1Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
1Now a certain man was sick, Lazarus from Bethany, of the village of Mary and her sister, Martha.
2Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
2It was that Mary who had anointed the Lord with ointment, and wiped his feet with her hair, whose brother, Lazarus, was sick.
3Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: "Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!"
3The sisters therefore sent to him, saying, “Lord, behold, he for whom you have great affection is sick.”
4Yesu aliposikia hivyo akasema, "Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe."
4But when Jesus heard it, he said, “This sickness is not to death, but for the glory of God, that God’s Son may be glorified by it.”
5Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
5Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
6Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
6When therefore he heard that he was sick, he stayed two days in the place where he was.
7Kisha akawaambia wanafunzi wake, "Twendeni tena Yudea!"
7Then after this he said to the disciples, “Let’s go into Judea again.”
8Wanafunzi wakamwambia, "Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?"
8The disciples told him, “Rabbi, the Jews were just trying to stone you, and are you going there again?”
9Yesu akajibu, "Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
9Jesus answered, “Aren’t there twelve hours of daylight? If a man walks in the day, he doesn’t stumble, because he sees the light of this world.
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake."
10 But if a man walks in the night, he stumbles, because the light isn’t in him.”
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, "Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha."
11He said these things, and after that, he said to them, “Our friend, Lazarus, has fallen asleep, but I am going so that I may awake him out of sleep.”
12Wanafunzi wake wakamwambia, "Bwana, ikiwa amelala, basi atapona."
12The disciples therefore said, “Lord, if he has fallen asleep, he will recover.”
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
13Now Jesus had spoken of his death, but they thought that he spoke of taking rest in sleep.
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, "Lazaro amekufa;
14So Jesus said to them plainly then, “Lazarus is dead.
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake."
15 I am glad for your sakes that I was not there, so that you may believe. Nevertheless, let’s go to him.”
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, "Twendeni nasi tukafe pamoja naye!"
16Thomas therefore, who is called Didymus, “Didymus” means “Twin” said to his fellow disciples, “Let’s go also, that we may die with him.”
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
17So when Jesus came, he found that he had been in the tomb four days already.
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
18Now Bethany was near Jerusalem, about fifteen stadia 15 stadia is about 2.8 kilometers or 1.7 miles away.
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
19Many of the Jews had joined the women around Martha and Mary, to console them concerning their brother.
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
20Then when Martha heard that Jesus was coming, she went and met him, but Mary stayed in the house.
21Martha akamwambia Yesu, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
21Therefore Martha said to Jesus, “Lord, if you would have been here, my brother wouldn’t have died.
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa."
22Even now I know that, whatever you ask of God, God will give you.”
23Yesu akamwambia, "Kaka yako atafufuka."
23Jesus said to her, “Your brother will rise again.”
24Martha akamjibu, "Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho."
24Martha said to him, “I know that he will rise again in the resurrection at the last day.”
25Yesu akamwambia, "Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
25Jesus said to her, “I am the resurrection and the life. He who believes in me will still live, even if he dies.
26na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?"
26 Whoever lives and believes in me will never die. Do you believe this?”
27Martha akamwambia, "Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni."
27She said to him, “Yes, Lord. I have come to believe that you are the Christ, God’s Son, he who comes into the world.”
28Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, "Mwalimu yuko hapa, anakuita."
28When she had said this, she went away, and called Mary, her sister, secretly, saying, “The Teacher is here, and is calling you.”
29Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
29When she heard this, she arose quickly, and went to him.
30Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
30Now Jesus had not yet come into the village, but was in the place where Martha met him.
31Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
31Then the Jews who were with her in the house, and were consoling her, when they saw Mary, that she rose up quickly and went out, followed her, saying, “She is going to the tomb to weep there.”
32Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!"
32Therefore when Mary came to where Jesus was, and saw him, she fell down at his feet, saying to him, “Lord, if you would have been here, my brother wouldn’t have died.”
33Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
33When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews weeping who came with her, he groaned in the spirit, and was troubled,
34Kisha akawauliza, "Mlimweka wapi?" Wakamwambia, "Bwana, njoo uone."
34and said, “Where have you laid him?” They told him, “Lord, come and see.”
35Yesu akalia machozi.
35Jesus wept.
36Basi, Wayahudi wakasema, "Tazameni jinsi alivyompenda!"
36The Jews therefore said, “See how much affection he had for him!”
37Lakini baadhi yao wakasema, "Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?"
37Some of them said, “Couldn’t this man, who opened the eyes of him who was blind, have also kept this man from dying?”
38Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
38Jesus therefore, again groaning in himself, came to the tomb. Now it was a cave, and a stone lay against it.
39Yesu akasema, "Ondoeni hilo jiwe!" Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, "Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!"
39Jesus said, “Take away the stone.” Martha, the sister of him who was dead, said to him, “Lord, by this time there is a stench, for he has been dead four days.”
40Yesu akamwambia, "Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?"
40Jesus said to her, “Didn’t I tell you that if you believed, you would see God’s glory?”
41Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, "Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
41So they took away the stone from the place where the dead man was lying. NU omits “from the place where the dead man was lying.” Jesus lifted up his eyes, and said, “Father, I thank you that you listened to me.
42Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma."
42 I know that you always listen to me, but because of the multitude that stands around I said this, that they may believe that you sent me.”
43Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: "Lazaro! Toka nje!"
43When he had said this, he cried with a loud voice, “Lazarus, come out!”
44Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, "Mfungueni, mkamwache aende zake."
44He who was dead came out, bound hand and foot with wrappings, and his face was wrapped around with a cloth. Jesus said to them, “Free him, and let him go.”
45Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
45Therefore many of the Jews, who came to Mary and saw what Jesus did, believed in him.
46Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
46But some of them went away to the Pharisees, and told them the things which Jesus had done.
47kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, "Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
47The chief priests therefore and the Pharisees gathered a council, and said, “What are we doing? For this man does many signs.
48Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!"
48If we leave him alone like this, everyone will believe in him, and the Romans will come and take away both our place and our nation.”
49Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, "Ninyi hamjui kitu!
49But a certain one of them, Caiaphas, being high priest that year, said to them, “You know nothing at all,
50Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?"
50nor do you consider that it is advantageous for us that one man should die for the people, and that the whole nation not perish.”
51Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
51Now he didn’t say this of himself, but being high priest that year, he prophesied that Jesus would die for the nation,
52na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
52and not for the nation only, but that he might also gather together into one the children of God who are scattered abroad.
53Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
53So from that day forward they took counsel that they might put him to death.
54Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
54Jesus therefore walked no more openly among the Jews, but departed from there into the country near the wilderness, to a city called Ephraim. He stayed there with his disciples.
55Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
55Now the Passover of the Jews was at hand. Many went up from the country to Jerusalem before the Passover, to purify themselves.
56Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, "Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?"
56Then they sought for Jesus and spoke one with another, as they stood in the temple, “What do you think—that he isn’t coming to the feast at all?”
57Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
57Now the chief priests and the Pharisees had commanded that if anyone knew where he was, he should report it, that they might seize him.