Swahili: New Testament

World English Bible

2 John

1

1Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi,
1The elder, to the chosen lady and her children, whom I love in truth; and not I only, but also all those who know the truth;
2kwa sababu ukweli unakaa nasi milele.
2for the truth’s sake, which remains in us, and it will be with us forever:
3Neema na huruma na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika ukweli na upendo.
3Grace, mercy, and peace will be with us, from God the Father, and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, in truth and love.
4Nilifurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama Baba alivyotuamuru.
4I rejoice greatly that I have found some of your children walking in truth, even as we have been commanded by the Father.
5Basi, Bimkubwa, ninalo ombi moja kwako: tupendane. Ombi hili si amri mpya, bali ni amri ileile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.
5Now I beg you, dear lady, not as though I wrote to you a new commandment, but that which we had from the beginning, that we love one another.
6Upendo maana yake ni kuishi kwa kuzitii amri zake Mungu. Amri niliyoisikia tangu mwanzo ndiyo hii: mnapaswa nyote kuishi katika upendo.
6This is love, that we should walk according to his commandments. This is the commandment, even as you heard from the beginning, that you should walk in it.
7Wadanganyifu wengi wamezuka duniani, watu ambao hawakiri kwamba Yesu Kristo amekuja kwetu akawa binadamu. Mtu asemaye hivyo ni mdanganyifu na ni Adui wa Kristo.
7For many deceivers have gone out into the world, those who don’t confess that Jesus Christ came in the flesh. This is the deceiver and the Antichrist.
8Basi, jihadharini ninyi wenyewe ili msije mkapoteza kile mlichokishugulikia, bali mpate tuzo lenu kamili.
8Watch yourselves, that we don’t lose the things which we have accomplished, but that we receive a full reward.
9Asiyezingatia na kudumu katika mafundisho ya Kristo, bali anayakiuka, hana Mungu. Lakini anayedumu katika mafundisho hayo anaye Baba na Mwana.
9Whoever transgresses and doesn’t remain in the teaching of Christ, doesn’t have God. He who remains in the teaching, the same has both the Father and the Son.
10Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.
10If anyone comes to you, and doesn’t bring this teaching, don’t receive him into your house, and don’t welcome him,
11Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.
11for he who welcomes him participates in his evil works.
12Ninayo mengi ya kuwaambieni lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.
12Having many things to write to you, I don’t want to do so with paper and ink, but I hope to come to you, and to speak face to face, that our joy may be made full.
13Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.
13The children of your chosen sister greet you. Amen.