Swahili: New Testament

World English Bible

Colossians

3

1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
1If then you were raised together with Christ, seek the things that are above, where Christ is, seated on the right hand of God.
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
2Set your mind on the things that are above, not on the things that are on the earth.
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
3For you died, and your life is hidden with Christ in God.
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
4When Christ, our life, is revealed, then you will also be revealed with him in glory.
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
5Put to death therefore your members which are on the earth: sexual immorality, uncleanness, depraved passion, evil desire, and covetousness, which is idolatry;
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
6for which things’ sake the wrath of God comes on the children of disobedience.
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
7You also once walked in those, when you lived in them;
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
8but now you also put them all away: anger, wrath, malice, slander, and shameful speaking out of your mouth.
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
9Don’t lie to one another, seeing that you have put off the old man with his doings,
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
10and have put on the new man, who is being renewed in knowledge after the image of his Creator,
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
11where there can’t be Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, bondservant, freeman; but Christ is all, and in all.
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
12Put on therefore, as God’s chosen ones, holy and beloved, a heart of compassion, kindness, lowliness, humility, and perseverance;
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
13bearing with one another, and forgiving each other, if any man has a complaint against any; even as Christ forgave you, so you also do.
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
14Above all these things, walk in love, which is the bond of perfection.
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
15And let the peace of God rule in your hearts, to which also you were called in one body; and be thankful.
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
16Let the word of Christ dwell in you richly; in all wisdom teaching and admonishing one another with psalms, hymns, and spiritual songs, singing with grace in your heart to the Lord.
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
17Whatever you do, in word or in deed, do all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father, through him.
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
18Wives, be in subjection to your husbands, as is fitting in the Lord.
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
19Husbands, love your wives, and don’t be bitter against them.
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
20Children, obey your parents in all things, for this pleases the Lord.
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
21Fathers, don’t provoke your children, so that they won’t be discouraged.
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
22Servants, obey in all things those who are your masters according to the flesh, not just when they are looking, as men pleasers, but in singleness of heart, fearing God.
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
23And whatever you do, work heartily, as for the Lord, and not for men,
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
24knowing that from the Lord you will receive the reward of the inheritance; for you serve the Lord Christ.
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
25But he who does wrong will receive again for the wrong that he has done, and there is no partiality.