1Sasa, kwa vile tumekubaliwa kuwa wadilifu kwa imani, basi, tunayo amani na Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo.
1ܡܛܠ ܕܐܙܕܕܩܢ ܗܟܝܠ ܒܗܝܡܢܘܬܐ ܢܗܘܐ ܠܢ ܫܠܡܐ ܠܘܬ ܐܠܗܐ ܒܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
2Kwa imani yetu, yeye ametuleta katika hali hii ya neema ya Mungu ambamo sasa tunaishi. Basi, tunajivunia tumaini tulilo nalo la kushiriki utukufu wa Mungu.
2ܕܒܗ ܐܬܩܪܒܢ ܒܗܝܡܢܘܬܐ ܠܛܝܒܘܬܐ ܗܕܐ ܕܒܗ ܩܝܡܝܢܢ ܘܡܫܬܒܗܪܝܢܢ ܒܤܒܪܐ ܕܬܫܒܘܚܬܗ ܕܐܠܗܐ ܀
3Naam, si hayo tu, bali tunafurahi pia katika taabu tukijua kwamba taabu huleta saburi,
3ܘܠܐ ܗܟܢܐ ܒܠܚܘܕ ܐܠܐ ܐܦ ܒܐܘܠܨܢܝܢ ܡܫܬܒܗܪܝܢܢ ܕܝܕܥܝܢܢ ܕܐܘܠܨܢܐ ܡܤܝܒܪܢܘܬܐ ܓܡܪ ܒܢ ܀
4nayo saburi huleta uthabiti, na uthabiti huleta tumaini.
4ܘܡܤܝܒܪܢܘܬܐ ܒܘܩܝܐ ܘܒܘܩܝܐ ܤܒܪܐ ܀
5Tumaini hilo haliwezi kutuhadaa, maana Mungu amekwisha miminia mioyoni mwetu upendo wake kwa njia ya Roho Mtakatifu aliyetujalia.
5ܤܒܪܐ ܕܝܢ ܠܐ ܡܒܗܬ ܡܛܠ ܕܚܘܒܗ ܕܐܠܗܐ ܡܫܦܥ ܥܠ ܠܒܘܬܢ ܒܪܘܚܐ ܕܩܘܕܫܐ ܕܐܬܝܗܒܬ ܠܢ ܀
6Tulipokuwa bado wanyonge, Kristo, wakati ulipotimia, alikufa kwa ajili yetu sisi waovu.
6ܐܢ ܕܝܢ ܡܫܝܚܐ ܡܛܠ ܟܪܝܗܘܬܢ ܒܙܒܢܐ ܗܢܐ ܚܠܦ ܪܫܝܥܐ ܡܝܬ ܀
7Si rahisi mtu kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu; labda mtu anaweza kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
7ܠܡܚܤܢ ܓܝܪ ܐܢܫ ܚܠܦ ܪܫܝܥܐ ܡܐܬ ܚܠܦ ܛܒܐ ܓܝܪ ܛܟ ܡܡܪܚ ܐܢܫ ܠܡܡܬ ܀
8Lakini Mungu amethibitisha kwamba anatupenda, maana wakati tulipokuwa bado wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
8ܗܪܟܐ ܡܚܘܐ ܐܠܗܐ ܚܘܒܗ ܕܠܘܬܢ ܕܐܢ ܟܕ ܚܛܝܐ ܐܝܬܝܢ ܗܘܝܢ ܡܫܝܚܐ ܚܠܦܝܢ ܡܝܬ ܀
9Kwa kuwa sasa tumekubaliwa kuwa waadilifu kwa damu ya Kristo, ni dhahiri zaidi kwamba atatuokoa katika ghadhabu ya Mungu.
9ܟܡܐ ܗܟܝܠ ܝܬܝܪܐܝܬ ܢܙܕܕܩ ܗܫܐ ܒܕܡܗ ܘܒܗ ܢܬܦܨܐ ܡܢ ܪܘܓܙܐ ܀
10Maana, tulipokuwa bado adui zake, Mungu alitupatanisha naye kwa kifo cha Mwanae. Na kwa vile sasa tumepatanishwa naye, ni dhahiri zaidi kwamba tutaokolewa kwa uzima wa Kristo.
