Swahili: New Testament

Turkish: New Testament

Galatians

2

1Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
1On dört yıl aradan sonra Titus'u da yanıma alıp Barnaba'yla birlikte yine Kudüs'e gittim.
2Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
2Tanrısal esine uyarak gittim. Boş yere koşmayayım, ya da koşmuş olmayayım diye, diğer uluslar arasında yaydığım müjdeyi özel olarak ileri gelenlere sundum.
3Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
3Benimle birlikte olan Titus bile, Grek olmasına karşın, sünnet edilmeye zorlanmadı.
4ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
4Ne var ki, İsa Mesih'te sahip olduğumuz özgürlüğü el altından öğrenmek ve böylece bizi köleleştirmek için gizlice aramıza sızan sahte kardeşler vardı.
5Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
5Müjde'nin gerçeği sizinle sürekli kalsın diye, bir an bile onlara boyun eğip teslim olmadık.
6Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi--kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje--watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
6Ama ileri gelenler - ne oldukları bence önemli değil, Tanrı insanlar arasında ayrım yapmaz - evet, bu ileri gelenler söylediklerime bir şey katmadılar.
7Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
7Tam tersine, Müjde'yi sünnetlilere bildirme işi nasıl Petrus'a verildiyse, sünnetsizlere bildirme işinin de bana verildiğini gördüler.
8Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
8Çünkü sünnetlilere elçilik etmesi için Petrus'ta etkin olan Tanrı, diğer uluslara elçilik etmem için bende de etkin oldu.
9Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
9Topluluğun direkleri sayılan Yakup, Kefas ve Yuhanna bana bağışlanan lütfu sezdikleri zaman, paydaşlığımızın işareti olarak bana ve Barnaba'ya sağ ellerini uzattılar. Diğer uluslara bizlerin, Yahudilere ise kendilerinin gitmesini uygun gördüler.
10Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
10Ancak yoksulları hatırlamamızı istediler. Ben de tam bunu yapmaya gayret ediyordum.
11Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
11Ne var ki, Kefas Antakya'ya geldiği zaman, suçlu olduğu için ona açıkça karşı geldim.
12Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
12Çünkü Yakup'un yanından bazı adamlar gelmeden önce Kefas, diğer uluslardan olanlarla beraber yemek yerdi. Ama o adamlar gelince sünnet yanlılarından korkarak sünnetsizlerden uzaklaştı, onlarla yemek yemez oldu.
13Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
13Öbür Yahudiler de onun gibi ikiyüzlülük ettiler. Öyle ki, Barnaba bile onların ikiyüzlülüğüne kapıldı.
14Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: "Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?"
14Müjde'nin gerçeğine uygun davranmadıklarını görünce hepsinin önünde Kefas'a şöyle dedim: «Sen Yahudi olduğun halde Yahudi gibi değil, diğer uluslardan biri gibi yaşıyorsan, nasıl olur da ulusları Yahudileşmeye zorlarsın?
15Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
15Biz Yahudi doğduk, diğer uluslardan olan `günahkâr'lar değiliz.
16Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
16Yine de kişinin, Kutsal Yasa'nın gereklerini yapmakla değil, İsa Mesih'e olan imanla aklandığını biliyoruz. Bunun için biz de, Yasa'nın gereklerini yapmakla değil, Mesih'e imanla aklanalım diye Mesih İsa'ya iman ettik. Çünkü hiç kimse Yasa'nın gereklerini yapmakla aklanmaz.
17Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
17Eğer biz Mesih'te aklanmak isterken günahlı çıkarsak, Mesih günahın yardakçısı mı olur? Kesinlikle hayır!
18Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
18Yıktığım şeyleri yeniden kurarsam, yasa bozucusu olduğumu kanıtlarım.
19Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
19Çünkü ben, Tanrı için yaşamak üzere Yasa'nın aracılığıyla Yasa karşısında öldüm.
20na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
20Mesih'le birlikte çarmıha gerildim. Artık ben yaşamıyorum, Mesih bende yaşıyor. Şimdi bedende sürdürdüğüm yaşamı, beni seven ve uğruma kendini feda eden Tanrı Oğluna imanla sürdürüyorum.
21Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!
21Tanrı'nın lütfunu geçersiz saymış değilim. Çünkü aklanma Yasa aracılığıyla kazanılabilseydi, o zaman Mesih boş yere ölmüş olurdu.»