Turkish

Swahili: New Testament

Hebrews

1

1Tanrı eski zamanlarda peygamberler aracılığıyla birçok kez çeşitli yollardan atalarımıza seslendi.
1Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
2Bu son çağda da her şeye mirasçı kıldığı ve aracılığıyla evreni yarattığı kendi Oğluyla bize seslenmiştir.
2lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote.
3Oğul, Tanrı yüceliğinin parıltısı, Onun varlığının öz görünümüdür. Güçlü sözüyle her şeyi devam ettirir. Günahlardan arınmayı sağladıktan sonra, yücelerde ulu Tanrının sağında oturdu.
3Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
4Meleklerden ne denli üstün bir adı miras aldıysa, onlardan o denli üstün oldu.
4Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
5Çünkü Tanrı meleklerin herhangi birine, ‹‹Sen benim Oğlumsun, Bugün ben sana Baba oldum›› Ya da, ‹‹Ben Ona Baba olacağım, O da bana Oğul olacak››
5Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: "Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako." Wala hakusema juu ya malaika yeyote: "Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu."
6Yine Tanrı ilk doğanı dünyaya gönderirken diyor ki, ‹‹Tanrının bütün melekleri Ona tapınsın.››
6Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: "Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu."
7Melekler için, ‹‹Kendi meleklerini rüzgar, Hizmetkârlarını ateş alevi yapar›› diyor.
7Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: "Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto."
8Ama Oğul için şöyle diyor: ‹‹Ey Tanrı, tahtın sonsuzluklar boyunca kalıcıdır, Egemenliğinin asası adalet asasıdır.
8Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: "Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki.
9Doğruluğu sevdin, kötülükten nefret ettin. Bunun için Tanrı, senin Tanrın, Seni sevinç yağıyla Arkadaşlarından daha çok meshetti.››
9Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako."
10Yine diyor ki, ‹‹Ya Rab, başlangıçta Dünyanın temellerini sen attın. Gökler de senin ellerinin yapıtıdır.
10Pia alisema: "Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
11Onlar yok olacak, ama sen kalıcısın. Hepsi bir giysi gibi eskiyecek.
11Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
12Bir kaftan gibi düreceksin onları, Bir giysi gibi değiştirilecekler. Ama sen hep aynısın, Yılların tükenmeyecek.››
12Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma."
13Tanrı meleklerin herhangi birine, ‹‹Ben düşmanlarını Ayaklarının altına serinceye dek, Sağımda otur››
13Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: "Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako."
14Bütün melekler kurtuluşu miras alacaklara hizmet etmek için gönderilen görevli ruhlar değil midir?
14Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.