Syriac: NT

Swahili: New Testament

Romans

14

1ܠܐܝܢܐ ܕܝܢ ܕܟܪܝܗ ܒܗܝܡܢܘܬܐ ܗܒܘ ܠܗ ܐܝܕܐ ܘܠܐ ܬܗܘܘܢ ܡܬܦܠܓܝܢ ܒܡܚܫܒܬܟܘܢ ܀
1Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
2ܐܝܬ ܓܝܪ ܕܡܗܝܡܢ ܕܟܠܡܕܡ ܢܐܟܘܠ ܘܕܟܪܝܗ ܝܪܩܐ ܗܘ ܐܟܠ ܀
2Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
3ܗܘ ܕܝܢ ܕܐܟܠ ܠܗܘ ܡܢ ܕܠܐ ܐܟܠ ܠܐ ܢܫܘܛ ܘܗܘ ܡܢ ܕܠܐ ܐܟܠ ܠܗܘ ܡܢ ܕܐܟܠ ܠܐ ܢܕܘܢ ܐܠܗܐ ܓܝܪ ܩܪܒܗ ܀
3Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
4ܐܢܬ ܡܢ ܐܢܬ ܕܕܐܢ ܐܢܬ ܠܥܒܕܐ ܕܠܐ ܕܝܠܟ ܕܐܢ ܩܐܡ ܠܡܪܗ ܩܐܡ ܘܐܢ ܢܦܠ ܠܡܪܗ ܢܦܠ ܡܩܡ ܗܘ ܕܝܢ ܩܐܡ ܡܛܐ ܓܝܪ ܒܐܝܕܝ ܡܪܗ ܕܢܩܝܡܝܘܗܝ ܀
4Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
5ܐܝܬ ܕܕܐܢ ܝܘܡܐ ܡܢ ܝܘܡܐ ܘܐܝܬ ܕܕܐܢ ܟܠܗܘܢ ܝܘܡܬܐ ܟܠܢܫ ܕܝܢ ܒܡܕܥܐ ܕܢܦܫܗ ܢܫܬܪܪ ܀
5Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
6ܡܢ ܕܡܬܪܥܐ ܕܝܘܡܐ ܠܡܪܗ ܡܬܪܥܐ ܘܟܠ ܕܠܐ ܡܬܪܥܐ ܕܝܘܡܐ ܠܡܪܗ ܠܐ ܡܬܪܥܐ ܘܕܐܟܠ ܠܡܪܗ ܐܟܠ ܘܠܐܠܗܐ ܡܘܕܐ ܘܕܠܐ ܐܟܠ ܠܡܪܗ ܠܐ ܐܟܠ ܘܡܘܕܐ ܠܐܠܗܐ ܀
6Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
7ܠܝܬ ܓܝܪ ܐܢܫ ܡܢܢ ܕܠܢܦܫܗ ܚܝ ܘܠܝܬ ܐܢܫ ܕܠܢܦܫܗ ܡܐܬ ܀
7Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
8ܡܛܠ ܕܐܢ ܚܐܝܢܢ ܠܡܪܢ ܚܐܝܢܢ ܘܐܢ ܡܝܬܝܢܢ ܠܡܪܢ ܗܘ ܡܝܬܝܢܢ ܘܐܢ ܚܝܝܢܢ ܗܟܝܠ ܘܐܢ ܡܝܬܝܢܢ ܕܡܪܢ ܚܢܢ ܀
8maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
9ܡܛܠ ܗܢܐ ܐܦ ܡܫܝܚܐ ܡܝܬ ܘܚܝܐ ܘܩܡ ܕܗܘ ܢܗܘܐ ܡܪܝܐ ܠܡܝܬܐ ܘܠܚܝܐ ܀
9Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
10ܐܢܬ ܕܝܢ ܡܢܐ ܕܐܢ ܐܢܬ ܠܐܚܘܟ ܐܘ ܐܦ ܐܢܬ ܠܡܢܐ ܫܐܛ ܐܢܬ ܠܐܚܘܟ ܟܠܢ ܓܝܪ ܥܬܝܕܝܢܢ ܠܡܩܡ ܩܕܡ ܒܝܡ ܕܡܫܝܚܐ ܀
10Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
11ܐܝܟ ܕܟܬܝܒ ܕܚܝ ܐܢܐ ܐܡܪ ܡܪܝܐ ܕܠܝ ܬܟܘܦ ܟܠ ܒܪܘܟ ܘܠܝ ܢܘܕܐ ܟܠ ܠܫܢ ܀
11Maana Maandiko yanasema: "Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu."
