Swahili: New Testament

Turkish

Revelation

13

1(G12-18) Na likajisimamia ukingoni mwa bahari. (G13-1) Kisha nikaona mnyama mmoja akitoka baharini. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kila pembe ilikuwa na taji. Jina la kashfa lilikuwa limeandikwa juu ya vichwa hivyo.
1Sonra on boynuzlu, yedi başlı bir canavarın denizden çıktığını gördüm. Boynuzlarının üzerinde on taç vardı, başlarının üzerinde küfür niteliğinde adlar yazılıydı.
2Mnyama huyo niliyemwona alikuwa kama chui; miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na kinywa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu yake, kiti chake cha enzi na uwezo mkuu.
2Gördüğüm canavar parsa benziyordu. Ayakları ayı ayağı, ağzı aslan ağzı gibiydi. Ejderha canavara kendi gücü ve tahtıyla birlikte büyük yetki verdi.
3Kichwa kimojawapo cha huyo mnyama kilionekana kama kilikwisha jeruhiwa vibaya sana, lakini jeraha hilo lilikuwa limepona. Dunia nzima ilishangazwa na huyo mnyama na kumfuata.
3Canavarın başlarından biri ölümcül bir yara almışa benziyordu. Ne var ki, bu ölümcül yara iyileşmişti. Bütün dünya şaşkınlık içinde canavarın ardından gitti.
4Watu wote wakaliabudu lile joka kwa sababu lilimpa huyo mnyama uwezo wake. Wakamwabudu pia huyo mnyama wakisema, "Nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana naye?"
4İnsanlar canavara yetki veren ejderhaya taptılar. ‹‹Canavar gibisi var mı? Onunla kim savaşabilir?›› diyerek canavara da taptılar.
5Kisha huyo mnyama akaruhusiwa kusema maneno ya kujigamba na kumkufuru Mungu; akaruhusiwa kuwa na mamlaka kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
5Canavara, kurumlu sözler söyleyen, küfürler savuran bir ağız ve kırk iki ay süreyle kullanabileceği bir yetki verildi.
6Basi, akaanza kumtukana Mungu, kulitukana jina lake, makao yake, na wote wakaao mbinguni.
6Tanrıya küfretmek, Onun adına ve konutuna, yani gökte yaşayanlara küfretmek için ağzını açtı.
7Aliruhusiwa kuwapiga vita na kuwashinda watu wa Mungu. Alipewa mamlaka juu ya watu wa kila kabila, ukoo, lugha na taifa.
7Kutsallarla savaşıp onları yenmesine izin verildi. Canavar her oymak, her halk, her dil, her ulus üzerinde yetkili kılındı.
8Wote waishio duniani watamwabudu isipokuwa tu wale ambao majina yao yameandikwa tangu mwanzo wa ulimwengu katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo aliyechinjwa.
8Yeryüzünde yaşayan ve dünya kurulalı beri boğazlanmış Kuzunun yaşam kitabına adı yazılmamış olan herkes ona tapacak.
9"Aliye na masikio, na asikie!
9Kulağı olan işitsin!
10Waliokusudiwa kuchukuliwa mateka lazima watatekwa; waliokusudiwa kuuawa kwa upanga lazima watauawa kwa upanga. Kutokana na hayo ni lazima watu wa Mungu wawe na uvumilivu na imani."
10Tutsak düşecek olan Tutsak düşecek. Kılıçla öldürülecek olan Kılıçla öldürülecek.
11Kisha nikamwona mnyama mwingine anatoka ardhini. Alikuwa na pembe mbili kama pembe za kondoo, na aliongea kama joka.
11Bundan sonra başka bir canavar gördüm. Yerden çıkan bu canavarın kuzu gibi iki boynuzu vardı, ama ejderha gibi ses çıkarıyordu.
12Alikuwa na mamlaka kamili kutoka kwa yule mnyama wa kwanza, na akautumia uwezo huo mbele ya huyo mnyama. Akailazimisha dunia yote na wote waliomo humo kumwabudu huyo mnyama wa kwanza ambaye alikuwa na jeraha la kifo lililokuwa limepona.
12İlk canavarın bütün yetkisini onun adına kullanıyor, yeryüzünü ve orada yaşayanları ölümcül yarası iyileşen ilk canavara tapmaya zorluyordu.
13Basi, huyu mnyama wa pili akafanya miujiza mikubwa hata akasababisha moto kutoka mbinguni ushuke duniani mbele ya watu.
13İnsanların gözü önünde, gökten yere ateş yağdıracak kadar büyük belirtiler gerçekleştiriyordu.
14Aliwapotosha wakazi wa dunia kwa miujiza hiyo aliyojaliwa kutenda mbele ya mnyama wa kwanza. Aliwaambia wakazi wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi tena.
14İlk canavarın adına gerçekleştirmesine izin verilen belirtiler sayesinde, yeryüzünde yaşayanları saptırdı. Onlara kılıçla yaralanan, ama sağ kalan canavarın onuruna bir heykel yapmalarını buyurdu.
15Kisha alijaliwa kuipulizia uhai hiyo sanamu ya yule mnyama wa kwanza, hata ikaweza kuongea na kuwaua watu wote ambao hawakuiabudu.
15Canavarın heykeline yaşam soluğu vermesi için kendisine güç verildi. Öyle ki, heykel konuşabilsin ve kendisine tapmayan herkesi öldürebilsin.
16Aliwalazimisha wote, wadogo na wakubwa, matajiri na maskini, watu huru na watumwa, watiwe alama juu ya mikono yao ya kulia au juu ya paji za nyuso zao.
16Küçük büyük, zengin yoksul, özgür köle, herkesin sağ eline ya da alnına bir işaret vurduruyordu.
17Akapiga marufuku mtu yeyote kununua au kuuza kitu isipokuwa tu mtu aliyetiwa alama hiyo, yaani jina la yule mnyama au tarakimu ya jina hilo.
17Öyle ki, bu işareti, yani canavarın adını ya da adını simgeleyen sayıyı taşımayan ne bir şey satın alabilsin, ne de satabilsin.
18Hapa ni lazima kutumia ujasiri! Mwenye akili anaweza kufafanua maana ya tarakimu ya mnyama huyo, maana ni tarakimu yenye maana ya mtu fulani. Tarakimu hiyo ni mia sita sitini na sita.
18Bu konu bilgelik gerektirir. Anlayabilen, canavara ait sayıyı hesaplasın. Çünkü bu sayı insanı simgeler. Sayısı 666'dır.