Turkish

Swahili: New Testament

Galatians

2

1On dört yıl aradan sonra Titusu da yanıma alıp Barnabayla birlikte yine Yeruşalime gittim.
1Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
2Vahiy uyarınca gittim. Boş yere koşmayayım ya da koşmuş olmayayım diye, öteki uluslar arasında yaydığım Müjdeyi özel olarak ileri gelenlere sundum.
2Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
3Benimle birlikte olan Titus bile Grek olmasına karşın sünnet edilmeye zorlanmadı.
3Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
4Ne var ki, İsa Mesihte sahip olduğumuz özgürlüğü el altından öğrenmek ve böylece bizi köleleştirmek için gizlice aramıza sızan sahte kardeşler vardı.
4ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
5Müjde gerçeği sürekli sizinle kalsın diye bir an bile onlara boyun eğip teslim olmadık.
5Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
6Ama ileri gelenler -ne oldukları bence önemli değil, Tanrı insanlar arasında ayrım yapmaz- evet, bu ileri gelenler söylediklerime bir şey katmadılar.
6Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi--kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje--watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
7Tam tersine, Müjdeyi sünnetlilere bildirme işi nasıl Petrusa verildiyse, sünnetsizlere bildirme işinin de bana verildiğini gördüler.
7Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
8Çünkü sünnetlilere elçilik etmesi için Petrusta etkin olan Tanrı, öteki uluslara elçilik etmem için bende de etkin oldu.
8Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
9Topluluğun direkleri sayılan Yakup, Kefas ve Yuhanna bana bağışlanan lütfu sezince paydaşlığımızın işareti olarak bana ve Barnabaya sağ ellerini uzattılar. Öteki uluslara bizlerin, Yahudilere kendilerinin gitmesini uygun gördüler.
9Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
10Ancak yoksulları anımsamamızı istediler. Zaten ben de bunu yapmaya gayret ediyordum.
10Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
11Ne var ki, Kefas Antakyaya geldiği zaman, suçlu olduğu için ona açıkça karşı geldim.
11Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
12Çünkü Yakupun yanından bazı adamlar gelmeden önce Kefas öteki uluslardan olanlarla birlikte yemek yerdi. Ama o adamlar gelince sünnet yanlılarından korkarak sünnetsizlerden uzaklaştı, onlarla yemek yemez oldu.
12Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
13Öbür Yahudiler de onun gibi ikiyüzlülük ettiler. Sonunda Barnaba bile onların ikiyüzlülüğüne kapıldı.
13Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
14Müjde gerçeğine uygun davranmadıklarını görünce hepsinin önünde Kefasa şöyle dedim: ‹‹Yahudi olduğun halde Yahudi gibi değil, öteki uluslardan biri gibi yaşıyorsun, nasıl olur da ulusları Yahudi gibi yaşamaya zorlarsın?
14Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: "Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?"
15Doğuştan Yahudi olan bizler öteki uluslardan olan ‹günahlılar› değiliz.
15Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
16Yine de insanın Kutsal Yasanın gereklerini yaparak değil, İsa Mesihe iman ederek aklandığını biliyoruz. Bunun için biz de Yasanın gereklerini yaparak değil, Mesihe iman ederek aklanalım diye Mesih İsaya iman ettik. Çünkü hiç kimse Yasanın gereklerini yaparak aklanmaz.
16Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
17Mesihte aklanmak isterken kendimiz günahlı çıkarsak, Mesih günahın yardakçısı mı olur? Kesinlikle hayır!
17Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
18Yıktığımı yeniden kurarsam, yasayı çiğnediğimi kanıtlamış olurum.
18Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
19Çünkü ben Tanrı için yaşamak üzere Yasa aracılığıyla Yasa karşısında öldüm.
19Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
20Mesihle birlikte çarmıha gerildim. Artık ben yaşamıyorum, Mesih bende yaşıyor. Şimdi bedende sürdürdüğüm yaşamı, beni seven ve benim için kendini feda eden Tanrı Oğluna imanla sürdürüyorum.
20na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
21Tanrı'nın lütfunu geçersiz saymış değilim. Çünkü aklanma Yasa aracılığıyla sağlanabilseydi, o zaman Mesih boş yere ölmüş olurdu.››
21Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!