Swahili: New Testament

Turkish

Revelation

17

1Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na bakuli akaja, akaniambia, "Njoo, mimi nitakuonyesha adhabu aliyopewa yule mzinzi mkuu, mji ule uliojengwa juu ya maji mengi.
1Yedi tası alan yedi melekten biri gelip benimle konuştu: ‹‹Gel!›› dedi. ‹‹Sana engin suların kenarında oturan büyük fahişenin çarptırılacağı cezayı göstereyim.
2Wafalme wa dunia wamefanya uzinzi pamoja naye; na wakazi wa dunia wamelewa divai ya uzinzi wake."
2Dünya kralları onunla fuhuş yaptılar. Yeryüzünde yaşayanlar onun fuhşunun şarabıyla sarhoş oldular.››
3Kisha, Roho akanikumba, akaniongoza mpaka jangwani. Huko nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama mwekundu. Mnyama huyo alikuwa ameandikwa kila mahali majina ya makufuru; alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
3Bundan sonra melek beni Ruhun yönetiminde çöle götürdü. Orada yedi başlı, on boynuzlu, üzeri küfür niteliğinde adlarla kaplı kırmızı bir canavarın üstüne oturmuş bir kadın gördüm.
4Mwanamke huyo alikuwa amevaa vazi la rangi ya zambarau na nyekundu; alikuwa amejipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu. Mkononi mwake alishika kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa machukizo na mambo machafu yanayoonyesha uzinzi wake.
4Kadın, mor ve kırmızı giysilere bürünmüş, altınlar, değerli taşlar, incilerle süslenmişti. Elinde iğrenç şeylerle, fuhşunun çirkeflikleriyle dolu altın bir kâse vardı.
5Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina la fumbo "Babuloni mkuu, mama wa wazinzi na wa mambo yote ya kuchukiza sana duniani."
5Alnına şu gizemli ad yazılmıştı: BÜYÜK BABİL, DÜNYA FAHİŞELERİNİN VE İĞRENÇLİKLERİNİN ANASI
6Nikamwona huyo mwanamke amelewa damu ya watu wa Mungu, na damu ya watu waliouawa kwa sababu ya kumtangaza Yesu. Nilipomwona nilishangaa mno.
6Kadının, kutsalların ve İsaya tanıklık etmiş olanların kanıyla sarhoş olduğunu gördüm. Onu görünce büyük bir şaşkınlığa düştüm.
7Lakini malaika akaniambia, "Kwa nini unashangaa? Mimi nitakuambia maana iliyofichika ya mwanamke huyu na mnyama huyo amchukuaye ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.
7Melek bana, ‹‹Neden şaştın?›› diye sordu. ‹‹Kadının ve onu taşıyan yedi başlı, on boynuzlu canavarın sırrını ben sana açıklayayım.
8Huyo mnyama uliyemwona alikuwa hai hapo awali, lakini sasa amekufa. Hata hivyo, karibu sana atapanda kutoka shimoni kuzimu, lakini ataangamizwa. Wanaoishi duniani watashangaa; naam, watu wote ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangu mwanzo wa ulimwengu, watashangaa kumwona huyo mnyama ambaye hapo awali, aliishi, kisha akafa na sasa anatokea tena!
8Gördüğün canavar bir zamanlar vardı, ama şimdi yok. Biraz sonra dipsiz derinliklerden çıkacak ve yıkıma gidecek. Yeryüzünde yaşayan ve dünya kurulalı beri adları yaşam kitabına yazılmamış olanlar canavarı görünce şaşacaklar. Çünkü o bir zamanlar vardı, şimdi yok, ama yine gelecek.
9"Hapa panahitaji akili na hekima! Hivyo vichwa saba ni vilima saba, na huyo mwanamke anaketi juu yake. Vichwa hivyo pia ni wafalme saba.
9‹‹Bunu anlamak için bilgelik gerek. Yedi baş, kadının üzerinde oturduğu yedi tepedir; aynı zamanda yedi kraldır.
10Kati ya hao wafalme saba, watano wamekwisha angamia, mmoja anatawala bado, na yule mwingine bado hajafika; na atakapofika atabaki kwa muda mfupi.
10Bunların beşi düştü, biri duruyor, ötekiyse henüz gelmedi. Gelince kısa süre kalması gerek.
11Huyo mnyama ambaye alikuwa anaishi hapo awali lakini sasa haishi tena ni mfalme wa nane, naye pia ni miongoni mwa hao saba, na anakwenda zake kuharibiwa.
11Yaşamış, ama şimdi yok olan canavarın kendisi sekizinci kraldır. O da yedilerden biridir ve yıkıma gitmektedir.
12"Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme ambao bado hawajaanza kutawala. Lakini watapewa mamlaka ya kutawala kwa muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
12Gördüğün on boynuz henüz egemenlik sürmemiş on kraldır; canavarla birlikte bir saat egemenlik sürmek üzere yetki alacaklar.
13Shabaha ya hawa kumi ni moja, na watampa yule mnyama nguvu na mamlaka yao yote.
13Düşünce birliği içinde olan bu krallar güçlerini ve yetkilerini canavara verecekler.
14Watapigana na Mwanakondoo, lakini Mwanakondoo pamoja na wale aliowaita na kuwachagua, ambao ni waaminifu, atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme."
14Kuzuya karşı savaşacaklar, ama Kuzu onları yenecek. Çünkü Kuzu, rablerin Rabbi, kralların Kralıdır. Onunla birlikte olanlar, çağrılmış, seçilmiş ve Ona sadık kalmış olanlardır.››
15Malaika akaniambia pia, "Yale maji uliyoyaona pale alipokaa yule mzinzi, ni mataifa, watu wa kila rangi na lugha.
15Bundan sonra melek bana, ‹‹Şu gördüğün sular -fahişenin kenarında oturduğu sular- halklar, toplumlar, uluslar ve dillerdir›› dedi.
16Pembe zile kumi ulizoziona na yule mnyama watamchukia huyo mzinzi. Watachukua kila kitu alicho nacho na kumwacha uchi; watakula nyama yake na kumteketeza kwa moto.
16‹‹Gördüğün canavarla on boynuz fahişeden nefret edecek, onu perişan edip çıplak bırakacaklar. Etini yiyip kendisini ateşte yakacaklar.
17Maana Mungu ametia mioyoni mwao nia ya kutekeleza shabaha yake, yaani kwa kukubaliana wao kwa wao na kumpa huyo mnyama mamlaka yao ya kutawala, mpaka hapo neno la Mungu litakapotimia.
17Çünkü Tanrı, amacını gerçekleştirme isteğini onların yüreğine koymuştur. Öyle ki, Tanrının sözleri yerine gelinceye dek krallıklarını canavara devretmekte sözbirliği edecekler.
18"Na yule mwanamke uliyemwona ndio ule mji mkuu unaowatawala wafalme wa dunia."
18Gördüğün kadın dünya kralları üzerinde egemenlik süren büyük kenttir.››