12ܡܕܝܢ ܟܠ ܐܢܫ ܡܢܢ ܦܬܓܡܐ ܚܠܦ ܢܦܫܗ ܝܗܒ ܠܐܠܗܐ ܀
12Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
13ܠܐ ܡܟܝܠ ܢܕܘܢ ܚܕ ܠܚܕ ܐܠܐ ܗܕܐ ܕܘܢܘ ܝܬܝܪܐܝܬ ܕܬܘܩܠܬܐ ܠܐܚܘܟ ܠܐ ܬܤܝܡ ܀
13Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
14ܝܕܥ ܐܢܐ ܓܝܪ ܘܡܦܤ ܐܢܐ ܒܡܪܝܐ ܝܫܘܥ ܕܡܕܡ ܕܡܤܝܒ ܡܢ ܠܘܬܗ ܠܝܬ ܐܠܐ ܠܐܝܢܐ ܕܪܢܐ ܥܠ ܡܕܡ ܕܛܡܐ ܠܗܘ ܗܘ ܒܠܚܘܕ ܛܡܐ ܀
14Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
15ܐܢ ܕܝܢ ܡܛܠ ܡܐܟܘܠܬܐ ܡܥܝܩ ܐܢܬ ܠܐܚܘܟ ܠܐ ܗܘܐ ܒܚܘܒܐ ܡܗܠܟ ܐܢܬ ܠܐ ܬܘܒܕ ܒܡܐܟܘܠܬܟ ܠܗܘ ܕܡܛܠܬܗ ܡܝܬ ܡܫܝܚܐ ܀
15Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
16ܘܠܐ ܬܬܓܕܦ ܛܒܬܢ ܀
16Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
17ܡܠܟܘܬܗ ܓܝܪ ܕܐܠܗܐ ܠܐ ܗܘܬ ܡܐܟܠܐ ܘܡܫܬܝܐ ܐܠܐ ܟܐܢܘܬܐ ܘܫܠܡܐ ܘܚܕܘܬܐ ܒܪܘܚܐ ܕܩܘܕܫܐ ܀
17Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
18ܡܢ ܕܒܗܠܝܢ ܓܝܪ ܡܫܡܫ ܠܡܫܝܚܐ ܫܦܪ ܠܐܠܗܐ ܘܩܕܡ ܒܢܝܢܫܐ ܒܩܐ ܀
18Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
19ܗܫܐ ܒܬܪ ܫܠܡܐ ܢܪܗܛ ܘܒܬܪ ܒܢܝܢܐ ܚܕ ܕܚܕ ܀
19Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
20ܘܠܐ ܡܛܠ ܡܐܟܘܠܬܐ ܢܫܪܐ ܥܒܕܐ ܕܐܠܗܐ ܟܠܡܕܡ ܓܝܪ ܕܟܐ ܗܘ ܐܠܐ ܒܝܫ ܗܘ ܠܒܪܢܫܐ ܕܒܬܘܩܠܬܐ ܐܟܠ ܀
20Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
21ܫܦܝܪ ܗܘ ܕܠܐ ܢܐܟܘܠ ܒܤܪܐ ܘܠܐ ܢܫܬܐ ܚܡܪܐ ܘܠܐ ܡܕܡ ܕܡܬܬܩܠ ܒܗ ܐܚܘܢ ܀
21Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
22ܐܢܬ ܕܐܝܬ ܒܟ ܗܝܡܢܘܬܐ ܒܢܦܫܟ ܐܚܘܕܝܗ ܩܕܡ ܐܠܗܐ ܛܘܒܘܗܝ ܠܡܢ ܕܠܐ ܕܢ ܢܦܫܗ ܒܡܕܡ ܕܦܪܫ ܀
22Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
23ܐܝܢܐ ܓܝܪ ܕܡܬܦܠܓ ܘܐܟܠ ܐܬܚܝܒ ܠܗ ܡܛܠ ܕܠܘ ܒܗܝܡܢܘܬܐ ܟܠ ܡܕܡ ܓܝܪ ܕܠܐ ܗܘܐ ܡܢ ܗܝܡܢܘܬܐ ܚܛܝܬܐ ܗܘ ܀
23Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.