cha enzi. Taa hizo ni roho saba za Mungu.
5ܘܡܢ ܟܘܪܤܘܬܐ ܢܦܩܝܢ ܪܥܡܐ ܘܒܪܩܐ ܘܩܠܐ ܘܫܒܥܐ ܢܗܝܪܐ ܕܝܩܕܝܢ ܩܕܡܘܗܝ ܕܟܘܪܤܝܐ ܐܝܠܝܢ ܕܐܝܬܝܗܘܢ ܫܒܥ ܪܘܚܝܢ ܕܐܠܗܐ ܀
6Mbele ya kiti cha enzi kulikuwa na kitu kama bahari ya kioo, angavu kama jiwe linga'aalo sana. Katika pande zote za hicho kiti cha enzi na kukizunguka, kilikuwa na viumbe hai vinne. Viumbe hivyo vilikuwa vimejaa macho mbele na nyuma.
6ܘܩܕܡ ܟܘܪܤܝܐ ܝܡܐ ܕܙܓܘܓܝܬܐ ܐܝܟ ܕܘܡܝܐ ܕܓܠܝܕܐ ܘܒܡܨܥܬ ܟܘܪܤܝܐ ܘܚܕܪܘܗܝ ܕܟܘܪܤܝܐ ܐܪܒܥ ܚܝܘܢ ܕܡܠܝܢ ܥܝܢܐ ܡܢ ܩܕܡܝܗܝܢ ܘܡܢ ܒܤܬܪܗܝܢ ܀
7Kiumbe cha kwanza kulikuwa kama simba, cha pili kama ng'ombe, cha tatu kilikuwa na sura kama mtu, na cha nne kilikuwa kama tai anayeruka.
7ܚܝܘܬܐ ܩܕܡܝܬܐ ܕܡܝܐ ܠܐܪܝܐ ܘܚܝܘܬܐ ܕܬܪܬܝܢ ܕܡܘܬܐ ܕܥܓܠܐ ܘܚܝܘܬܐ ܕܬܠܬ ܐܝܬ ܠܗ ܐܦܐ ܐܝܟ ܕܒܪܢܫܐ ܘܚܝܘܬܐ ܕܐܪܒܥ ܕܡܘܬܐ ܕܢܫܪܐ ܕܦܪܚ ܀
8Viumbe hivyo vinne vilikuwa na mabawa sita kila kimoja, na vilikuwa vimejaa macho, ndani na nje. Usiku na mchana, bila kupumzika huimba: "Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Bwana, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwako, aliyeko na anayekuja!"
8ܐܪܒܥܬܝܗܝܢ ܚܝܘܬܐ ܟܠܚܕܐ ܡܢܗܝܢ ܩܝܡܐ ܘܐܝܬ ܠܗ ܡܢ ܛܦܪܝܗ ܘܠܥܠ ܫܬܐ ܓܦܝܢ ܚܘܕܪܢܐܝܬ ܘܡܢ ܠܓܘ ܡܠܝܢ ܥܝܢܐ ܘܫܠܝܐ ܠܝܬ ܠܗܝܢ ܐܝܡܡܐ ܘܠܠܝܐ ܠܡܐܡܪ ܩܕܝܫ ܩܕܝܫ ܩܕܝܫ ܡܪܝܐ ܐܠܗܐ ܐܚܝܕ ܟܠ ܗܘ ܕܐܝܬܘܗܝ ܗܘܐ ܘܐܝܬܘܗܝ ܘܐܬܐ ܀
9Kila mara viumbe vinne vilipoimba nyimbo za kumtukuza, kumheshimu na kumshukuru huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, ambaye anaishi milele na milele,
9ܘܡܐ ܕܝܗܒ ܐܪܒܥܬܝܗܝܢ ܚܝܘܬܐ ܬܫܒܘܚܬܐ ܘܐܝܩܪܐ ܘܩܘܒܠ ܛܝܒܘܬܐ ܠܕܝܬܒ ܥܠ ܟܘܪܤܝܐ ܘܠܕܚܝ ܠܥܠܡ ܥܠܡܝܢ ܐܡܝܢ ܀
10wale wazee ishirini na wanne hujiangusha mbele ya huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi na kumwabudu huyo ambaye anaishi milele na milele; na huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi wakisema:
10ܢܦܠܘܢ ܥܤܪܝܢ ܘܐܪܒܥܐ ܩܫܝܫܝܢ ܩܕܡ ܡܢ ܕܝܬܒ ܥܠ ܟܘܪܤܝܐ ܘܢܤܓܕܘܢ ܠܥܠܡ ܥܠܡܝܢ ܐܡܝܢ ܠܡܢ ܕܚܝ ܘܢܪܡܘܢ ܟܠܝܠܝܗܘܢ ܩܕܡ ܟܘܪܤܝܐ ܟܕ ܐܡܪܝܢ ܀
11"Wewe ni Bwana na Mungu wetu, unastahili utukufu na heshima na nguvu; maana wewe uliumba vitu vyote, na kwa matakwa yako kila kitu kimepewa uhai na uzima."
11ܕܫܘܝܬ ܗܘ ܡܪܢ ܘܐܠܗܢ ܠܡܤܒ ܬܫܒܘܚܬܐ ܘܐܝܩܪܐ ܘܚܝܠܐ ܡܛܠ ܕܐܢܬ ܒܪܝܬ ܟܠ ܘܒܝܕ ܨܒܝܢܟ ܗܘܝ ܘܐܬܒܪܝ ܀