1Children, obey your parents in the Lord, for this is right.
1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2“Honor your father and mother,” which is the first commandment with a promise:
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3“that it may be well with you, and you may live long on the earth.” Deuteronomy 5:16
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
4You fathers, don’t provoke your children to wrath, but nurture them in the discipline and instruction of the Lord.
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5Servants, be obedient to those who according to the flesh are your masters, with fear and trembling, in singleness of your heart, as to Christ;
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6not in the way of service only when eyes are on you, as men pleasers; but as servants of Christ, doing the will of God from the heart;
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7with good will doing service, as to the Lord, and not to men;
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8knowing that whatever good thing each one does, he will receive the same again from the Lord, whether he is bound or free.
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9You masters, do the same things to them, and give up threatening, knowing that he who is both their Master and yours is in heaven, and there is no partiality with him.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10Finally, be strong in the Lord, and in the strength of his might.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11Put on the whole armor of God, that you may be able to stand against the wiles of the devil.
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12For our wrestling is not against flesh and blood, but against the principalities, against the powers, against the world’s rulers of the darkness of this age, and against the spiritual forces of wickedness in the heavenly places.
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
13Therefore put on the whole armor of God, that you may be able to withstand in the evil day, and, having done all, to stand.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14Stand therefore, having the utility belt of truth buckled around your waist, and having put on the breastplate of righteousness,
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15and having fitted your feet with the preparation of the Good News of peace;
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16above all, taking up the shield of faith, with which you will be able to quench all the fiery darts of the evil one.
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17And take the helmet of salvation, and the sword of the Spirit, which is the word from Greek rhema, which means spoken word of God;
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18with all prayer and requests, praying at all times in the Spirit, and being watchful to this end in all perseverance and requests for all the saints:
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19on my behalf, that utterance may be given to me in opening my mouth, to make known with boldness the mystery of the Good News,
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20for which I am an ambassador in chains; that in it I may speak boldly, as I ought to speak.
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21But that you also may know my affairs, how I am doing, Tychicus, the beloved brother and faithful servant in the Lord, will make known to you all things;
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22whom I have sent to you for this very purpose, that you may know our state, and that he may comfort your hearts.
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23Peace be to the brothers, and love with faith, from God the Father and the Lord Jesus Christ.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24Grace be with all those who love our Lord Jesus Christ with incorruptible love. Amen.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.