1ܗܪܛܘ ܒܬܪ ܚܘܒܐ ܘܛܢܘ ܒܡܘܗܒܬܐ ܕܪܘܚܐ ܝܬܝܪܐܝܬ ܕܝܢ ܕܬܬܢܒܘܢ ܀
1Jitahidini kuwa na upendo. Vilevile fanyeni bidii ya kupata vipaji vingine vya kiroho, hasa kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu.
2ܡܢ ܕܡܡܠܠ ܓܝܪ ܒܠܫܢܐ ܠܐ ܗܘܐ ܠܒܢܝܢܫܐ ܡܡܠܠ ܐܠܐ ܠܐܠܗܐ ܠܐ ܓܝܪ ܐܢܫ ܫܡܥ ܡܕܡ ܕܡܡܠܠ ܐܠܐ ܒܪܘܚ ܐܪܙܐ ܡܡܠܠ ܀
2Mwenye kunena lugha ngeni hasemi na watu bali anasema na Mungu. Yeye hunena kwa nguvu ya Roho mambo yaliyofichika.
3ܐܝܢܐ ܕܝܢ ܕܡܬܢܒܐ ܠܒܢܝܢܫܐ ܡܡܠܠ ܒܢܝܢܐ ܘܠܘܒܒܐ ܘܒܘܝܐܐ ܀
3Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, husema na watu kwa ajili ya kuwajenga, kuwafariji na kuwatia moyo.
4ܕܡܡܠܠ ܒܠܫܢܐ ܢܦܫܗ ܗܘ ܒܢܐ ܘܕܡܬܢܒܐ ܥܕܬܐ ܒܢܐ ܀
4Mwenye kunena lugha ngeni anajijenga mwenyewe. Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, analijenga kanisa.
5ܨܒܐ ܐܢܐ ܕܝܢ ܕܟܠܟܘܢ ܬܡܠܠܘܢ ܒܠܫܢܐ ܝܬܝܪܐܝܬ ܕܝܢ ܕܬܬܢܒܘܢ ܪܒ ܗܘ ܓܝܪ ܐܝܢܐ ܕܡܬܢܒܐ ܡܢ ܗܘ ܕܡܡܠܠ ܒܠܫܢܐ ܐܢ ܠܐ ܡܦܫܩ ܐܢ ܕܝܢ ܡܦܫܩ ܥܕܬܐ ܒܢܐ ܀
5Basi, ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha ngeni lakini ningependelea hasa muwe na kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, maana mtu mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, ni wa maana zaidi kuliko yule mwenye kusema lugha ngeni, isipokuwa tu kama yupo hapo mtu awezaye kuyafafanua hayo mambo asemayo, ili kanisa lipate kujengwa.
6ܘܗܫܐ ܐܚܝ ܐܢ ܐܬܐ ܠܘܬܟܘܢ ܘܐܡܠܠ ܥܡܟܘܢ ܒܠܫܢܐ ܡܢܐ ܡܘܬܪ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܐܠܐ ܐܢ ܐܡܠܠ ܥܡܟܘܢ ܐܘ ܒܓܠܝܢܐ ܐܘ ܒܝܕܥܬܐ ܐܘ ܒܢܒܝܘܬܐ ܐܘ ܒܝܘܠܦܢܐ ܀
6Hivyo, ndugu zangu, kama nikija kwenu na kusema nanyi kwa lugha ngeni itawafaa nini? Haitawafaa chochote, isipokuwa tu kama nitawaelezeni ufunuo wa Mungu au ujuzi fulani au ujumbe wa Mungu au mafundisho fulani.
7ܐܦ ܨܒܘܬܐ ܓܝܪ ܐܝܠܝܢ ܕܠܝܬ ܒܗܝܢ ܢܦܫܐ ܘܝܗܒܢ ܩܠܐ ܐܢ ܐܒܘܒܐ ܘܐܢ ܩܝܬܪܐ ܐܢ ܦܘܪܫܢܐ ܠܐ ܥܒܕܢ ܒܝܬ ܩܝܢܬܐ ܠܚܒܪܬܗ ܐܝܟܢܐ ܡܬܝܕܥ ܡܕܡ ܕܡܙܕܡܪ ܐܘ ܡܕܡ ܕܡܬܢܩܫ ܀
7Ndivyo ilivyo kwa vyombo visivyo na uhai vyenye kutoa sauti kama vile filimbi au kinanda. Je, mtu anawezaje kuutambua wimbo unaochezwa kama vyombo hivyo havitoi sauti waziwazi vinapopigwa?
