World English Bible

Swahili: New Testament

1 Corinthians

12

1Now concerning spiritual things, brothers, I don’t want you to be ignorant.
1Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2You know that when you were heathen , you were led away to those mute idols, however you might be led.
2Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3Therefore I make known to you that no man speaking by God’s Spirit says, “Jesus is accursed.” No one can say, “Jesus is Lord,” but by the Holy Spirit.
3Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4Now there are various kinds of gifts, but the same Spirit.
4Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5There are various kinds of service, and the same Lord.
5Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6There are various kinds of workings, but the same God, who works all things in all.
6Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7But to each one is given the manifestation of the Spirit for the profit of all.
7Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8For to one is given through the Spirit the word of wisdom, and to another the word of knowledge, according to the same Spirit;
8Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9to another faith, by the same Spirit; and to another gifts of healings, by the same Spirit;
9Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10and to another workings of miracles; and to another prophecy; and to another discerning of spirits; to another different kinds of languages; and to another the interpretation of languages.
10humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11But the one and the same Spirit works all of these, distributing to each one separately as he desires.
11Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12For as the body is one, and has many members, and all the members of the body, being many, are one body; so also is Christ.
12Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13For in one Spirit we were all baptized into one body, whether Jews or Greeks, whether bond or free; and were all given to drink into one Spirit.
13Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14For the body is not one member, but many.
14Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15If the foot would say, “Because I’m not the hand, I’m not part of the body,” it is not therefore not part of the body.
15Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16If the ear would say, “Because I’m not the eye, I’m not part of the body,” it’s not therefore not part of the body.
16Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17If the whole body were an eye, where would the hearing be? If the whole were hearing, where would the smelling be?
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18But now God has set the members, each one of them, in the body, just as he desired.
18Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19If they were all one member, where would the body be?
19Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20But now they are many members, but one body.
20Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21The eye can’t tell the hand, “I have no need for you,” or again the head to the feet, “I have no need for you.”
21Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."
22No, much rather, those members of the body which seem to be weaker are necessary.
22Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23Those parts of the body which we think to be less honorable, on those we bestow more abundant honor; and our unpresentable parts have more abundant propriety;
23Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24whereas our presentable parts have no such need. But God composed the body together, giving more abundant honor to the inferior part,
24ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25that there should be no division in the body, but that the members should have the same care for one another.
25ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26When one member suffers, all the members suffer with it. Or when one member is honored, all the members rejoice with it.
26Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27Now you are the body of Christ, and members individually.
27Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28God has set some in the assembly: first apostles, second prophets, third teachers, then miracle workers, then gifts of healings, helps, governments, and various kinds of languages.
28Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29Are all apostles? Are all prophets? Are all teachers? Are all miracle workers?
29Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30Do all have gifts of healings? Do all speak with various languages? Do all interpret?
30Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31But earnestly desire the best gifts. Moreover, I show a most excellent way to you.
31Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.