Syriac: NT

Swahili: New Testament

1 John

2

1ܒܢܝ ܗܠܝܢ ܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܕܠܐ ܬܚܛܘܢ ܘܐܢ ܐܢܫ ܢܚܛܐ ܐܝܬ ܠܢ ܦܪܩܠܛܐ ܠܘܬ ܐܒܐ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܙܕܝܩܐ ܀
1Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini, ikijatokea mtu akatenda dhambi, tunaye mmoja ambaye hutuombea kwa Baba, ndiye Yesu Kristo aliye mwadilifu kabisa.
2ܗܘܝܘ ܓܝܪ ܚܘܤܝܐ ܕܥܠ ܐܦܝ ܚܛܗܝܢ ܘܠܘ ܚܠܦܝܢ ܕܝܠܢ ܒܠܚܘܕ ܐܠܐ ܐܦ ܚܠܦ ܟܠܗ ܥܠܡܐ ܀
2Kristo ndiye sadaka iondoayo dhambi zetu; wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.
3ܘܒܗܕܐ ܡܪܓܫܝܢܢ ܕܝܕܥܢܝܗܝ ܐܢ ܢܛܪܝܢܢ ܦܘܩܕܢܘܗܝ ܀
3Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.
4ܗܘ ܓܝܪ ܕܐܡܪ ܕܝܕܥܬܗ ܘܦܘܩܕܢܘܗܝ ܠܐ ܢܛܪ ܕܓܠܐ ܗܘ ܘܫܪܪܐ ܠܝܬ ܒܗ ܀
4Mtu akisema kwamba anamjua, lakini hazitii amri zake, basi mtu huyo ni mwongo, na ukweli haumo ndani yake.
5ܗܘ ܕܝܢ ܕܢܛܪ ܡܠܬܗ ܒܗܢܐ ܡܫܠܡ ܫܪܝܪܐܝܬ ܚܘܒܗ ܕܐܠܗܐ ܒܗܕܐ ܓܝܪ ܝܕܥܝܢܢ ܕܒܗ ܚܢܢ ܀
5Lakini mtu yeyote anayeshika neno la Mungu, huyo ndiye aliye na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hivi ndivyo tunavyoweza kuwa na hakika kwamba tunaungana naye:
6ܗܘ ܕܐܡܪ ܕܒܗ ܐܝܬܝ ܘܠܐ ܠܗ ܕܐܝܟ ܗܠܟܬܗ ܕܝܠܗ ܢܗܠܟ ܀
6mtu yeyote anayesema kwamba ameungana na Mungu, anapaswa kuishi kama alivyoishi Yesu Kristo.
7ܚܒܝܒܝ ܠܘ ܦܘܩܕܢܐ ܚܕܬܐ ܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܐܠܐ ܦܘܩܕܢܐ ܥܬܝܩܐ ܗܘ ܕܐܝܬ ܗܘܐ ܠܟܘܢ ܡܢ ܒܪܫܝܬ ܦܘܩܕܢܐ ܕܝܢ ܥܬܝܩܐ ܐܝܬܘܗܝ ܡܠܬܐ ܗܝ ܕܫܡܥܬܘܢ ܀
7Wapenzi wangu, amri hii ninayowaandikieni si amri mpya; ni amri ileile ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Amri hiyo ya zamani ni ule ujumbe mliousikia.
8ܬܘܒ ܦܘܩܕܢܐ ܚܕܬܐ ܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܗܘ ܕܐܝܬܘܗܝ ܫܪܝܪܐ ܒܗ ܘܒܟܘܢ ܕܚܫܘܟܐ ܥܒܪ ܠܗ ܘܢܘܗܪܐ ܫܪܝܪܐ ܫܪܝ ܡܬܚܙܐ ܀
8Hata hivyo, amri hii ninayowaandikieni ni amri mpya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu pia. Maana giza linatoweka, na mwanga wa ukweli umekwisha anza kuangaza.
