Swahili: New Testament

World English Bible

John

2

1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
1The third day, there was a marriage in Cana of Galilee. Jesus’ mother was there.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
2Jesus also was invited, with his disciples, to the marriage.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
3When the wine ran out, Jesus’ mother said to him, “They have no wine.”
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
4Jesus said to her, “Woman, what does that have to do with you and me? My hour has not yet come.”
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
5His mother said to the servants, “Whatever he says to you, do it.”
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
6Now there were six water pots of stone set there after the Jews’ way of purifying, containing two or three metretes apiece.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
7Jesus said to them, “Fill the water pots with water.” They filled them up to the brim.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
8He said to them, “Now draw some out, and take it to the ruler of the feast.” So they took it.
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
9When the ruler of the feast tasted the water now become wine, and didn’t know where it came from (but the servants who had drawn the water knew), the ruler of the feast called the bridegroom,
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
10and said to him, “Everyone serves the good wine first, and when the guests have drunk freely, then that which is worse. You have kept the good wine until now!”
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
11This beginning of his signs Jesus did in Cana of Galilee, and revealed his glory; and his disciples believed in him.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
12After this, he went down to Capernaum, he, and his mother, his brothers, and his disciples; and they stayed there a few days.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
13The Passover of the Jews was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
14He found in the temple those who sold oxen, sheep, and doves, and the changers of money sitting.
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
15He made a whip of cords, and threw all out of the temple, both the sheep and the oxen; and he poured out the changers’ money, and overthrew their tables.
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
16To those who sold the doves, he said, “Take these things out of here! Don’t make my Father’s house a marketplace!”
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
17His disciples remembered that it was written, “Zeal for your house will eat me up.”
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
18The Jews therefore answered him, “What sign do you show us, seeing that you do these things?”
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
19Jesus answered them, “Destroy this temple, and in three days I will raise it up.”
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
20The Jews therefore said, “It took forty-six years to build this temple! Will you raise it up in three days?”
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
21But he spoke of the temple of his body.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
22When therefore he was raised from the dead, his disciples remembered that he said this, and they believed the Scripture, and the word which Jesus had said.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
23Now when he was in Jerusalem at the Passover, during the feast, many believed in his name, observing his signs which he did.
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
24But Jesus didn’t trust himself to them, because he knew everyone,
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
25and because he didn’t need for anyone to testify concerning man; for he himself knew what was in man.