Swahili: New Testament

Turkish

Galatians

3

1Enyi Wagalatia, mmekuwa wajinga kweli! Ni nani aliyewaloga? Habari juu ya kusulubiwa kwake Yesu Kristo ilielezwa waziwazi mbele ya macho yenu.
1Ey akılsız Galatyalılar! Sizi kim büyüledi? İsa Mesih çarmıha gerilmiş olarak gözlerinizin önünde tasvir edilmedi mi?
2Napenda kujua tu kitu kimoja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kutimiza matakwa ya Sheria ama kwa sababu ya kuisikia na kuiamini Habari Njema?
2Sizden yalnız şunu öğrenmek istiyorum: Kutsal Ruhu, Yasanın gereklerini yaparak mı, yoksa duyduklarınıza iman ederek mi aldınız?
3Je, mu wajinga kiasi hicho? Ninyi mlianza yote kwa msaada wa Roho je, mnataka sasa kumaliza kwa nguvu zenu wenyewe?
3Bu kadar akılsız mısınız? Ruhla başladıktan sonra şimdi insan çabasıyla mı bitirmeye çalışıyorsunuz?
4Je, mambo yale yote yaliyowapata ninyi yamekuwa bure tu? Haiwezekani!
4Boş yere mi bu kadar acı çektiniz? Gerçekten boşuna mıydı?
5Je, Mungu huwajalia Roho na kutenda miujiza kati yenu ati kwa sababu mnatimiza yanayotakiwa na sheria, ama kwa sababu mnasikia Habari Njema na kuiamini?
5Size Kutsal Ruhu veren ve aranızda mucizeler yaratan Tanrı, bunu Yasanın gereklerini yaptığınız için mi, yoksa duyduklarınıza iman ettiğiniz için mi yapıyor?
6Chukueni kwa mfano habari za Abrahamu: yeye alimwamini Mungu, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.
6Örneğin, ‹‹İbrahim Tanrıya iman etti, böylece aklanmış sayıldı.››
7Sasa basi jueni kwamba watu wenye kumwamini ndio walio watoto halisi wa Abrahamu.
7Öyleyse şunu bilin ki, İbrahimin gerçek oğulları iman edenlerdir.
8Maandiko Matakatifu yalionyesha kabla kwamba Mungu atawakubali watu wa mataifa kuwa waadilifu kwa njia ya imani. Hivyo Maandiko Matakatifu yalitangulia kumtangazia Abrahamu Habari Njema: "Katika wewe mataifa yote yatabarikiwa."
8Kutsal Yazı, Tanrının öteki ulusları imanlarına göre aklayacağını önceden görerek İbrahime, ‹‹Bütün uluslar senin aracılığınla kutsanacak›› müjdesini önceden verdi.
9Basi, wale walio na imani wanabarikiwa pamoja na Abrahamu aliyeamini.
9Böylece iman edenler, iman etmiş olan İbrahimle birlikte kutsanırlar.
10Lakini wote wanaotegemea tu kutimiza yanayotakiwa na Sheria, wako chini ya laana. Maana, Maandiko Matakatifu yasema: "Yeyote asiyeshika na kutimiza yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria, yuko chini ya laana."
10Yasanın gereklerini yapmış olmaya güvenenlerin hepsi lanet altındadır. Çünkü şöyle yazılmıştır: ‹‹Yasa Kitabında yazılı olan her şeyi sürekli yerine getirmeyen herkes lanetlidir.››
11Ni dhahiri kwamba Sheria haiwezi kumfanya mtu akubaliwe kuwa mwadilifu; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
11Tanrı katında hiç kimsenin Yasayla aklanmadığı açıktır. Çünkü ‹‹İmanla aklanan yaşayacaktır.››
12Lakini Sheria haitegemei imani, ila Maandiko yasema: "Mwenye kutimiza yanayotakiwa na Sheria ataishi."
12Yasa imana dayalı değildir. Tersine, ‹‹Yasanın gereklerini yapan, onlar sayesinde yaşayacaktır.››
13Kristo alitukomboa kutoka katika laana ya Sheria kwa kujitwalia laana hiyo kwa ajili yetu; maana Maandiko yanasema: "Yeyote aliyetundikwa msalabani amelaaniwa."
13İbrahime sağlanan kutsama Mesih İsa aracılığıyla uluslara sağlansın ve bizler vaat edilen Ruhu imanla alalım diye, Mesih bizim için lanetlenerek bizi Yasanın lanetinden kurtardı. Çünkü, ‹‹Ağaç üzerine asılan herkes lanetlidir›› diye yazılmıştır.
14Jambo hili lilifanyika kusudi ile baraka aliyopewa Abrahamu iwashukie watu wa mataifa mengine kwa njia ya Kristo, na ili kwa imani, tumpokee yule Roho ambaye Mungu alituahidia.
15Kardeşler, insan yaşamından bir örnek vereyim. İnsanlar arasında yapılmış bile olsa, onaylanmış bir antlaşmayı kimse geçersiz saymaz, ona bir şey eklemez.
