Swahili: New Testament

Turkish

Revelation

22

1Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
1Melek bana Tanrının ve Kuzunun tahtından çıkan billur gibi berrak yaşam suyu ırmağını gösterdi.
2Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
2Kentin anayolunun ortasında akan ırmağın iki yanında on iki çeşit meyve üreten ve her ay meyvesini veren yaşam ağacı bulunuyordu. Ağacın yaprakları uluslara şifa vermek içindir.
3Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
3Artık hiçbir lanet kalmayacak. Tanrının ve Kuzunun tahtı kentin içinde olacak, kulları Ona tapınacak.
4Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
4Onun yüzünü görecek, alınlarında Onun adını taşıyacaklar.
5Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele.
5Artık gece olmayacak. Çıra ışığına da güneş ışığına da gereksinmeleri olmayacak. Çünkü Rab Tanrı onlara ışık verecek ve sonsuzlara dek egemenlik sürecekler.
6Kisha malaika akaniambia, "Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
6Melek bana, ‹‹Bu sözler güvenilir ve gerçektir›› dedi. ‹‹Peygamberlerin ruhlarının Tanrısı olan Rab, yakın zamanda olması gereken olayları kullarına göstermek için meleğini gönderdi.››
7"Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki."
7‹‹İşte tez geliyorum! Bu kitaptaki peygamberlik sözlerine uyana ne mutlu!››
8Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
8Bunları işiten ve gören ben Yuhannayım. İşitip gördüğümde bunları bana gösteren meleğe tapmak için ayaklarına kapandım.
9Lakini yeye akaniambia, "Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!"
9Ama o bana, ‹‹Sakın yapma!›› dedi, ‹‹Ben senin, peygamber kardeşlerin ve bu kitabın sözlerine uyanlar gibi bir Tanrı kuluyum. Tanrıya tap!››
10Tena akaniambia, "Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
10Sonra bana, ‹‹Bu kitabın peygamberlik sözlerini mühürleme›› dedi, ‹‹Çünkü beklenen zaman yakındır.
11Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu."
11Kötülük yapan, yine kötülük yapsın. Kirli olan, kirli işlerini sürdürsün. Doğru olan, yine doğruyu yapsın. Kutsal olan kutsal kalsın.››
12"Sikiliza!" Asema Yesu, "Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
12‹‹İşte tez geliyorum! Vereceğim ödüller yanımdadır. Herkese yaptığının karşılığını vereceğim.
13Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho."
13Alfa ve Omega, birinci ve sonuncu, başlangıç ve son Benim.
14Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
14‹‹Kaftanlarını yıkayan, böylelikle yaşam ağacından yemeye hak kazanarak kapılardan geçip kente girenlere ne mutlu!
15Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
15Köpekler, büyücüler, fuhuş yapanlar, adam öldürenler, putperestler, yalanı sevip hile yapanların hepsi dışarıda kalacaklar.
16"Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!"
16‹‹Ben İsa, kiliselerle ilgili bu tanıklığı sizlere iletsin diye meleğimi gönderdim. Davutun kökü ve soyu Benim, parlak sabah yıldızı Benim.››
17Roho na Bibiarusi waseme, "Njoo!" Kila mtu asikiaye hili, na aseme, "Njoo!" Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
17Ruh ve Gelin, ‹‹Gel!›› diyorlar. İşiten, ‹‹Gel!›› desin. Susayan gelsin. Dileyen, yaşam suyundan karşılıksız alsın.
18Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
18Bu kitaptaki peygamberlik sözlerini duyan herkesi uyarıyorum! Her kim bu sözlere bir şey katarsa, Tanrı da bu kitapta yazılı belaları ona katacaktır.
19Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
19Her kim bu peygamberlik kitabının sözlerinden bir şey çıkarırsa, Tanrı da bu kitapta yazılı yaşam ağacından ve kutsal kentten ona düşen payı çıkaracaktır.
20Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: "Naam! Naja upesi." Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
20Bunlara tanıklık eden, ‹‹Evet, tez geliyorum!›› diyor. Amin! Gel, ya Rab İsa!
21Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.
21Rab İsa'nın lütfu kutsallarla birlikte olsun! Amin.