World English Bible

Swahili: New Testament

1 Corinthians

3

1Brothers, I couldn’t speak to you as to spiritual, but as to fleshly, as to babies in Christ.
1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2I fed you with milk, not with meat; for you weren’t yet ready. Indeed, not even now are you ready,
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3for you are still fleshly. For insofar as there is jealousy, strife, and factions among you, aren’t you fleshly, and don’t you walk in the ways of men?
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4For when one says, “I follow Paul,” and another, “I follow Apollos,” aren’t you fleshly?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5Who then is Apollos, and who is Paul, but servants through whom you believed; and each as the Lord gave to him?
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6I planted. Apollos watered. But God gave the increase.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7So then neither he who plants is anything, nor he who waters, but God who gives the increase.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8Now he who plants and he who waters are the same, but each will receive his own reward according to his own labor.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9For we are God’s fellow workers. You are God’s farming, God’s building.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10According to the grace of God which was given to me, as a wise master builder I laid a foundation, and another builds on it. But let each man be careful how he builds on it.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11For no one can lay any other foundation than that which has been laid, which is Jesus Christ.
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12But if anyone builds on the foundation with gold, silver, costly stones, wood, hay, or stubble;
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13each man’s work will be revealed. For the Day will declare it, because it is revealed in fire; and the fire itself will test what sort of work each man’s work is.
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14If any man’s work remains which he built on it, he will receive a reward.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15If any man’s work is burned, he will suffer loss, but he himself will be saved, but as through fire.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16Don’t you know that you are a temple of God, and that God’s Spirit lives in you?
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17If anyone destroys the temple of God, God will destroy him; for God’s temple is holy, which you are.
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18Let no one deceive himself. If anyone thinks that he is wise among you in this world, let him become a fool, that he may become wise.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
19For the wisdom of this world is foolishness with God. For it is written, “He has taken the wise in their craftiness.”
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
20And again, “The Lord knows the reasoning of the wise, that it is worthless.”
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
21Therefore let no one boast in men. For all things are yours,
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22whether Paul, or Apollos, or Cephas, or the world, or life, or death, or things present, or things to come. All are yours,
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23and you are Christ’s, and Christ is God’s.
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.