Swahili: New Testament

World English Bible

James

4

1Mapigano na magombano yote kati yenu yanatoka wapi? Hutoka katika tamaa zenu mbaya ambazo hupigana daima ndani yenu.
1Where do wars and fightings among you come from? Don’t they come from your pleasures that war in your members?
2Mnatamani vitu na kwa vile hamvipati mko tayari kuua; mwatamani sana kupata vitu, lakini hamvipati, hivyo mnagombana na kupigana. Hampati kile mnachotaka kwa sababu hamkiombi kwa Mungu.
2You lust, and don’t have. You kill, covet, and can’t obtain. You fight and make war. You don’t have, because you don’t ask.
3Tena, mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya; mnaomba ili mpate kutosheleza tamaa zenu.
3You ask, and don’t receive, because you ask with wrong motives, so that you may spend it for your pleasures.
4Ninyi ni watu msio na uaminifu kama wazinzi. Je, hamjui kwamba kuwa rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu? Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu.
4You adulterers and adulteresses, don’t you know that friendship with the world is enmity with God? Whoever therefore wants to be a friend of the world makes himself an enemy of God.
5Msifikiri kwamba Maandiko Matakatifu yamesema maneno ya bure, yanaposema: "Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu ana wivu mkubwa."
5Or do you think that the Scripture says in vain, “The Spirit who lives in us yearns jealously”?
6Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: "Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu."
6But he gives more grace. Therefore it says, “God resists the proud, but gives grace to the humble.”
7Basi, jiwekeni chini ya Mungu; mpingeni Ibilisi naye atawakimbieni.
7Be subject therefore to God. But resist the devil, and he will flee from you.
8Mkaribieni Mungu, naye atakuja karibu nanyi. Osheni mikono yenu enyi wakosefu! Safisheni mioyo yenu enyi wanafiki!
8Draw near to God, and he will draw near to you. Cleanse your hands, you sinners; and purify your hearts, you double-minded.
9Oneni huzuni, lieni na kuomboleza; kicheko chenu na kiwe kilio; na furaha yenu iwe huzuni kubwa.
9Lament, mourn, and weep. Let your laughter be turned to mourning, and your joy to gloom.
10Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.
10Humble yourselves in the sight of the Lord, and he will exalt you.
11Ndugu, msilaumiane ninyi kwa ninyi. Anayemlaumu ndugu yake na kumhukumu, huyo huilaumu na kuihukumu Sheria. Kama ukiihukumu Sheria, basi, wewe huitii Sheria, bali waihukumu.
11Don’t speak against one another, brothers. He who speaks against a brother and judges his brother, speaks against the law and judges the law. But if you judge the law, you are not a doer of the law, but a judge.
12Mungu peke yake ndiye mwenye kuweka Sheria na kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi, wewe ni nani hata umhukumu binadamu mwenzako?
12Only one is the lawgiver, who is able to save and to destroy. But who are you to judge another?
13Basi, sasa sikilizeni ninyi mnaosema: "Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani na kukaa huko mwaka mzima tukifanya biashara na kupata faida."
13Come now, you who say, “Today or tomorrow let’s go into this city, and spend a year there, trade, and make a profit.”
14Ninyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Ninyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.
14Whereas you don’t know what your life will be like tomorrow. For what is your life? For you are a vapor, that appears for a little time, and then vanishes away.
15Mngalipaswa kusema: "Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile."
15For you ought to say, “If the Lord wills, we will both live, and do this or that.”
16Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.
16But now you glory in your boasting. All such boasting is evil.
17Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.
17To him therefore who knows to do good, and doesn’t do it, to him it is sin.