Turkish

Swahili: New Testament

Hebrews

11

1İman, umut edilenlere güvenmek, görünmeyen şeylerin varlığından emin olmaktır.
1Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
2Atalarımız bununla Tanrının beğenisini kazandılar.
2Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
3Evrenin Tanrının buyruğuyla yaratıldığını, böylece görülenlerin görünmeyenlerden oluştuğunu iman sayesinde anlıyoruz.
3Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana.
4Habilin Tanrıya Kayinden daha iyi bir kurban sunması iman sayesinde oldu. İmanı sayesinde doğru biri olarak Tanrının beğenisini kazandı. Çünkü Tanrı onun sunduğu adakları kabul etti. Nitekim Habil ölmüş olduğu halde, iman sayesinde hâlâ konuşmaktadır.
4Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
5İman sayesinde Hanok ölümü tatmamak üzere yukarı alındı. Kimse onu bulamadı, çünkü Tanrı onu yukarı almıştı. Yukarı alınmadan önce Tanrıyı hoşnut eden biri olduğuna tanıklık edildi.
5Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
6İman olmadan Tanrıyı hoşnut etmek olanaksızdır. Tanrıya yaklaşan, Onun var olduğuna ve kendisini arayanları ödüllendireceğine iman etmelidir.
6Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
7İman sayesinde Nuh, henüz olmamış olaylarla ilgili olarak Tanrı tarafından uyarılınca, Tanrı korkusuyla ev halkının kurtuluşu için bir gemi yaptı. Bununla dünyayı yargıladı ve imana dayanan doğruluğun mirasçısı oldu.
7Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
8İman sayesinde İbrahim miras alacağı yere gitmesi için çağrılınca, Tanrının sözünü dinledi ve nereye gideceğini bilmeden yola çıktı.
8Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
9İman sayesinde bir yabancı olarak vaat edilen ülkeye yerleşti. Aynı vaadin ortak mirasçıları olan İshak ve Yakupla birlikte çadırlarda yaşadı.
9Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
10Çünkü mimarı ve kurucusu Tanrı olan temelli kenti bekliyordu.
10Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
11İman sayesinde Saranın kendisi de kısır ve yaşı geçmiş olduğu halde vaat edeni güvenilir saydığından çocuk sahibi olmak için güç buldu.
11Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
12Böylece tek bir adamdan, üstelik ölüden farksız birinden gökteki yıldızlar, deniz kıyısındaki kum kadar sayısız torun meydana geldi.
12Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
13Bu kişilerin hepsi imanlı olarak öldüler. Vaat edilenlere kavuşamadılarsa da bunları uzaktan görüp selamladılar, yeryüzünde yabancı ve konuk olduklarını açıkça kabul ettiler.
13Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
14Böyle konuşanlar bir vatan aradıklarını gösteriyorlar.
14Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
15Ayrıldıkları ülkeyi düşünselerdi, geri dönmeye fırsatları olurdu.
15Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16Ama onlar daha iyisini, yani göksel olanı arzu ediyorlardı. Bunun içindir ki, Tanrı onların Tanrısı olarak anılmaktan utanmıyor. Çünkü onlara bir kent hazırladı.
16Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
17İbrahim sınandığı zaman imanla İshakı kurban olarak sundu. Vaatleri almış olan İbrahim biricik oğlunu kurban etmek üzereydi.
17Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
18Oysa Tanrı ona, ‹‹Senin soyun İshakla sürecek›› demişti.
18ingawa Mungu alikuwa amemwambia: "Wazawa wako watatokana na Isaka."
19İbrahim Tanrının ölüleri bile diriltebileceğini düşündü; nitekim İshakı simgesel şekilde ölümden geri aldı.
19Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
20İman sayesinde İshak gelecek olaylarla ilgili olarak Yakupla Esavı kutsadı.
20Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
21Yakup ölürken iman sayesinde Yusufun iki oğlunu da kutsadı, değneğinin ucuna yaslanarak Tanrıya tapındı.
21Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
22Yusuf ölürken iman sayesinde İsrailoğullarının Mısırdan çıkacağını anımsattı ve kemiklerine ilişkin buyruk verdi.
22Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
23Musa doğduğunda annesiyle babası onu imanla üç ay gizlediler. Çünkü çocuğun güzel olduğunu gördüler ve kralın fermanından korkmadılar.
23Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24Musa büyüyünce iman sayesinde firavunun kızının oğlu olarak tanınmayı reddetti.
24Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25Bir süre için günahın sefasını sürmektense, Tanrının halkıyla birlikte baskı görmeyi yeğledi.
25Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
26Mesih uğruna aşağılanmayı Mısır hazinelerinden daha büyük zenginlik saydı. Çünkü alacağı ödülü düşünüyordu.
26Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
27Kralın öfkesinden korkmadan imanla Mısırdan ayrıldı. Görünmez Olanı görür gibi dayandı.
27Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
28İlk doğanları öldüren melek İsraillilere dokunmasın diye Musa imanla, Fısıh kurbanının kesilmesini ve kanının kapılara sürülmesini sağladı.
28Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
29İman sayesinde İsrailliler karadan geçer gibi Kızıldenizden geçtiler. Mısırlılar bunu deneyince boğuldular.
29Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
30İsrailliler yedi gün boyunca Eriha surları çevresinde dolandılar; sonunda imanları sayesinde surlar yıkıldı.
30Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
31Fahişe Rahav casusları dostça karşıladığı için imanı sayesinde söz dinlemeyenlerle birlikte öldürülmedi.
31Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
32Daha ne diyeyim? Gidyon, Barak, Şimşon, Yiftah, Davut, Samuel ve peygamberlerle ilgili olanları anlatsam, zaman yetmeyecek.
32Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
33Bunlar iman sayesinde ülkeler ele geçirdiler, adaleti sağladılar, vaat edilenlere kavuştular, aslanların ağzını kapadılar.
33Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
34Kızgın ateşi söndürdüler, kılıcın ağzından kaçıp kurtuldular. Güçsüzlükte kuvvet buldular, savaşta güçlendiler, yabancı orduları bozguna uğrattılar.
34Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
35Kadınlar dirilen ölülerini geri aldılar. Başkalarıysa salıverilmeyi reddederek dirilip daha iyi bir yaşama kavuşma umuduyla işkencelere katlandılar.
35Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
36Daha başkaları alaya alınıp kamçılandı, hatta zincire vurulup hapsedildi.
36Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
37Taşlandılar, testereyle biçildiler, kılıçtan geçirilip öldürüldüler. Koyun postu, keçi derisi içinde dolaştılar, yoksulluk çektiler, sıkıntılara uğradılar, baskı gördüler.
37Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
38Dünya onlara layık değildi. Çöllerde, dağlarda, mağaralarda, yeraltı oyuklarında dolanıp durdular.
38Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
39İmanları sayesinde bunların hepsi Tanrının beğenisini kazandıkları halde, hiçbiri vaat edilene kavuşmadı.
39Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
40Bizden ayrı olarak yetkinliğe ermesinler diye, Tanrı bizim için daha iyi bir şey hazırlamıştı.
40maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.