9ܡܢ ܕܐܡܪ ܗܟܝܠ ܕܐܝܬܘܗܝ ܒܢܘܗܪܐ ܘܤܢܐ ܠܐܚܘܗܝ ܒܚܫܘܟܐ ܐܝܬܘܗܝ ܥܕܡܐ ܠܗܫܐ ܀
9Yeyote asemaye kwamba yumo katika mwanga, lakini anamchukia ndugu yake, mtu huyo bado yumo gizani.
10ܗܘ ܕܝܢ ܕܡܚܒ ܠܐܚܘܗܝ ܒܢܘܗܪܐ ܡܟܬܪ ܘܟܫܠܐ ܠܝܬ ܒܗ ܀
10Yeyote ampendaye ndugu yake, yuko katika mwanga, na hamna chochote ndani yake kiwezacho kumkwaza mtu mwingine.
11ܗܘ ܕܝܢ ܕܤܢܐ ܠܐܚܘܗܝ ܒܚܫܘܟܐ ܐܝܬܘܗܝ ܘܒܚܫܘܟܐ ܡܗܠܟ ܘܠܐ ܝܕܥ ܠܐܝܟܐ ܐܙܠ ܡܛܠ ܕܚܫܘܟܐ ܤܡܝ ܐܢܝܢ ܥܝܢܘܗܝ ܀
11Lakini anayemchukia ndugu yake, yumo gizani; anatembea gizani, na hajui anakokwenda, maana giza limempofusha.
12ܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܒܢܝܐ ܕܐܫܬܒܩܘ ܠܟܘܢ ܚܛܗܝܟܘܢ ܡܛܠ ܫܡܗ ܀
12Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa kuwa dhambi zenu zimeondolewa kwa jina la Kristo.
13ܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܐܒܗܐ ܕܝܕܥܬܘܢܝܗܝ ܠܗܘ ܕܐܝܬܘܗܝ ܗܘܐ ܡܢ ܒܪܫܝܬ ܟܬܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܥܠܝܡܐ ܕܙܟܝܬܘܢܝܗܝ ܠܒܝܫܐ ܟܬܒܬ ܠܟܘܢ ܛܠܝܐ ܕܝܕܥܬܘܢ ܠܐܒܐ ܀
13Nawaandikieni ninyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo, Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.
14ܟܬܒܬ ܠܟܘܢ ܐܒܗܐ ܕܝܕܥܬܘܢ ܠܗܘ ܕܡܢ ܒܪܫܝܬ ܟܬܒܬ ܠܟܘܢ ܥܠܝܡܐ ܕܚܝܠܬܢܐ ܐܢܬܘܢ ܘܡܠܬܗ ܕܐܠܗܐ ܫܪܝܐ ܒܟܘܢ ܘܙܟܝܬܘܢܝܗܝ ܠܒܝܫܐ ܀
14Nawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mnamjua Baba. Nawaandikieni ninyi kina baba, kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo. Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu; neno la Mungu limo ndani yenu na mmemshinda yule Mwovu.
15ܠܐ ܬܪܚܡܘܢ ܠܥܠܡܐ ܘܠܐ ܠܡܕܡ ܕܐܝܬ ܒܗ ܡܢ ܓܝܪ ܕܪܚܡ ܠܥܠܡܐ ܚܘܒܗ ܕܐܒܐ ܠܝܬ ܒܗ ܀
15Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
16ܟܠ ܡܕܡ ܓܝܪ ܕܐܝܬ ܒܗ ܒܥܠܡܐ ܪܓܬܐ ܗܘ ܕܦܓܪܐ ܘܪܓܬܐ ܕܥܝܢܐ ܘܫܘܒܗܪܐ ܕܥܠܡܐ ܗܠܝܢ ܕܠܐ ܗܘܝ ܡܢ ܐܒܐ ܐܠܐ ܡܢܗ ܐܢܝܢ ܡܢ ܥܠܡܐ ܀
16Vitu vyote vya ulimwengu-tamaa mbaya za mwili, vitu wanavyoviona watu na kuvitamani, majivuno yasababishwayo na mali-vyote hivyo havitoki kwa Baba, bali vyatoka kwa ulimwengu.
