Syriac: NT

Swahili: New Testament

Colossians

4

1ܡܪܝܐ ܥܒܕܘ ܫܘܝܘܬܐ ܘܟܐܢܘܬܐ ܠܘܬ ܥܒܕܝܟܘܢ ܘܗܘܝܬܘܢ ܝܕܥܝܢ ܕܐܦ ܠܟܘܢ ܐܝܬ ܗܘ ܡܪܐ ܒܫܡܝܐ ܀
1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2ܒܨܠܘܬܐ ܐܬܐܡܢܘ ܘܗܘܝܬܘܢ ܥܝܪܝܢ ܐܢܬܘܢ ܒܗ ܘܡܘܕܝܢ ܀
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3ܘܡܨܠܝܢ ܐܦ ܥܠܝܢ ܕܐܠܗܐ ܢܦܬܚ ܠܢ ܬܪܥܐ ܕܡܠܬܐ ܠܡܡܠܠܘ ܐܪܙܐ ܕܡܫܝܚܐ ܕܡܛܠܬܗ ܐܤܝܪ ܐܢܐ ܀
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4ܕܐܓܠܝܘܗܝ ܘܐܡܠܠܝܘܗܝ ܐܝܟܢܐ ܕܘܠܐ ܠܝ ܀
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5ܒܚܟܡܬܐ ܗܠܟܘ ܠܘܬ ܒܪܝܐ ܘܙܒܢܘ ܩܐܪܤܟܘܢ ܀
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6ܘܡܠܬܟܘܢ ܒܟܠܙܒܢ ܒܛܝܒܘܬܐ ܐܝܟ ܕܒܡܠܚܐ ܬܗܘܐ ܡܡܕܟܐ ܘܗܘܝܬܘܢ ܝܕܥܝܢ ܠܐܢܫ ܐܢܫ ܐܝܟܢܐ ܘܠܐ ܠܟܘܢ ܠܡܬܒܘ ܦܬܓܡܐ ܀
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7ܡܕܡ ܕܠܘܬܝ ܕܝܢ ܢܘܕܥܟܘܢ ܛܘܟܝܩܘܤ ܐܚܐ ܚܒܝܒܐ ܘܡܫܡܫܢܐ ܡܗܝܡܢܐ ܘܟܢܬܢ ܒܡܪܝܐ ܀
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8ܗܢܐ ܕܫܕܪܬ ܠܘܬܟܘܢ ܥܠܝܗ ܥܠ ܗܕܐ ܕܢܕܥ ܡܐ ܕܠܘܬܟܘܢ ܘܢܒܝܐ ܠܒܘܬܟܘܢ ܀
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9ܥܡ ܐܢܤܝܡܘܤ ܐܚܐ ܡܗܝܡܢܐ ܘܚܒܝܒܐ ܗܘ ܕܐܝܬܘܗܝ ܡܢܟܘܢ ܗܢܘܢ ܢܘܕܥܘܢܟܘܢ ܡܕܡ ܕܠܘܬܢ ܀
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10ܫܐܠ ܒܫܠܡܟܘܢ ܐܪܤܛܪܟܘܤ ܫܒܝܐ ܕܥܡܝ ܘܡܪܩܘܤ ܒܪ ܕܕܗ ܕܒܪܢܒܐ ܗܘ ܕܐܬܦܩܕܬܘܢ ܥܠܘܗܝ ܕܐܢ ܐܬܐ ܠܘܬܟܘܢ ܬܩܒܠܘܢܝܗܝ ܀
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11ܘܝܫܘܥ ܗܘ ܕܡܬܩܪܐ ܝܘܤܛܘܤ ܗܠܝܢ ܕܐܝܬܝܗܘܢ ܡܢ ܓܙܘܪܬܐ ܘܗܢܘܢ ܒܠܚܘܕ ܥܕܪܘܢܝ ܒܡܠܟܘܬܗ ܕܐܠܗܐ ܘܗܢܘܢ ܗܘܘ ܠܝ ܒܘܝܐܐ ܀
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12ܫܐܠ ܒܫܠܡܟܘܢ ܐܦܦܪܐ ܗܘ ܕܡܢܟܘܢ ܥܒܕܐ ܕܡܫܝܚܐ ܟܕ ܒܟܠܙܒܢ ܥܡܠ ܚܠܦܝܟܘܢ ܒܨܠܘܬܐ ܕܬܩܘܡܘܢ ܓܡܝܪܐ ܘܡܫܡܠܝܐ ܒܟܠܗ ܨܒܝܢܗ ܕܐܠܗܐ ܀
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13ܤܗܕ ܐܢܐ ܓܝܪ ܥܠܘܗܝ ܕܛܢܢܐ ܤܓܝܐܐ ܐܝܬ ܠܗ ܚܠܦܝܟܘܢ ܘܚܠܦ ܗܢܘܢ ܕܒܠܕܝܩܝܐ ܘܕܒܐܝܪܦܘܠܝܤ ܀
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14ܫܐܠ ܒܫܠܡܟܘܢ ܠܘܩܐ ܐܤܝܐ ܚܒܝܒܢ ܘܕܡܐ ܀
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15ܫܐܠܘ ܒܫܠܡܐ ܕܐܚܐ ܕܒܠܕܝܩܝܐ ܘܕܢܘܡܦܐ ܘܕܥܕܬܐ ܕܒܒܝܬܗ ܀
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16ܘܡܐ ܕܐܬܩܪܝܬ ܐܓܪܬܐ ܗܕܐ ܠܘܬܟܘܢ ܥܒܕܘ ܕܐܦ ܒܥܕܬܐ ܕܠܕܝܩܝܐ ܬܬܩܪܐ ܘܗܝ ܕܐܬܟܬܒܬ ܡܢ ܠܕܝܩܝܐ ܩܪܐܘܗ ܐܢܬܘܢ ܀
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17ܘܐܡܪܘ ܠܐܪܟܝܦܘܤ ܕܐܙܕܗܪ ܒܬܫܡܫܬܐ ܗܝ ܕܩܒܠܬ ܒܡܪܢ ܕܬܗܘܐ ܡܫܡܠܐ ܠܗ ܀
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18ܫܠܡܐ ܗܢܐ ܒܐܝܕܐ ܕܝܠܝ ܕܦܘܠܘܤ ܗܘܝܬܘܢ ܥܗܕܝܢ ܠܐܤܘܪܝ ܛܝܒܘܬܐ ܥܡܟܘܢ ܐܡܝܢ ܀
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.