8ܘܐܢ ܩܪܢܐ ܬܩܪܐ ܩܠܐ ܕܠܐ ܦܪܝܫ ܡܢܘ ܢܬܛܝܒ ܠܩܪܒܐ ܀
8La mgambo likilia bila kufuata taratibu zake, nani atajiweka tayari kwa vita?
9ܗܟܢܐ ܐܦ ܐܢܬܘܢ ܐܢ ܬܐܡܪܘܢ ܡܠܬܐ ܒܠܫܢܐ ܘܠܐ ܬܗܘܐ ܡܦܫܩܐ ܐܝܟܢܐ ܡܬܝܕܥ ܡܕܡ ܕܐܡܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܗܘܝܬܘܢ ܠܟܘܢ ܐܝܟ ܗܘ ܕܥܡ ܐܐܪ ܡܡܠܠܝܢ ܐܢܬܘܢ ܀
9Hali kadhalika na ninyi, kama ulimi wenu hausemi kitu chenye kueleweka, nani ataweza kufahamu mnayosema? Maneno yenu yatapotea hewani.
10ܗܐ ܓܝܪ ܓܢܤܐ ܕܠܫܢܐ ܤܓܝܐܐ ܐܝܬ ܒܥܠܡܐ ܘܠܝܬ ܚܕ ܡܢܗܘܢ ܕܠܐ ܩܠܐ ܀
10Zipo lugha mbalimbali ulimwenguni, na hakuna hata mojawapo isiyo na maana.
11ܘܐܢ ܠܐ ܝܕܥ ܐܢܐ ܚܝܠܗ ܕܩܠܐ ܗܘܐ ܐܢܐ ܠܝ ܒܪܒܪܝܐ ܠܗܘ ܕܡܡܠܠ ܘܐܦ ܗܘ ܕܡܡܠܠ ܗܘܐ ܠܗ ܠܝ ܒܪܒܪܝܐ ܀
11Lakini ikiwa mimi sifahamu maana ya lugha asemayo mtu fulani, mimi ni mgeni kwake mtu huyo naye pia ni mgeni kwangu.
12ܗܟܢܐ ܐܦ ܐܢܬܘܢ ܡܛܠ ܕܛܢܢܐ ܐܢܬܘܢ ܕܡܘܗܒܬܐ ܕܪܘܚܐ ܠܒܢܝܢܐ ܕܥܕܬܐ ܒܥܘ ܕܬܬܝܬܪܘܢ ܀
12Hali kadhalika na ninyi, maadam mna hamu ya kupata vipaji vya Roho, jitahidini hasa kujipatia vile vinavyosaidia kulijenga kanisa.
13ܘܗܘ ܕܡܡܠܠ ܒܠܫܢܐ ܢܨܠܐ ܕܢܦܫܩ ܀
13Kwa hiyo, mwenye kunena lugha ngeni na aombe apate uwezo wa kuzifafanua.
14ܐܢ ܗܘ ܓܝܪ ܕܗܘܝܬ ܡܨܠܐ ܒܠܫܢܐ ܪܘܚܝ ܗܘ ܡܨܠܝܐ ܡܕܥܝ ܕܝܢ ܕܠܐ ܦܐܪܝܢ ܗܘ ܀
14Maana, nikisali kwa lugha ngeni roho yangu ndiyo inayosali, lakini akili yangu hubaki bure.
15ܡܢܐ ܗܟܝܠ ܐܥܒܕ ܐܨܠܐ ܒܪܘܚܝ ܘܐܨܠܐ ܐܦ ܒܡܕܥܝ ܘܐܙܡܪ ܒܪܘܚܝ ܘܐܙܡܪ ܐܦ ܒܡܕܥܝ ܀
15Nifanye nini, basi? Nitasali kwa roho yangu, nitasali pia kwa akili yangu; nitaimba kwa roho yangu, nitaimba pia kwa akili yangu.