15Ndugu, nitawapeni mfano kutoka maisha yetu ya kila siku. Fikirini juu ya mkataba kati ya watu wawili. Mkataba ukisha fanyika na kutiwa sahihi hapana mtu anayeuweka kando au kuuongezea kitu.
16Vaatler İbrahime ve soyundan olana verildi. Tanrı birçok kişiden söz ediyormuş gibi, ‹‹Ve soyundan olanlara›› demiyor; ‹‹Soyundan olana›› demekle tek bir kişiden, yani Mesihten söz ediyor.
16Basi, Abrahamu alipewa ahadi, yeye pamoja na mzawa wake. Maandiko hayasemi: "Na wazawa wake," yaani wengi, bali yasema, "Na mzawa wake," yaani mmoja, naye ndiye Kristo.
17Şunu demek istiyorum: Dört yüz otuz yıl sonra gelen Yasa, Tanrının önceden onayladığı antlaşmayı geçersiz kılmaz, vaadi ortadan kaldırmaz.
17Ninachotaka kusema ni hiki: Mungu alifanya agano lake akalithibitisha; Sheria ambayo ilitokea miaka mia nne na thelathini baadaye, haiwezi kulitangua hilo agano wala kuibatilisha hiyo ahadi.
18Çünkü miras Yasaya bağlıysa, artık vaade bağlı değildir. Ama Tanrı mirası İbrahime vaatle bağışlamıştır.
18Maana, kama urithi ya Mungu inategemea Sheria, basi, haiwezi kutegemea tena ahadi ya Mungu. Kumbe, lakini Mungu alimkirimia Abrahamu kwa sababu aliahidi.
19Öyleyse Yasanın amacı neydi? Yasa suçları ortaya çıkarmak için antlaşmaya eklendi. Vaadi alan ve İbrahimin soyundan olan Kişi gelene dek yürürlükte kalacaktı. Melekler yoluyla, bir aracı eliyle düzenlendi.
19Ya nini basi, Sheria? Iliongezwa hapo ili kuonyesha uhalifu ni kitu gani, mpaka atakapokuja yule mzawa wa Abrahamu aliyepewa ile ahadi. Sheria ililetwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20Aracı tek bir tarafa ait değildir; Tanrı ise birdir.
20Ama hakika, mpatanishi hahitajiwi ikiwa jambo lenyewe lamhusu mtu mmoja; na Mungu ni mmoja.
21Öyleyse Kutsal Yasa Tanrının vaatlerine aykırı mıdır? Kesinlikle hayır! Çünkü yaşam sağlayabilen bir yasa verilseydi, elbette insanlar yasayla aklanırdı.
21Je, Sheria inapingana na ahadi za Mungu? Hata kidogo! Maana, kama kungalitolewa sheria ambayo ingeweza kuwapa watu uzima, basi, tungeweza kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Sheria.
22Oysa İsa Mesihe olan imana dayanan vaat iman edenlere verilsin diye, Kutsal Yazı bütün dünyayı günahın tutsağı ilan ediyor.
22Lakini sivyo; Maandiko Matakatifu yamekwisha sema kwamba ulimwengu wote upo chini ya utawala wa dhambi; na hivyo, kwa kumwamini Yesu Kristo, wenye kuamini watimiziwe ile ahadi.
23Bu iman gelmeden önce Yasa altında hapsedilmiştik, gelecek iman açıklanıncaya dek Yasanın tutuklusuyduk.
23Kabla ya kujaliwa imani, Sheria ilitufanya wafungwa mpaka imani hiyo iliyokuwa inakuja ifunuliwe.
24Yani imanla aklanalım diye Mesihin gelişine dek Yasa eğitmenimiz oldu.
24Basi, hiyo Sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani, tukubaliwe kuwa waadilifu.
25Ama iman gelmiş olduğundan, artık Yasanın denetiminde değiliz.
25Tangu kufika kwa hiyo imani, Sheria si mlezi wetu tena.
26Çünkü Mesih İsaya iman ettiğiniz için hepiniz Tanrının oğullarısınız.
26Kwa njia ya imani, ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika kuungana na Kristo.
27Vaftizde Mesihle birleşenlerinizin hepsi Mesihi giyindi.
27Ninyi nyote mliobatizwa mkaungana na Kristo ni kama vile mmemvaa Kristo.
28Artık ne Yahudi ne Grek, ne köle ne özgür, ne erkek ne dişi ayrımı var. Hepiniz Mesih İsada birsiniz.
28Hivyo, hakuna tena tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki, mtumwa na mtu huru, mwanamume na mwanamke. Nyote ni kitu kimoja katika kuungana na Kristo Yesu.
29Eğer Mesih'e aitseniz, İbrahim'in soyundansınız, vaade göre de mirasçısınız.
29Ikiwa ninyi ni wa Kristo, basi ni wazawa wa Abrahamu, na mtapokea yale aliyoahidi Mungu.