1Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
1I exhort therefore, first of all, that petitions, prayers, intercessions, and givings of thanks, be made for all men:
2kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
2for kings and all who are in high places; that we may lead a tranquil and quiet life in all godliness and reverence.
3Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
3For this is good and acceptable in the sight of God our Savior;
4ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
4who desires all people to be saved and come to full knowledge of the truth.
5Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
5For there is one God, and one mediator between God and men, the man Christ Jesus,
6ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
6who gave himself as a ransom for all; the testimony in its own times;
7Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
7to which I was appointed a preacher and an apostle (I am telling the truth in Christ, not lying), a teacher of the Gentiles in faith and truth.
8Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
8I desire therefore that the men in every place pray, lifting up holy hands without anger and doubting.
9Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
9In the same way, that women also adorn themselves in decent clothing, with modesty and propriety; not just with braided hair, gold, pearls, or expensive clothing;
10bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
10but (which becomes women professing godliness) with good works.
11Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
11Let a woman learn in quietness with all subjection.
12Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
12But I don’t permit a woman to teach, nor to exercise authority over a man, but to be in quietness.
13Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
13For Adam was first formed, then Eve.
14Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
14Adam wasn’t deceived, but the woman, being deceived, has fallen into disobedience;
15Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.
15but she will be saved through her childbearing, if they continue in faith, love, and sanctification with sobriety.