10ܐܢ ܓܝܪ ܟܕ ܐܝܬܝܢ ܒܥܠܕܒܒܐ ܐܬܪܥܝ ܥܡܢ ܐܠܗܐ ܒܡܘܬܐ ܕܒܪܗ ܟܡܐ ܗܟܝܠ ܝܬܝܪܐܝܬ ܒܬܪܥܘܬܗ ܢܚܐ ܒܚܝܘܗܝ ܀
11Wala si hayo tu, ila tunafurahi pia katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ametupatanisha na Mungu.
11ܘܠܐ ܗܟܢܐ ܒܠܚܘܕ ܐܠܐ ܐܦ ܢܫܬܒܗܪ ܒܐܠܗܐ ܒܝܕ ܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܕܒܗ ܗܘ ܗܫܐ ܩܒܠܢ ܬܪܥܘܬܐ ܀
12Kwa njia ya mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, nayo ikasababisha kifo. Hivyo kifo kimeenea katika jumuiya yote ya binadamu, kwa maana wote wametenda dhambi.
12ܐܝܟܢܐ ܓܝܪ ܕܒܝܕ ܚܕ ܒܪܢܫܐ ܥܠܬ ܚܛܝܬܐ ܠܥܠܡܐ ܘܒܝܕ ܚܛܝܬܐ ܡܘܬܐ ܘܗܟܢܐ ܒܟܠܗܘܢ ܒܢܝ ܐܢܫܐ ܥܒܪ ܡܘܬܐ ܒܗܝ ܕܟܠܗܘܢ ܚܛܘ ܀
13Kabla ya Sheria kuwako, dhambi ilikuwako ulimwenguni; lakini dhambi haiwekwi katika kumbukumbu bila sheria.
13ܥܕܡܐ ܓܝܪ ܠܢܡܘܤܐ ܚܛܝܬܐ ܟܕ ܐܝܬܝܗ ܗܘܬ ܒܥܠܡܐ ܠܐ ܚܫܝܒܐ ܗܘܬ ܚܛܝܬܐ ܡܛܠ ܕܠܝܬ ܗܘܐ ܢܡܘܤܐ ܀
14Lakini tangu wakati wa Adamu mpaka wakati wa Mose, kifo kiliwatawala hata wale ambao hawakutenda dhambi kama ile ya Adamu, ya kumwasi Mungu. Adamu alikuwa kielelezo cha yule ambaye atakuja baadaye.
14ܐܠܐ ܐܡܠܟ ܡܘܬܐ ܡܢ ܐܕܡ ܘܥܕܡܐ ܠܡܘܫܐ ܐܦ ܥܠ ܐܝܠܝܢ ܕܠܐ ܚܛܘ ܒܕܡܘܬܐ ܕܥܒܪ ܢܡܘܤܗ ܕܐܕܡ ܗܘ ܕܐܝܬܘܗܝ ܕܡܘܬܐ ܕܗܘ ܕܥܬܝܕ ܀
15Lakini ipo tofauti: neema ya Mungu si kama dhambi ya Adamu. Maana, ingawa dhambi ya mtu mmoja ilisababisha kifo kwa wote, kwa fadhili ya mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, Mungu amewazidishia wote neema na zawadi zake.
15ܐܠܐ ܠܐ ܗܘܐ ܐܝܟ ܫܘܪܥܬܐ ܗܟܢܐ ܡܘܗܒܬܐ ܐܢ ܓܝܪ ܡܛܠ ܫܘܪܥܬܗ ܕܚܕ ܤܓܝܐܐ ܡܝܬܘ ܟܡܐ ܗܟܝܠ ܝܬܝܪܐܝܬ ܛܝܒܘܬܗ ܕܐܠܗܐ ܘܡܘܗܒܬܗ ܡܛܠ ܚܕ ܒܪܢܫܐ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܒܤܓܝܐܐ ܬܬܝܬܪ ܀
16Kuna tofauti baina ya zawadi ya Mungu, na dhambi ya mtu yule mmoja. Maana, baada ya kosa la mtu mmoja, Mungu alitoa hukumu; lakini baada ya makosa ya watu wengi, Mungu aliwapa zawadi yake kwa kuwasamehe.
