1Paul, an apostle of Christ Jesus through the will of God, to the saints who are at Ephesus, and the faithful in Christ Jesus:
1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
2Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who has blessed us with every spiritual blessing in the heavenly places in Christ;
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4even as he chose us in him before the foundation of the world, that we would be holy and without blemish before him in love;
4Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5having predestined us for adoption as children through Jesus Christ to himself, according to the good pleasure of his desire,
5Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6to the praise of the glory of his grace, by which he freely bestowed favor on us in the Beloved,
6Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7in whom we have our redemption through his blood, the forgiveness of our trespasses, according to the riches of his grace,
7Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8which he made to abound toward us in all wisdom and prudence,
8aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9making known to us the mystery of his will, according to his good pleasure which he purposed in him
9Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10to an administration of the fullness of the times, to sum up all things in Christ, the things in the heavens, and the things on the earth, in him;
10Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11in whom also we were assigned an inheritance, having been foreordained according to the purpose of him who works all things after the counsel of his will;
11Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12to the end that we should be to the praise of his glory, we who had before hoped in Christ:
12Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13in whom you also, having heard the word of the truth, the Good News of your salvation—in whom, having also believed, you were sealed with the Holy Spirit of promise,
13Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14who is a pledge of our inheritance, to the redemption of God’s own possession, to the praise of his glory.
14Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15For this cause I also, having heard of the faith in the Lord Jesus which is among you, and the love which you have toward all the saints,
15Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16don’t cease to give thanks for you, making mention of you in my prayers,
16sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17that the God of our Lord Jesus Christ, the Father of glory, may give to you a spirit of wisdom and revelation in the knowledge of him;
17ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18having the eyes of your hearts TR reads “understanding” instead of “hearts” enlightened, that you may know what is the hope of his calling, and what are the riches of the glory of his inheritance in the saints,
18Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19and what is the exceeding greatness of his power toward us who believe, according to that working of the strength of his might
19mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20which he worked in Christ, when he raised him from the dead, and made him to sit at his right hand in the heavenly places,
20aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21far above all rule, and authority, and power, and dominion, and every name that is named, not only in this age, but also in that which is to come.
21Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao.
22He put all things in subjection under his feet, and gave him to be head over all things for the assembly,
22Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23which is his body, the fullness of him who fills all in all.
23Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.