Swahili: New Testament

Turkish: New Testament

Acts

21

1Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
1Onlardan ayrılınca denize açılıp doğru İstanköy'e gittik. Ertesi gün Rodos'a, oradan da Patara'ya geçtik.
2Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
2Fenike'ye gidecek bir gemi bulduk, buna binip denize açıldık.
3Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
3Kıbrıs'ı görünce güneyinden geçerek Suriye'ye yöneldik ve Sur kentinde karaya çıktık. Gemi, yükünü orada boşaltacaktı.
4Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
4Oradaki İsa öğrencilerini arayıp bulduk ve yanlarında bir hafta kaldık. Öğrenciler, Ruh'un yönlendirmesiyle Pavlus'u, Kudüs'e gitmemesi için uyardılar.
5Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
5Günümüz dolunca kentten ayrılıp yolumuza devam ettik. İmanlıların hepsi, eşleri ve çocuklarıyla birlikte bizi kentin dışına kadar geçirdiler. Deniz kıyısında diz çöküp dua ettik.
6Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
6Birbirimizle vedalaştıktan sonra biz gemiye bindik, onlar da evlerine döndüler.
7Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
7Sur'dan deniz yolculuğumuza devam ederek Batlamya kentine geldik. Oradaki kardeşleri ziyaret edip bir gün yanlarında kaldık.
8Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
8Ertesi gün ayrılıp Sezariye'ye geldik. Yedilerden biri olan müjdeci Filipus'un evine giderek onun yanında kaldık.
9Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
9Bu adamın peygamberlik eden, evlenmemiş dört kızı vardı.
10Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
10Oraya varışımızdan birkaç gün sonra Yahudiye'den Agabus adlı bir peygamber geldi.
11Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema "Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa."
11Bu adam bize yaklaşıp Pavlus'un kuşağını aldı, bununla kendi ellerini ayaklarını bağlayarak dedi ki, «Kutsal Ruh şöyle diyor: `Yahudiler, bu kuşağın sahibini Kudüs'te böyle bağlayıp diğer uluslara teslim edecekler.'»
12Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
12Bu sözleri duyunca hem bizler hem de oralılar Kudüs'e gitmemesi için Pavlus'a yalvardık.
13Lakini yeye alijibu, "Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu."
13Bunun üzerine Pavlus şöyle karşılık verdi: «Ne yapıyorsunuz, ne diye ağlayıp yüreğimi sızlatıyorsunuz? Ben Rab İsa'nın adı uğruna Kudüs'te yalnız bağlanmaya değil, ölmeye de hazırım.»
14Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: "Mapenzi ya Bwana yafanyike"
14Pavlus'u ikna edemeyince, «Rab'bin istediği olsun» diyerek sustuk.
15Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
15Bir süre sonra hazırlığımızı yapıp Kudüs'e doğru yola çıktık.
16Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
16Sezariye'deki öğrencilerden bazıları da bizimle birlikte geldiler. Bizi, evinde kalacağımız adama, eski öğrencilerden Kıbrıslı Minason'a götürdüler.
17Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
17Kudüs'e vardığımız zaman kardeşler bizi sevinçle karşıladılar.
18Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
18Ertesi gün Pavlus'la birlikte Yakup'u görmeye gittik. İhtiyarların hepsi de orada toplanmıştı.
19Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
19Pavlus, onların hal hatırını sorduktan sonra hizmetinin aracılığıyla Tanrı'nın diğer uluslar arasında yaptıklarını teker teker anlattı.
20Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, "Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
20Bunları işitince Tanrı'yı yücelttiler. Pavlus'a, «Görüyorsun kardeş, Yahudiler arasında binlerce imanlı var ve hepsi Kutsal Yasa'nın candan savunucusudur» dediler.
21Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
21«Ne var ki, duyduklarına göre sen diğer uluslar arasında yaşayan bütün Yahudilere, çocuklarını sünnet etmemelerini, törelerimize uymamalarını söylüyor, Musa'nın yasasına sırt çevirmeleri gerektiğini öğretiyormuşsun.
22Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
22Şimdi ne yapmalı? Senin buraya geldiğini mutlaka duyacaklar.
23Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
23Bunun için sana dediğimizi yap. Aramızda adak adamış dört kişi var.
24Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
24Bunları yanına al, kendileriyle birlikte arınma törenine katıl. Başlarını traş edebilmeleri için kurban masraflarını sen öde. Böylelikle herkes, seninle ilgili duyduklarının asılsız olduğunu, senin de Kutsal Yasa'ya uygun olarak yaşadığını anlasın.
25Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati."
25Diğer uluslardan olan imanlılara gelince, biz onlara, putlara sunulan kurbanların etinden, kandan, boğularak öldürülen hayvanlardan ve cinsel ahlaksızlıktan sakınmalarını öngören kararımızı yazmıştık.»
26Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
26Bunun üzerine Pavlus o dört kişiyi yanına aldı, ertesi gün onlarla birlikte arınma törenine katıldı. Sonra tapınağa girerek arınma günlerinin ne zaman tamamlanacağını, her birinin adına ne zaman kurban sunulacağını bildirdi.
27Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
27Yedi günlük süre bitmek üzereydi. Asya ilinden bazı Yahudiler Pavlus'u tapınakta görünce tüm kalabalığı kışkırtarak onu yakaladılar.
28wakipiga kelele: "Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu."
28«Ey İsrailliler, yardım edin!» diye bağırdılar. «Her yerde herkese, halkımıza, Kutsal Yasa'ya ve bu kutsal yere karşı öğretiler yayan adam budur. Üstelik tapınağa bazı Grekleri sokarak bu kutsal yeri kirletti.»
29Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
29Bu Yahudiler, daha önce kentte Pavlus'un yanında görmüş oldukları Efesli Trofimus'un, Pavlus tarafından tapınağa sokulduğunu sanıyorlardı.
30Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
30Bütün kent ayağa kalkmıştı. Her taraftan koşuşup gelen halk Pavlus'u tutup tapınaktan dışarı sürükledi. Arkasından tapınağın kapıları hemen kapatıldı.
31Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
31Onlar Pavlus'u öldürmeye çalışırken, tüm Kudüs'ün karıştığı haberi Roma taburunun komutanına ulaştı.
32Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
32Komutan hemen yüzbaşılarla askerleri yanına alarak kalabalığın olduğu yere koşturdu. Komutanla askerleri gören halk Pavlus'u dövmeyi bıraktı.
33Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, "Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?"
33O zaman komutan yaklaşıp Pavlus'u yakaladı, iki zincirle bağlanması için buyruk verdi. Sonra, «Kimdir bu adam, ne yaptı?» diye sordu.
34Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
34Kalabalıktakilerin her biri ayrı bir şey bağırıyordu. Kargaşalıktan ötürü kesin bilgi edinemeyen komutan, Pavlus'un kaleye götürülmesini buyurdu.
35Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
35Pavlus merdivenlere geldiğinde kalabalık öylesine azmıştı ki, askerler onu taşımak zorunda kaldılar.
36Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, "Muulie mbali!"
36Kalabalık, «Öldürün onu!» diye bağırarak onları izliyordu.
37Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, "Naweza kukwambia kitu?" Yule mkuu wa jeshi akamjibu, "Je unajua Kigiriki?
37Kaleden içeri girmek üzereyken Pavlus komutana, «Sana bir şey söyleyebilir miyim?» dedi. Komutan, «Grekçe biliyor musun?» dedi.
38Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?"
38«Sen bundan bir süre önce bir ayaklanma başlatıp dört bin tedhişçiyi çöle götüren Mısırlı değil misin?»
39Paulo akajibu, "Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
39Pavlus, «Ben Kilikya'dan Tarsuslu bir Yahudi, hiç de önemsiz olmayan bir kentin vatandaşıyım» dedi. «Rica ederim, halka birkaç söz söylememe izin ver.»
40Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.
40Komutanın izin vermesi üzerine Pavlus merdivende dikilip eliyle halka bir işaret yaptı. Derin bir sessizlik olunca, İbrani dilinde konuşmaya başladı.