Syriac: NT

Swahili: New Testament

1 Corinthians

1

1ܦܘܠܘܤ ܩܪܝܐ ܘܫܠܝܚܐ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܒܨܒܝܢܗ ܕܐܠܗܐ ܘܤܘܤܬܢܤ ܐܚܐ ܀
1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2ܠܥܕܬܐ ܕܐܠܗܐ ܕܒܩܘܪܢܬܘܤ ܩܪܝܐ ܘܩܕܝܫܐ ܕܒܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܡܩܕܫܝܢ ܘܠܟܠܗܘܢ ܐܝܠܝܢ ܕܩܪܝܢ ܫܡܗ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܒܟܠ ܐܬܪ ܕܝܠܗܘܢ ܘܕܝܠܢ ܀
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3ܛܝܒܘܬܐ ܥܡܟܘܢ ܘܫܠܡܐ ܡܢ ܐܠܗܐ ܐܒܘܢ ܘܡܢ ܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4ܡܘܕܐ ܐܢܐ ܠܐܠܗܝ ܒܟܠܙܒܢ ܚܠܦܝܟܘܢ ܥܠ ܛܝܒܘܬܐ ܕܐܠܗܐ ܕܐܬܝܗܒܬ ܠܟܘܢ ܒܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5ܕܒܟܠ ܡܕܡ ܥܬܪܬܘܢ ܒܗ ܒܟܠ ܡܠܐ ܘܒܟܠ ܝܕܥܬܐ ܀
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6ܐܝܟ ܕܤܗܕܘܬܗ ܕܡܫܝܚܐ ܐܫܬܪܪܬ ܒܟܘܢ ܀
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7ܕܠܐ ܐܬܒܨܪܬܘܢ ܒܚܕܐ ܡܢ ܡܘܗܒܬܗ ܐܠܐ ܡܤܟܝܢ ܐܢܬܘܢ ܠܓܠܝܢܗ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8ܕܗܘ ܢܫܪܪܟܘܢ ܥܕܡܐ ܠܐܚܪܝܬܐ ܕܕܠܐ ܪܫܝܢ ܬܗܘܘܢ ܒܝܘܡܗ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9ܡܗܝܡܢ ܗܘ ܐܠܗܐ ܕܒܐܝܕܗ ܐܬܩܪܝܬܘܢ ܠܫܘܬܦܘܬܐ ܕܒܪܗ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܡܪܢ ܀
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10ܒܥܐ ܐܢܐ ܕܝܢ ܡܢܟܘܢ ܐܚܝ ܒܫܡܗ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܕܬܗܘܐ ܚܕܐ ܡܠܬܐ ܠܟܠܟܘܢ ܘܠܐ ܢܗܘܝܢ ܒܟܘܢ ܦܠܓܘܬܐ ܐܠܐ ܬܗܘܘܢ ܓܡܝܪܝܢ ܒܚܕܐ ܬܪܥܝܬܐ ܘܒܚܕ ܪܥܝܢܐ ܀
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11ܫܠܚܘ ܠܝ ܓܝܪ ܥܠܝܟܘܢ ܐܚܝ ܡܢ ܒܝܬ ܟܠܐܐ ܕܚܪܝܢܐ ܐܝܬ ܒܝܢܬܟܘܢ ܀
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12ܗܕܐ ܕܝܢ ܐܡܪ ܐܢܐ ܕܐܝܬ ܡܢܟܘܢ ܕܐܡܪ ܐܢܐ ܕܦܘܠܘܤ ܐܢܐ ܘܐܝܬ ܕܐܡܪ ܐܢܐ ܕܐܦܠܘ ܐܢܐ ܘܐܝܬ ܕܐܡܪ ܐܢܐ ܕܟܐܦܐ ܐܢܐ ܘܐܝܬ ܕܐܡܪ ܐܢܐ ܕܡܫܝܚܐ ܐܢܐ ܀
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
13ܕܠܡܐ ܐܬܦܠܓ ܠܗ ܡܫܝܚܐ ܐܘ ܠܡܐ ܦܘܠܘܤ ܐܙܕܩܦ ܥܠ ܐܦܝܟܘܢ ܐܘ ܒܫܡܗ ܕܦܘܠܘܤ ܥܡܕܬܘܢ ܀
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14ܡܘܕܐ ܐܢܐ ܠܐܠܗܝ ܕܠܐܢܫ ܡܢܟܘܢ ܠܐ ܐܥܡܕܬ ܐܠܐ ܠܟܪܝܤܦܘܤ ܘܠܓܐܝܘܤ ܀
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15ܕܠܐ ܐܢܫ ܢܐܡܪ ܕܒܫܡܝ ܐܥܡܕܬ ܀
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16ܐܥܡܕܬ ܕܝܢ ܐܦ ܠܒܝܬܗ ܕܐܤܛܦܢܐ ܬܘܒ ܕܝܢ ܠܐ ܝܕܥ ܐܢܐ ܐܢ ܠܐܢܫ ܐܚܪܝܢ ܐܥܡܕܬ ܀
