World English Bible

Swahili: New Testament

2 Thessalonians

3

1Finally, brothers, pray for us, that the word of the Lord may spread rapidly and be glorified, even as also with you;
1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2and that we may be delivered from unreasonable and evil men; for not all have faith.
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3But the Lord is faithful, who will establish you, and guard you from the evil one.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4We have confidence in the Lord concerning you, that you both do and will do the things we command.
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5May the Lord direct your hearts into the love of God, and into the patience of Christ.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6Now we command you, brothers, in the name of our Lord Jesus Christ, that you withdraw yourselves from every brother who walks in rebellion, and not after the tradition which they received from us.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7For you know how you ought to imitate us. For we didn’t behave ourselves rebelliously among you,
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8neither did we eat bread from anyone’s hand without paying for it, but in labor and travail worked night and day, that we might not burden any of you;
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9not because we don’t have the right, but to make ourselves an example to you, that you should imitate us.
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10For even when we were with you, we commanded you this: “If anyone will not work, neither let him eat.”
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
11For we hear of some who walk among you in rebellion, who don’t work at all, but are busybodies.
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12Now those who are that way, we command and exhort in the Lord Jesus Christ, that with quietness they work, and eat their own bread.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13But you, brothers, don’t be weary in doing well.
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14If any man doesn’t obey our word in this letter, note that man, that you have no company with him, to the end that he may be ashamed.
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15Don’t count him as an enemy, but admonish him as a brother.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16Now may the Lord of peace himself give you peace at all times in all ways. The Lord be with you all.
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17The greeting of me, Paul, with my own hand, which is the sign in every letter: this is how I write.
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18The grace of our Lord Jesus Christ be with you all. Amen.
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.