17ܘܥܒܪ ܥܠܡܐ ܗܘ ܘܪܓܬܗ ܗܘ ܕܝܢ ܕܥܒܕ ܨܒܝܢܗ ܕܐܠܗܐ ܡܩܘܐ ܠܥܠܡ ܀
17Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele.
18ܒܢܝ ܙܒܢܐ ܗܘ ܐܚܪܝܐ ܘܐܝܟ ܡܕܡ ܕܫܡܥܬܘܢ ܕܐܬܐ ܡܫܝܚܐ ܕܓܠܐ ܘܗܫܐ ܗܘܘ ܠܗܘܢ ܤܓܝܐܐ ܡܫܝܚܐ ܕܓܠܐ ܘܡܢ ܗܕܐ ܝܕܥܝܢܢ ܕܙܒܢܐ ܗܘ ܐܚܪܝܐ ܀
18Watoto, mwisho u karibu! Mlikwisha sikia kwamba adui wa Kristo anakuja, na sasa adui wengi wa Kristo wamekwisha fika, na hivyo twajua kwamba mwisho u karibu.
19ܡܢܢ ܢܦܩܘ ܐܠܐ ܠܘ ܡܢܢ ܗܘܘ ܐܠܘ ܓܝܪ ܡܢܢ ܗܘܘ ܠܘܬܢ ܡܟܬܪܝܢ ܗܘܘ ܐܠܐ ܢܦܩܘ ܡܢܢ ܕܬܬܝܕܥ ܕܠܘ ܡܢܢ ܗܘܘ ܀
19Watu hao wametokea kati yetu lakini hawakuwa kweli wa kwetu na ndiyo maana walituacha; Kama wangalikuwa wa kwetu, wangalibaki nasi. Lakini waliondoka, wakaenda zao, kusudi ionekane wazi kwamba hawakuwa kamwe wa kwetu.
20ܘܐܢܬܘܢ ܡܫܝܚܘܬܐ ܐܝܬ ܠܟܘܢ ܡܢ ܩܕܝܫܐ ܘܦܪܫܝܢ ܐܢܬܘܢ ܗܘ ܠܟܠ ܐܢܫ ܀
20Ninyi, lakini, mlipata kumiminiwa Roho Mtakatifu na Kristo, na hivyo mnaujua ukweli.
21ܠܐ ܟܬܒܬ ܠܟܘܢ ܕܠܐ ܝܕܥܝܢ ܐܢܬܘܢ ܠܗ ܠܫܪܪܐ ܐܠܐ ܕܝܕܥܝܢ ܐܢܬܘܢ ܠܗ ܘܕܟܠܗ ܕܓܠܘܬܐ ܠܐ ܗܘܬ ܡܢܗ ܡܢ ܫܪܪܐ ܀
21Basi, nawaandikieni, si kwa kuwa hamuujui ukweli, bali kwa sababu mnaujua; na pia mnajua kwamba uongo wowote haupatikani katika ukweli.
22ܡܢܘ ܕܓܠܐ ܐܠܐ ܐܢ ܐܝܢܐ ܕܟܦܪ ܕܝܫܘܥ ܠܐ ܗܘܐ ܡܫܝܚܐ ܗܢܐ ܗܘ ܡܫܝܚܐ ܕܓܠܐ ܗܘ ܕܟܦܪ ܒܐܒܐ ܟܦܪ ܐܦ ܒܒܪܐ ܀
22Mwongo ni nani? Ni yule anayekana kwamba Yesu ni Masiha. Mtu wa namna hiyo ni adui wa Kristo--anamkana Baba na Mwana.
