Swahili: New Testament

World English Bible

Ephesians

6

1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
1Children, obey your parents in the Lord, for this is right.
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
2“Honor your father and mother,” which is the first commandment with a promise:
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
3“that it may be well with you, and you may live long on the earth.”
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
4You fathers, don’t provoke your children to wrath, but nurture them in the discipline and instruction of the Lord.
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
5Servants, be obedient to those who according to the flesh are your masters, with fear and trembling, in singleness of your heart, as to Christ;
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
6not in the way of service only when eyes are on you, as men pleasers; but as servants of Christ, doing the will of God from the heart;
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
7with good will doing service, as to the Lord, and not to men;
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
8knowing that whatever good thing each one does, he will receive the same again from the Lord, whether he is bound or free.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
9You masters, do the same things to them, and give up threatening, knowing that he who is both their Master and yours is in heaven, and there is no partiality with him.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
10Finally, be strong in the Lord, and in the strength of his might.
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
11Put on the whole armor of God, that you may be able to stand against the wiles of the devil.
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
12For our wrestling is not against flesh and blood, but against the principalities, against the powers, against the world’s rulers of the darkness of this age, and against the spiritual forces of wickedness in the heavenly places.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
13Therefore put on the whole armor of God, that you may be able to withstand in the evil day, and, having done all, to stand.
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
14Stand therefore, having the utility belt of truth buckled around your waist, and having put on the breastplate of righteousness,
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
15and having fitted your feet with the preparation of the Good News of peace;
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
16above all, taking up the shield of faith, with which you will be able to quench all the fiery darts of the evil one.
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
17And take the helmet of salvation, and the sword of the Spirit, which is the word of God;
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
18with all prayer and requests, praying at all times in the Spirit, and being watchful to this end in all perseverance and requests for all the saints:
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
19on my behalf, that utterance may be given to me in opening my mouth, to make known with boldness the mystery of the Good News,
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
20for which I am an ambassador in chains; that in it I may speak boldly, as I ought to speak.
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
21But that you also may know my affairs, how I am doing, Tychicus, the beloved brother and faithful servant in the Lord, will make known to you all things;
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
22whom I have sent to you for this very purpose, that you may know our state, and that he may comfort your hearts.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
23Peace be to the brothers, and love with faith, from God the Father and the Lord Jesus Christ.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.
24Grace be with all those who love our Lord Jesus Christ with incorruptible love. Amen.