Turkish

Swahili: New Testament

Revelation

5

1Tahtta oturanın sağ elinde iki yanı da yazılı, yedi mühürle mühürlenmiş bir tomar gördüm.
1Kisha katika mkono wa kulia wa huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, nikaona kitabu; nacho kilikuwa kimeandikwa ndani na nje na kufungwa na mihuri saba.
2Yüksek sesle, ‹‹Tomarı açmaya, mühürlerini çözmeye kim layıktır?›› diye seslenen güçlü bir melek de gördüm.
2Tena nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: "Nani anayestahili kuvunja hiyo mihuri na kukifungua kitabu hicho?"
3Ama ne gökte, ne yeryüzünde, ne de yer altında tomarı açıp içine bakabilecek kimse yoktu.
3Lakini hakupatikana mtu yeyote mbinguni, wala duniani, wala chini Kuzimu, aliyeweza kukifungua hicho kitabu au kukitazama ndani.
4Acı acı ağlamaya başladım. Çünkü tomarı açıp içine bakmaya layık kimse bulunamadı.
4Basi, mimi nikalia sana kwa sababu hakupatikana mtu aliyestahili kukifungua, au kukitazama ndani.
5Bunun üzerine ihtiyarlardan biri bana, ‹‹Ağlama!›› dedi. ‹‹İşte, Yahuda oymağından gelen Aslan, Davutun Kökü galip geldi. Tomarı ve yedi mührünü O açacak.››
5Kisha mmoja wa wale wazee akaniambia, "Usilie! Tazama! Simba wa kabila la Yuda, mjukuu maarufu wa Daudi, ameshinda. Yeye anaweza kuivunja mihuri yake saba na kukifungua hicho kitabu."
6Tahtın, dört yaratığın ve ihtiyarların ortasında, boğazlanmış gibi duran bir Kuzu gördüm. Yedi boynuzu, yedi gözü vardı. Bunlar Tanrının bütün dünyaya gönderilmiş yedi ruhudur.
6Kisha nikaona pale katikati ya kiti cha enzi Mwana kondoo amesimama, akizungukwa kila upande na vile viumbe hai vinne, na wale wazee. Huyo Mwanakondoo alionekana kana kwamba amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba ambayo ni roho saba za Mungu zilizokuwa zimepelekwa kila mahali duniani.
7Kuzu gelip tahtta oturanın sağ elinden tomarı aldı.
7Mwanakondoo akaenda, akakitwaa hicho kitabu kutoka mkono wa kulia wa yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi.
8Tomarı alınca, dört yaratıkla yirmi dört ihtiyar Onun önünde yere kapandılar. Her birinin elinde birer lir ve kutsalların duaları olan buhur dolu altın taslar vardı.
8Mara tu alipokwisha twaa hicho kitabu, vile viumbe hai vinne pamoja na wale wazee ishirini na wanne walianguka kifudifudi mbele ya Mwanakondoo. Kila mmoja, alikuwa na kinubi na bakuli za dhahabu zilizojaa ubani, ambao ni sala za watu wa Mungu.
9Yeni bir ezgi söylüyorlardı: ‹‹Tomarı almaya, Mühürlerini açmaya layıksın! Çünkü boğazlandın Ve kanınla her oymaktan, her dilden, Her halktan, her ulustan İnsanları Tanrıya satın aldın.
9Basi, wakaimba wimbo huu mpya: "Wewe unastahili kukitwaa hicho kitabu na kuivunja mihuri yake. Kwa sababu wewe umechinjwa, na kwa damu yako umemnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
10Onları Tanrımızın hizmetinde Bir krallık haline getirdin, Kâhinler yaptın. Dünya üzerinde egemenlik sürecekler.››
10Wewe umewafanya wawe ufalme wa makuhani wamtumikie Mungu wetu nao watatawala duniani."
11Sonra tahtın, yaratıkların ve ihtiyarların çevresinde çok sayıda melek gördüm, seslerini işittim. Sayıları binlerce binler, on binlerce on binlerdi.
11Kisha nikatazama, nikasikia sauti ya malaika wengi sana, idadi isiyohesabika, maelfu na maelfu. Walikuwa wamekaa kuzunguka kiti cha enzi, vile viumbe hai vinne na wale wazee;
12Yüksek sesle şöyle diyorlardı: ‹‹Boğazlanmış Kuzu Gücü, zenginliği, bilgeliği, kudreti, Saygıyı, yüceliği, övgüyü Almaya layıktır.››
12wakasema kwa sauti kuu: "Mwanakondoo aliyechinjwa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, utukufu na sifa."
13Ardından gökte, yeryüzünde, yer altında ve denizlerdeki bütün yaratıkların, bunlardaki bütün varlıkların şöyle dediğini işittim: ‹‹Övgü, saygı, yücelik ve güç sonsuzlara dek Tahtta oturanın ve Kuzunun olsun!››
13Nikasikia viumbe vyote mbinguni, duniani, chini kuzimuni na baharini--viumbe vyote ulimwenguni--vikisema: "Kwake yeye aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo, iwe sifa na heshima na utukufu na enzi milele na milele."
14Dört yaratık, ‹‹Amin›› dediler. İhtiyarlar da yere kapanıp tapındılar.
14Na vile viumbe vinne hai vikasema, "Amina!" Na wale wazee wakaanguka kifudifudi, wakaabudu.