16ܘܐܢ ܠܐ ܐܢ ܡܒܪܟ ܐܢܬ ܒܪܘܚ ܗܘ ܕܡܡܠܐ ܕܘܟܬܗ ܕܗܕܝܘܛܐ ܐܝܟܢܐ ܢܐܡܪ ܐܡܝܢ ܥܠ ܬܘܕܝܬܟ ܕܝܠܟ ܡܛܠ ܕܡܢܐ ܐܡܪ ܐܢܬ ܠܐ ܝܕܥ ܀
16Ukimsifu Mungu kwa roho yako tu, atawezaje mtu wa kawaida aliye katika mkutano kuitikia sala yako ya shukrani kwa kusema: "Amina," kama haelewi unachosema?
17ܐܢܬ ܓܝܪ ܫܦܝܪ ܡܒܪܟ ܐܢܬ ܐܠܐ ܚܒܪܟ ܠܐ ܡܬܒܢܐ ܀
17Sala yako ya shukrani yaweza kweli kuwa bora, lakini huyo mwingine haitamfaidia.
18ܡܘܕܐ ܐܢܐ ܠܐܠܗܐ ܕܝܬܝܪ ܡܢ ܟܠܟܘܢ ܡܡܠܠ ܐܢܐ ܒܠܫܢܐ ܀
18Namshukuru Mungu kwamba mimi nasema kwa lugha ngeni zaidi kuliko ninyi nyote.
19ܐܠܐ ܒܥܕܬܐ ܨܒܐ ܐܢܐ ܕܚܡܫ ܡܠܝܢ ܒܡܕܥܝ ܐܡܠܠ ܕܐܦ ܐܚܪܢܐ ܐܠܦ ܝܬܝܪ ܡܢ ܪܒܘ ܡܠܝܢ ܒܠܫܢܐ ܀
19Lakini katika mikutano ya waumini napendelea zaidi kusema maneno matano yenye kueleweka ili niwafundishe wengine, kuliko kusema maneno elfu ya lugha ngeni.
20ܐܚܝ ܠܐ ܗܘܝܬܘܢ ܛܠܝܢ ܒܪܥܝܢܝܟܘܢ ܐܠܐ ܠܒܝܫܬܐ ܗܘܘ ܝܠܘܕܐ ܘܒܪܥܝܢܝܟܘܢ ܗܘܘ ܓܡܝܪܝܢ ܀
20Ndugu, msiwe kama watoto katika fikira zenu. Kuhusu uovu muwe kama watoto wachanga lakini katika kufikiri ni lazima muwe kama watu waliokomaa.
21ܒܢܡܘܤܐ ܟܬܝܒ ܕܒܡܡܠܠܐ ܢܘܟܪܝܐ ܘܒܠܫܢܐ ܐܚܪܢܐ ܐܡܠܠ ܥܡܗ ܥܡ ܥܡܐ ܗܢܐ ܐܦܠܐ ܗܟܢܐ ܢܫܡܥܘܢܢܝ ܐܡܪ ܡܪܝܐ ܀
21Imeandikwa katika Sheria: "Bwana asema hivi: Kwa njia ya wenye kunena lugha ngeni, na kwa midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, hata hivyo, hawatanisikiliza."
22ܡܕܝܢ ܠܫܢܐ ܠܐܬܐ ܗܘ ܤܝܡܝܢ ܠܐ ܠܡܗܝܡܢܐ ܐܠܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܠܐ ܡܗܝܡܢܝܢ ܢܒܝܘܬܐ ܕܝܢ ܠܐ ܗܘܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܠܐ ܡܗܝܡܢܝܢ ܐܠܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܡܗܝܡܢܝܢ ܀
22Hivyo basi, kipaji cha kusema lugha ngeni ni ishara, si kwa ajili ya watu wenye imani, bali kwa ajili ya wale wasioamini; lakini kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni kwa ajili ya wale wanaoamini na si kwa ajili ya wasioamini.
23ܐܢ ܗܘ ܗܟܝܠ ܕܬܬܟܢܫ ܟܠܗ ܥܕܬܐ ܘܟܠܗܘܢ ܒܠܫܢܐ ܢܡܠܠܘܢ ܘܢܥܠܘܢ ܗܕܝܘܛܐ ܐܘ ܐܝܠܝܢ ܕܠܐ ܡܗܝܡܢܝܢ ܠܐ ܐܡܪܝܢ ܕܗܠܝܢ ܫܢܘ ܠܗܘܢ ܀
23Basi, kanisa lote linapokutana pamoja, na wote wakaanza kusema kwa lugha ngeni, kama wakija watu wa kawaida au wasioamini, je, hawatasema kwamba ninyi mna wazimu?