23ܘܗܘ ܕܟܦܪ ܒܒܪܐ ܐܦܠܐ ܒܐܒܐ ܡܗܝܡܢ ܡܢ ܕܡܘܕܐ ܒܒܪܐ ܐܦ ܒܐܒܐ ܡܘܕܐ ܀
23Maana yeyote anayemkana Mwana, anamkana pia Baba; na yeyote anayemkubali Mwana, anampata Baba pia.
24ܘܐܢܬܘܢ ܡܕܡ ܕܫܡܥܬܘܢ ܡܢ ܩܕܝܡ ܢܩܘܐ ܠܘܬܟܘܢ ܐܢ ܓܝܪ ܡܩܘܐ ܠܘܬܟܘܢ ܡܕܡ ܕܫܡܥܬܘܢ ܡܢ ܩܕܝܡ ܐܦ ܐܢܬܘܢ ܡܩܘܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܐܒܐ ܘܒܒܪܐ ܀
24Basi, ujumbe ule mliousikia tangu mwanzo na ukae mioyoni mwenu. Kama ujumbe huo mliousikia tangu mwanzo ukikaa ndani yenu, basi, mtaishi daima katika umoja na Mwana na Baba.
25ܘܗܢܘ ܫܘܘܕܝܐ ܕܐܫܬܘܕܝ ܠܢ ܚܝܐ ܕܠܥܠܡ ܀
25Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: uzima wa milele.
26ܗܠܝܢ ܕܝܢ ܟܬܒܬ ܠܟܘܢ ܡܛܠ ܐܝܠܝܢ ܕܡܛܥܝܢ ܠܟܘܢ ܀
26Nimewaandikieni mambo haya kuhusu wale wanaotaka kuwapotosha ninyi.
27ܘܐܦ ܐܢܬܘܢ ܐܢ ܬܩܘܐ ܠܘܬܟܘܢ ܡܫܝܚܘܬܐ ܕܩܒܠܬܘܢ ܡܢܗ ܠܐ ܤܢܝܩܝܢ ܐܢܬܘܢ ܕܐܢܫ ܢܠܦܟܘܢ ܐܠܐ ܐܝܟ ܡܫܝܚܘܬܐ ܕܐܝܬܝܗ ܡܢ ܐܠܗܐ ܗܝ ܡܠܦܐ ܠܟܘܢ ܥܠ ܟܠܡܕܡ ܘܫܪܝܪܐ ܗܝ ܘܠܝܬ ܒܗ ܕܓܠܘܬܐ ܘܐܝܟ ܕܐܠܦܟܘܢ ܩܘܘ ܒܗ ܀
27Lakini, kwa upande wenu ninyi, Kristo aliwamiminieni Roho wake. Na kama akiendelea kukaa ndani yenu, hamhitaji kufundishwa na mtu yeyote. Maana Roho wake anawafundisheni kila kitu na mafundisho yake ni ya kweli, si ya uongo. Basi shikeni mafundisho ya huyo Roho na kubaki katika muungano na Kristo.
28ܘܗܫܐ ܒܢܝ ܩܘܘ ܒܗ ܕܡܐ ܕܡܬܓܠܐ ܠܐ ܢܒܗܬ ܡܢܗ ܐܠܐ ܬܗܘܐ ܠܢ ܓܠܝܘܬ ܐܦܐ ܒܡܐܬܝܬܗ ܀
28Naam, watoto, kaeni ndani yake kusudi wakati atakapotokea tuwe hodari bila kuwa na sababu ya kujificha kwa aibu Siku ya kuja kwake.
29ܐܢ ܝܕܥܬܘܢ ܕܙܕܝܩ ܗܘ ܕܥܘ ܕܐܦ ܟܠ ܕܥܒܕ ܙܕܝܩܘܬܐ ܡܢܗ ܐܝܬܘܗܝ ܀
29Mnajua kwamba Kristo ni mwadilifu kabisa; basi, mnapaswa kujua pia kwamba kila mtu atendaye mambo adili ni mtoto wa Mungu.