1Now I would not have you ignorant, brothers, that our fathers were all under the cloud, and all passed through the sea;
1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
2and were all baptized into Moses in the cloud and in the sea;
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
3and all ate the same spiritual food;
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
4and all drank the same spiritual drink. For they drank of a spiritual rock that followed them, and the rock was Christ.
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
5However with most of them, God was not well pleased, for they were overthrown in the wilderness.
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
6Now these things were our examples, to the intent we should not lust after evil things, as they also lusted.
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
7Neither be idolaters, as some of them were. As it is written, “The people sat down to eat and drink, and rose up to play.” Exodus 32:6
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
8Neither let us commit sexual immorality, as some of them committed, and in one day twenty-three thousand fell.
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
9Neither let us test the Lord, as some of them tested, and perished by the serpents.
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
10Neither grumble, as some of them also grumbled, and perished by the destroyer.
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
11Now all these things happened to them by way of example, and they were written for our admonition, on whom the ends of the ages have come.
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
12Therefore let him who thinks he stands be careful that he doesn’t fall.
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
13No temptation has taken you except what is common to man. God is faithful, who will not allow you to be tempted above what you are able, but will with the temptation also make the way of escape, that you may be able to endure it.
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
14Therefore, my beloved, flee from idolatry.
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
15I speak as to wise men. Judge what I say.
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
16The cup of blessing which we bless, isn’t it a sharing of the blood of Christ? The bread which we break, isn’t it a sharing of the body of Christ?
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
17Because there is one loaf of bread, we, who are many, are one body; for we all partake of the one loaf of bread.
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
18Consider Israel according to the flesh. Don’t those who eat the sacrifices participate in the altar?
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
19What am I saying then? That a thing sacrificed to idols is anything, or that an idol is anything?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
20But I say that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons, and not to God, and I don’t desire that you would have fellowship with demons.
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
21You can’t both drink the cup of the Lord and the cup of demons. You can’t both partake of the table of the Lord, and of the table of demons.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
22Or do we provoke the Lord to jealousy? Are we stronger than he?
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
23“All things are lawful for me,” but not all things are profitable. “All things are lawful for me,” but not all things build up.
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
24Let no one seek his own, but each one his neighbor’s good.
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
25Whatever is sold in the butcher shop, eat, asking no question for the sake of conscience,
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
26for “the earth is the Lord’s, and its fullness.” Psalm 24:1
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
27But if one of those who don’t believe invites you to a meal, and you are inclined to go, eat whatever is set before you, asking no questions for the sake of conscience.
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
28But if anyone says to you, “This was offered to idols,” don’t eat it for the sake of the one who told you, and for the sake of conscience. For “the earth is the Lord’s, and all its fullness.”
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
29Conscience, I say, not your own, but the other’s conscience. For why is my liberty judged by another conscience?
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
30If I partake with thankfulness, why am I denounced for that for which I give thanks?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
31Whether therefore you eat, or drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
32Give no occasions for stumbling, either to Jews, or to Greeks, or to the assembly of God;
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
33even as I also please all men in all things, not seeking my own profit, but the profit of the many, that they may be saved.
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.