1Ey efendiler, gökte sizin de bir Efendiniz olduğunu bilerek kölelerinize adalet ve eşitlikle davranın.
1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2Kendinizi duaya verin. Duada uyanık kalın, şükredin.
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3Aynı zamanda bizim için de dua edin ki Tanrı, sözünü yaymamız ve uğruna hapsedildiğim Mesih sırrını açıklamamız için bize bir kapı açsın.
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4Bu sırrı gerektiği gibi açıklıkla bildirebilmem için dua edin.
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5Sizden olmayanlara karşı bilgece davranın. Fırsatı değerlendirin.
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6Sözünüz tuzla terbiye edilmiş gibi her zaman lütufla dolu olsun. Böylece herkese nasıl karşılık vermek gerektiğini bileceksiniz.
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7Rab yolunda emektaşım ve güvenilir bir hizmetkâr olan sevgili kardeşimiz Tihikos, benimle ilgili her şeyi size bildirecektir.
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8İşte bu amaçla, durumumuzu iletmesi ve yüreklerinize cesaret vermesi için kendisini size gönderiyorum.
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9Onunla birlikte, sizden biri olan, güvenilir ve sevgili kardeş Onisimosu da gönderiyorum. Burada olup biten her şeyi size bildirecekler.
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10Hapishane arkadaşım Aristarhus ve Barnabanın yeğeni Markos size selam ederler. Markosla ilgili buyruklar aldınız; yanınıza gelirse kendisini kabul edin.
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11Yustus diye tanınan Yeşu da size selam eder. Tanrının Egemenliği için çalışan emektaşım Yahudiler yalnız bunlardır. Bunlar bana teselli oldular.
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12Sizden biri ve Mesih İsanın kulu olan Epafras size selam eder. Tanrının her isteğinden emin, yetkin kişiler olarak ayakta kalasınız diye sizin için her zaman duayla mücadele ediyor.
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13Gerek sizin gerekse Laodikya ve Hierapolistekiler için çok emek verdiğine tanıklık ederim.
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14Sevgili hekim Lukayla Dimas da size selam ederler.
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15Laodikyadaki kardeşlere, Nimfaya ve evindeki topluluğa selam edin.
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16Bu mektup aranızda okunduktan sonra Laodikya kilisesine de okutun. Siz de Laodikyadan gelecek mektubu okuyun.
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17Arhippusa, ‹‹Rab yolunda üstlendiğin görevi tamamlamaya dikkat et!›› deyin.
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18Ben Pavlus bu selamı elimle yazıyorum. Zincire vurulduğumu unutmayın. Tanrı'nın lütfu sizinle birlikte olsun.
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.