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17ܠܐ ܓܝܪ ܫܕܪܢܝ ܡܫܝܚܐ ܠܡܥܡܕܘ ܐܠܐ ܠܡܤܒܪܘ ܠܐ ܒܚܟܡܬ ܡܠܐ ܕܠܐ ܢܤܬܪܩ ܙܩܝܦܗ ܕܡܫܝܚܐ ܀
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18ܡܠܬܐ ܓܝܪ ܕܙܩܝܦܐ ܠܐܒܝܕܐ ܫܛܝܘܬܐ ܗܝ ܠܢ ܕܝܢ ܠܐܝܠܝܢ ܕܚܝܝܢܢ ܚܝܠܐ ܗܝ ܕܐܠܗܐ ܀
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19ܟܬܝܒ ܓܝܪ ܕܐܘܒܕ ܚܟܡܬܐ ܕܚܟܝܡܐ ܘܐܓܠܘܙ ܬܪܥܝܬܐ ܕܤܟܘܠܬܢܐ ܀
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
20ܐܝܟܐ ܗܘ ܚܟܝܡܐ ܐܘ ܐܝܟܐ ܗܘ ܤܦܪܐ ܐܘ ܐܝܟܐ ܗܘ ܕܪܘܫܐ ܕܥܠܡܐ ܗܢܐ ܠܐ ܗܐ ܐܫܛܝܗ ܐܠܗܐ ܚܟܡܬܗ ܕܥܠܡܐ ܗܢܐ ܀
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
21ܡܛܠ ܓܝܪ ܕܒܚܟܡܬܗ ܕܐܠܗܐ ܠܐ ܝܕܥ ܥܠܡܐ ܒܚܟܡܬܐ ܠܐܠܗܐ ܨܒܐ ܐܠܗܐ ܕܒܫܛܝܘܬܐ ܕܟܪܘܙܘܬܐ ܢܚܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܡܗܝܡܢܝܢ ܀
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22ܡܛܠ ܕܝܗܘܕܝܐ ܐܬܘܬܐ ܫܐܠܝܢ ܘܐܪܡܝܐ ܚܟܡܬܐ ܒܥܝܢ ܀
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23ܚܢܢ ܕܝܢ ܡܟܪܙܝܢܢ ܡܫܝܚܐ ܟܕ ܙܩܝܦ ܬܘܩܠܬܐ ܠܝܗܘܕܝܐ ܘܠܐܪܡܝܐ ܫܛܝܘܬܐ ܀
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24ܠܗܢܘܢ ܕܝܢ ܕܩܪܝܢ ܝܗܘܕܝܐ ܘܐܪܡܝܐ ܡܫܝܚܐ ܚܝܠܐ ܕܐܠܗܐ ܘܚܟܡܬܐ ܕܐܠܗܐ ܀
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25ܡܛܠ ܕܫܛܝܘܬܗ ܕܐܠܗܐ ܚܟܝܡܐ ܗܝ ܡܢ ܒܢܝܢܫܐ ܘܟܪܝܗܘܬܗ ܕܐܠܗܐ ܚܝܠܬܢܝܐ ܗܝ ܡܢ ܒܢܝ ܐܢܫܐ ܀
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26ܚܙܘ ܓܝܪ ܐܦ ܩܪܝܬܟܘܢ ܐܚܝ ܕܠܐ ܤܓܝܐܝܢ ܒܟܘܢ ܚܟܝܡܐ ܒܒܤܪ ܘܠܐ ܤܓܝܐܝܢ ܒܟܘܢ ܚܝܠܬܢܐ ܘܠܐ ܤܓܝܐܝܢ ܒܟܘܢ ܒܢܝ ܛܘܗܡܐ ܪܒܐ ܀
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27ܐܠܐ ܓܒܐ ܐܠܗܐ ܠܤܟܠܘܗܝ ܕܥܠܡܐ ܕܢܒܗܬ ܠܚܟܝܡܐ ܘܓܒܐ ܟܪܝܗܘܗܝ ܕܥܠܡܐ ܕܢܒܗܬ ܠܚܝܠܬܢܐ ܀
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28ܘܓܒܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܒܨܝܪ ܛܘܗܡܗܘܢ ܒܥܠܡܐ ܘܠܡܤܠܝܐ ܘܠܐܝܠܝܢ ܕܠܝܬ ܐܢܘܢ ܕܢܒܛܠ ܠܐܝܠܝܢ ܕܐܝܬܝܗܘܢ ܀
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29ܕܠܐ ܢܫܬܒܗܪ ܟܠ ܒܤܪ ܩܕܡܘܗܝ ܀
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30ܐܦ ܐܢܬܘܢ ܕܝܢ ܡܢܗ ܐܢܬܘܢ ܒܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܗܘ ܕܗܘܐ ܠܢ ܚܟܡܬܐ ܡܢ ܐܠܗܐ ܘܙܕܝܩܘܬܐ ܘܩܕܝܫܘܬܐ ܘܦܘܪܩܢܐ ܀
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31ܐܝܟ ܕܟܬܝܒ ܕܡܢ ܕܡܫܬܒܗܪ ܒܡܪܝܐ ܢܫܬܒܗܪ ܀
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."