16ܘܠܐ ܐܝܟ ܤܟܠܘܬܐ ܕܚܕ ܗܟܢܐ ܡܘܗܒܬܐ ܕܝܢܐ ܓܝܪ ܕܗܘܐ ܡܢ ܚܕ ܠܚܘܝܒܐ ܗܘܐ ܡܘܗܒܬܐ ܕܝܢ ܡܢ ܚܛܗܐ ܤܓܝܐܐ ܗܘܬ ܠܟܐܢܘ ܀
17Kweli, kwa dhambi ya mtu mmoja kifo kilianza kutawala kwa sababu ya huyo mtu mmoja; lakini, ni dhahiri zaidi kwamba alichokifanya yule mtu mmoja, yaani Yesu Kristo, ni bora zaidi. Wote wanaopokea neema na zawadi hiyo ya kukubaliwa kuwa waadilifu, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mmoja, yaani Yesu Kristo.
17ܐܢ ܓܝܪ ܡܛܠ ܤܟܠܘܬܐ ܕܚܕ ܐܡܠܟ ܡܘܬܐ ܝܬܝܪܐܝܬ ܐܝܠܝܢ ܕܢܤܒܘ ܤܘܓܐܐ ܕܛܝܒܘܬܐ ܘܕܡܘܗܒܬܐ ܘܕܟܐܢܘܬܐ ܒܚܝܐ ܢܡܠܟܘܢ ܒܝܕ ܚܕ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
18Basi, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta hukumu kwa binadamu wote, kadhalika kitendo kimoja kiadilifu kinawapa uhuru na uzima.
18ܐܟܙܢܐ ܗܟܝܠ ܕܡܛܠ ܤܟܠܘܬܐ ܕܚܕ ܗܘܐ ܚܘܝܒܐ ܠܟܠܗܘܢ ܒܢܝܢܫܐ ܗܟܢܐ ܡܛܠ ܟܐܢܘܬܐ ܕܚܕ ܬܗܘܐ ܙܟܘܬܐ ܠܚܝܐ ܠܟܠܗܘܢ ܒܢܝܢܫܐ ܀
19Na kama kwa kutotii kwa mtu mmoja watu wengi walifanywa wenye dhambi, kadhalika kutii kwa mtu mmoja kutawafanya wengi wakubaliwe kuwa waadilifu.
19ܐܝܟܢܐ ܓܝܪ ܕܡܛܠ ܠܐ ܡܫܬܡܥܢܘܬܗ ܕܚܕ ܒܪܢܫܐ ܚܛܝܐ ܤܓܝܐܐ ܗܘܘ ܗܟܢܐ ܐܦ ܡܛܠ ܡܫܬܡܥܢܘܬܗ ܕܚܕ ܤܓܝܐܐ ܟܐܢܐ ܗܘܝܢ ܀
20Sheria ilitokea, ikasababisha kuongezeka kwa uhalifu; lakini pale dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi.
20ܡܥܠܢܐ ܕܝܢ ܕܗܘܐ ܠܢܡܘܤܐ ܕܬܤܓܐ ܚܛܝܬܐ ܘܟܪ ܕܤܓܝܬ ܚܛܝܬܐ ܬܡܢ ܐܬܝܬܪܬ ܛܝܒܘܬܐ ܀
21Kama vile dhambi ilivyotawala kwa kifo, kadhalika neema inatawala kwa njia ya uadilifu, na kuleta uzima wa milele kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.
21ܕܐܝܟ ܕܐܡܠܟܬ ܚܛܝܬܐ ܒܡܘܬܐ ܗܟܢܐ ܬܡܠܟ ܛܝܒܘܬܐ ܒܟܐܢܘܬܐ ܠܚܝܐ ܕܠܥܠܡ ܒܝܕ ܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