24ܘܐܢ ܟܠܟܘܢ ܬܗܘܘܢ ܡܬܢܒܝܢ ܘܢܥܘܠ ܠܘܬܟܘܢ ܗܕܝܘܛܐ ܐܘ ܡܢ ܕܠܐ ܡܗܝܡܢ ܡܬܒܨܐ ܡܢ ܟܠܟܘܢ ܘܡܬܟܘܢ ܡܢ ܟܠܟܘܢ ܀
24Lakini, wote wakiwa wanautangaza ujumbe wa Mungu, akija mtu wa kawaida au asiyeamini, yote atakayosikia yatamhakikishia ubaya wake mwenyewe; yote atakayosikia yatamhukumu.
25ܘܟܤܝܬܐ ܕܠܒܗ ܡܬܓܠܝܢ ܘܗܝܕܝܢ ܢܦܠ ܥܠ ܐܦܘܗܝ ܘܢܤܓܘܕ ܠܐܠܗܐ ܘܢܐܡܪ ܫܪܝܪܐܝܬ ܐܠܗܐ ܐܝܬ ܒܟܘܢ ܀
25Siri za moyo wake zitafichuliwa, naye atapiga magoti na kumwabudu Mungu akisema: "Kweli Mungu yupo pamoja nanyi."
26ܐܡܪ ܐܢܐ ܗܟܝܠ ܐܚܝ ܕܐܡܬܝ ܕܡܬܟܢܫܝܢ ܐܢܬܘܢ ܠܐܝܢܐ ܡܢܟܘܢ ܕܐܝܬ ܠܗ ܡܙܡܘܪܐ ܢܐܡܪ ܘܐܝܢܐ ܕܐܝܬ ܠܗ ܝܘܠܦܢܐ ܘܐܝܢܐ ܕܐܝܬ ܠܗ ܓܠܝܢܐ ܘܐܝܢܐ ܕܐܝܬ ܠܗ ܠܫܢܐ ܘܐܝܢܐ ܕܐܝܬ ܠܗ ܦܘܫܩܐ ܟܠܗܝܢ ܠܒܢܝܢܐ ܢܗܘܝܢ ܀
26Ndugu, tuseme nini, basi? Mnapokutana pamoja, mmoja aimbe wimbo, mwingine atoe mafundisho, mwingine awe na ufunuo kutoka kwa Mungu, mwingine atumie kipaji cha kusema kwa lugha ngeni na mwingine afafanue yanayosemwa. Yote yawe kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27ܘܐܢ ܒܠܫܢܐ ܐܢܫ ܢܡܠܠ ܬܪܝܢ ܢܡܠܠܘܢ ܘܟܕ ܤܓܝ ܬܠܬܐ ܘܚܕ ܚܕ ܢܡܠܠܘܢ ܘܚܕ ܢܦܫܩ ܀
27Wakiwepo watu wenye vipaji vya kusema kwa lugha ngeni, waseme wawili au watatu, si zaidi, tena mmojammoja; na aweko mtu wa kufafanua yanayosemwa.
28ܘܐܢ ܠܝܬ ܕܡܦܫܩ ܢܫܬܘܩ ܠܗ ܒܥܕܬܐ ܗܘ ܕܡܡܠܠ ܒܠܫܢܐ ܘܒܝܢܘܗܝ ܠܢܦܫܗ ܘܠܐܠܗܐ ܢܡܠܠ ܀
28Lakini kama hakuna awezaye kufafanua, basi, mwenye kusema lugha ngeni anyamaze mkutanoni, aseme na nafsi yake mwenyewe na Mungu.
29ܢܒܝܐ ܕܝܢ ܬܪܝܢ ܐܘ ܬܠܬܐ ܢܡܠܠܘܢ ܘܫܪܟܐ ܢܦܪܫܘܢ ܀
29Kuhusu wale wenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, waseme wawili au watatu, na wengine wayapime maneno yao.
