Syriac: NT

Swahili: New Testament

Philemon

1

1ܦܘܠܘܤ ܐܤܝܪܗ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܘܛܝܡܬܐܘܤ ܐܚܐ ܠܦܝܠܡܘܢ ܚܒܝܒܐ ܘܦܠܚܐ ܕܥܡܢ ܀
1Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2ܘܠܐܦܝܐ ܚܒܝܒܬܢ ܘܠܐܪܟܝܦܘܤ ܦܠܚܐ ܕܥܡܢ ܘܠܥܕܬܐ ܕܒܒܝܬܟ ܀
2na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3ܛܝܒܘܬܐ ܥܡܟܘܢ ܘܫܠܡܐ ܡܢ ܐܠܗܐ ܐܒܘܢ ܘܡܢ ܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4ܡܘܕܐ ܐܢܐ ܠܐܠܗܝ ܒܟܠܙܒܢ ܘܡܬܕܟܪ ܐܢܐ ܠܟ ܒܨܠܘܬܝ ܀
4Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5ܗܐ ܡܢ ܕܫܡܥܬ ܗܝܡܢܘܬܟ ܘܚܘܒܐ ܕܐܝܬ ܠܟ ܠܘܬ ܡܪܢ ܝܫܘܥ ܘܠܘܬ ܟܠܗܘܢ ܩܕܝܫܐ ܀
5maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6ܕܬܗܘܐ ܫܘܬܦܘܬܐ ܕܗܝܡܢܘܬܟ ܝܗܒܐ ܦܐܪܐ ܒܥܒܕܐ ܘܒܝܕܥܬܐ ܕܟܠ ܛܒܢ ܕܐܝܬ ܠܟܘܢ ܒܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
6Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7ܚܕܘܬܐ ܓܝܪ ܤܓܝܐܬܐ ܐܝܬ ܠܢ ܘܒܘܝܐܐ ܕܒܝܕ ܚܘܒܟ ܐܬܬܢܝܚܘ ܪܚܡܐ ܕܩܕܝܫܐ ܀
7Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8ܡܛܠ ܗܕܐ ܦܪܗܤܝܐ ܤܓܝܐܬܐ ܐܝܬ ܠܝ ܒܡܫܝܚܐ ܕܐܦܩܘܕ ܠܟ ܐܝܠܝܢ ܕܙܕܩܢ ܀
8Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9ܡܛܠ ܚܘܒܐ ܕܝܢ ܡܒܥܐ ܗܘ ܒܥܐ ܐܢܐ ܡܢܟ ܐܢܐ ܦܘܠܘܤ ܕܐܝܬܝ ܤܒܐ ܐܝܟ ܕܝܕܥ ܐܢܬ ܗܫܐ ܕܝܢ ܐܦ ܐܤܝܪܐ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
9Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10ܘܒܥܐ ܐܢܐ ܡܢܟ ܥܠ ܒܪܝ ܐܝܢܐ ܕܝܠܕܬ ܒܐܤܘܪܝ ܐܢܤܝܡܘܤ ܀
10Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11ܗܘ ܕܒܙܒܢ ܠܝܬ ܗܘܐ ܠܟ ܒܗ ܚܫܚܘ ܗܫܐ ܕܝܢ ܐܦ ܠܟ ܐܦ ܠܝ ܛܒ ܚܫܚ ܀
11Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12ܘܫܕܪܬܗ ܠܟ ܐܢܬ ܕܝܢ ܐܝܟ ܕܠܝܠܕܐ ܕܝܠܝ ܗܟܢܐ ܩܒܠܝܗܝ ܀
12Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13ܨܒܐ ܗܘܝܬ ܓܝܪ ܕܠܘܬܝ ܐܚܕܝܘܗܝ ܕܢܗܘܐ ܡܫܡܫ ܠܝ ܚܠܦܝܟ ܒܐܤܘܪܐ ܕܐܘܢܓܠܝܘܢ ܀
13Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14ܒܠܥܕ ܡܠܟܟ ܕܝܢ ܠܐ ܨܒܝܬ ܡܕܡ ܠܡܥܒܕ ܕܠܐ ܐܝܟ ܕܒܩܛܝܪܐ ܬܗܘܐ ܛܒܬܟ ܐܠܐ ܒܨܒܝܢܟ ܀
14Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15ܟܒܪ ܕܝܢ ܐܦ ܡܛܠ ܗܕܐ ܫܢܝ ܕܫܥܬܐ ܕܠܥܠܡ ܬܐܚܕܝܘܗܝ ܀
15Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima.
16ܠܐ ܡܟܝܠ ܐܝܟ ܥܒܕܐ ܐܠܐ ܝܬܝܪ ܡܢ ܥܒܕܐ ܐܚܐ ܚܒܝܒܐ ܕܝܠܝ ܚܕ ܟܡܐ ܕܝܠܟ ܘܒܒܤܪ ܘܒܡܪܢ ܀
16Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17ܐܢ ܗܟܝܠ ܐܝܬܝܟ ܠܝ ܫܘܬܦܐ ܩܒܠܝܗܝ ܐܝܟ ܕܠܝ ܀
17Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18ܘܐܢ ܡܕܡ ܚܤܪܟ ܐܘ ܚܝܒ ܗܕܐ ܥܠܝ ܚܫܘܒ ܀
18Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19ܐܢܐ ܦܘܠܘܤ ܟܬܒܬ ܒܐܝܕܝ ܐܢܐ ܦܪܥ ܐܢܐ ܕܠܐ ܐܡܪ ܠܟ ܕܐܦ ܢܦܫܟ ܚܝܒ ܐܢܬ ܠܝ ܀
19Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20ܐܝܢ ܐܚܝ ܐܢܐ ܐܬܬܢܝܚ ܒܟ ܒܡܪܢ ܐܢܝܚ ܪܚܡܝ ܒܡܫܝܚܐ ܀
20Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21ܡܛܠ ܕܬܟܝܠ ܐܢܐ ܕܫܡܥ ܐܢܬ ܠܝ ܟܬܒܬ ܠܟ ܘܝܕܥ ܐܢܐ ܕܝܬܝܪ ܡܢ ܡܐ ܕܐܡܪ ܐܢܐ ܥܒܕ ܐܢܬ ܀
21Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22ܒܚܕܐ ܕܝܢ ܐܦ ܛܝܒ ܠܝ ܒܝܬ ܡܫܪܝܐ ܡܤܒܪ ܐܢܐ ܓܝܪ ܕܒܨܠܘܬܟܘܢ ܡܬܝܗܒ ܐܢܐ ܠܟܘܢ ܀
22Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23ܫܐܠ ܒܫܠܡܟ ܐܦܦܪܐ ܫܒܝܐ ܕܥܡܝ ܒܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܀
23Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24ܘܡܪܩܘܤ ܘܐܪܤܛܪܟܘܤ ܘܕܡܐ ܘܠܘܩܐ ܡܥܕܪܢܝ ܀
24Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25ܛܝܒܘܬܗ ܕܡܪܢ ܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܥܡ ܪܘܚܟܘܢ ܐܡܝܢ ܀
25Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.