Turkish

Swahili: New Testament

2 Timothy

2

1Oğlum, Mesih İsada olan lütufla güçlen.
1Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
2Birçok tanık önünde benden işittiğin sözleri, başkalarına da öğretmeye yeterli olacak güvenilir kişilere emanet et.
2Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
3Mesih İsanın iyi bir askeri olarak benimle birlikte sıkıntıya göğüs ger.
3Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
4Askerlik yapan kişi günlük yaşamla ilgili işlere karışmaz; kendisini askerliğe çağıranı hoşnut etmeye çalışır.
4Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
5Bunun gibi, spor yarışmasına katılan kişi de kurallar uyarınca yarışmazsa zafer tacını giyemez.
5Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
6Emek veren çiftçi üründen ilk payı alan kişi olmalıdır.
6Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
7Dediklerimi iyi düşün. Rab sana her konuda anlayış verecektir.
7Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
8Yaydığım Müjdede açıklandığı gibi, Davutun soyundan olup ölümden dirilmiş olan İsa Mesihi anımsa.
8Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
9Bu Müjde uğruna bir suçlu gibi zincire vurulmaya kadar varan sıkıntılara katlanıyorum. Ama Tanrının sözü zincire vurulmuş değildir.
9Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
10Bunun içindir ki, seçilmişler uğruna her şeye dayanıyorum. Öyle ki, onlar da sonsuz yüceliğin yanısıra Mesih İsada olan kurtuluşa kavuşsunlar.
10na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele.
11Şu güvenilir bir sözdür: ‹‹Onunla birlikte öldüysek, Onunla birlikte yaşayacağız.
11Usemi huu ni wa kweli: "Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12Dayanırsak, Onunla birlikte egemenlik süreceğiz. Onu inkâr edersek, O da bizi inkâr edecek.
12Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
13Biz sadık kalmasak da, O sadık kalacak. Çünkü kendi özüne aykırı davranamaz.››
13Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe."
14Bu konuları imanlılara anımsat. Dinleyenleri felakete sürüklemekten başka yararı olmayan kelime kavgaları çıkarmamaları için onları Tanrının önünde uyar.
14Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
15Kendini Tanrıya makbul, gerçeğin bildirisini doğru kullanan, alnı ak bir işçi olarak sunmaya gayret et.
15Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
16Bayağı, boş sözlerden sakın. Çünkü bunlara dalanlar tanrısızlıkta daha da ileri gidecekler.
16Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
17Sözleri kangren gibi yayılacak. Himeneosla Filitos bunlardandır.
17Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
18Diriliş olup bitti diyerek gerçek yoldan saptılar. Şimdi de bazılarının imanını altüst ediyorlar.
18Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
19Ne var ki, Tanrının attığı sağlam temel, ‹‹Rab kendine ait olanları bilir›› ve ‹‹Rabbin adını anan herkes kötülükten uzak dursun›› sözleriyle mühürlenmiş olarak duruyor.
19Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: "Bwana anawafahamu wale walio wake," na "Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu."
20Büyük bir evde yalnız altın ve gümüş kaplar bulunmaz; tahta ve toprak kaplar da vardır. Kimi onurlu, kimi bayağı iş için kullanılır.
20Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
21Bunun gibi, kişi de kendini bayağı işlerden arıtırsa, onurlu amaçlara uygun, kutsal kılınmış, efendisine yararlı, her iyi işe hazır bir kap olur.
21Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
22Gençlik arzularından kaç. Temiz yürekle Rabbe yakaranlarla birlikte doğruluğun, imanın, sevginin ve esenliğin ardından koş.
22Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
23Saçma, cahilce tartışmalara girmeyi reddet. Bunların kavga doğurduğunu bilirsin.
23Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
24Rabbin kulu kavgacı olmamalı. Tersine, herkese şefkatle davranmalı, öğretme yeteneği olmalı, haksızlıklara sabırla dayanmalıdır.
24Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
25Kendisine karşı olanları yumuşak huyla yola getirmeli. Gerçeği anlamaları için Tanrı belki onlara bir tövbe yolu açar.
25ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
26Böylelikle ayılabilir, isteğini yerine getirmeleri için kendilerini tutsak eden İblis'in tuzağından kurtulabilirler.
26Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.