30ܘܐܢ ܠܐܚܪܢܐ ܢܬܓܠܐ ܟܕ ܝܬܒ ܩܕܡܝܐ ܢܫܬܘܩ ܠܗ ܀
30Ikiwa mmoja anaposema mwingine wa wasikilizaji amepata ufunuo kutoka kwa Mungu, basi, yule anayesema anyamaze.
31ܡܫܟܚܝܢ ܐܢܬܘܢ ܓܝܪ ܟܠܟܘܢ ܕܚܕ ܚܕ ܬܬܢܒܘܢ ܕܟܠܢܫ ܢܐܠܦ ܘܟܠܢܫ ܢܬܒܝܐ ܀
31Maana nyote mwaweza kutangaza ujumbe wa Mungu, mmoja baada ya mwingine, ili nyote mpate kujifunza na kutiwa moyo.
32ܪܘܚܐ ܓܝܪ ܕܢܒܝܐ ܠܢܒܝܐ ܡܫܬܥܒܕܐ ܀
32Kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni lazima kitawaliwe na huyo mwenye hicho kipaji.
33ܡܛܠ ܕܐܠܗܐ ܠܐ ܗܘܐ ܕܫܓܘܫܝܐ ܐܠܐ ܕܫܠܡܐ ܐܝܟ ܕܒܟܠܗܝܢ ܥܕܬܐ ܕܩܕܝܫܐ ܀
33Maana Mungu si Mungu wa fujo, ila wa amani.
34ܢܫܝܟܘܢ ܒܥܕܬܐ ܢܗܘܝܢ ܫܬܝܩܢ ܠܐ ܓܝܪ ܡܦܤ ܠܗܝܢ ܕܢܡܠܠܢ ܐܠܐ ܕܢܫܬܥܒܕܢ ܐܝܟܢܐ ܕܐܦ ܢܡܘܤܐ ܐܡܪ ܀
34Kama ilivyo desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu, wanawake wakae kimya katika mikutano ya waumini. Hawana ruhusa kusema; ila wawe watii kama isemavyo Sheria.
35ܘܐܢ ܡܕܡ ܨܒܝܢ ܕܢܐܠܦܢ ܒܒܬܝܗܝܢ ܢܫܐܠܢ ܠܒܥܠܝܗܝܢ ܒܗܬܬܐ ܗܝ ܓܝܪ ܕܢܫܐ ܒܥܕܬܐ ܢܡܠܠܢ ܀
35Ikiwa wanayo maswali ya kuuliza, wawaulize waume zao nyumbani, maana ni aibu kwa mwanamke kusema katika mikutano ya waumini.
36ܐܘ ܕܠܡܐ ܡܢܟܘܢ ܗܘ ܢܦܩܬ ܡܠܬܗ ܕܐܠܗܐ ܐܘ ܠܘܬܟܘܢ ܗܘ ܒܠܚܘܕ ܡܛܬ ܀
36Je, mnadhani neno la Mungu limetoka kwenu ninyi au kwamba limewajieni ninyi peke yenu?
37ܐܢ ܐܢܫ ܕܝܢ ܡܢܟܘܢ ܤܒܪ ܕܢܒܝܐ ܗܘ ܐܘ ܕܪܘܚܐ ܗܘ ܢܕܥ ܗܠܝܢ ܕܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܕܦܘܩܕܢܐ ܐܢܘܢ ܕܡܪܢ ܀
37Kama mtu yeyote anadhani kwamba yeye ni mjumbe wa Mungu au kwamba anacho kipaji cha Roho, na ajue kwamba haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.
38ܐܢ ܐܢܫ ܕܝܢ ܠܐ ܝܕܥ ܠܐ ܢܕܥ ܀
38Lakini mtu asiyetambua hayo, basi, mtu asimjali mtu huyo.
39ܛܢܘ ܗܟܝܠ ܐܚܝ ܠܡܬܢܒܝܘ ܘܠܡܡܠܠܘ ܒܠܫܢܐ ܠܐ ܬܟܠܘܢ ܀
39Hivyo basi, ndugu zangu, mnapaswa kuwa na hamu ya kutangaza ujumbe wa Mungu; lakini msimkataze mtu kusema kwa lugha ngeni.
40ܟܠܡܕܡ ܕܝܢ ܒܐܤܟܡܐ ܘܒܛܟܤܐ ܢܗܘܐ ܀
40Lakini yote yafanyike kwa heshima na kwa utaratibu.