1Paul, an apostle (not from men, neither through man, but through Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead),
1Mimi Paulo mtume,
2and all the brothers The word for “brothers” here and where context allows may also be correctly translated “brothers and sisters” or “siblings.” who are with me, to the assemblies of Galatia:
2na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
3Grace to you and peace from God the Father, and our Lord Jesus Christ,
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
4who gave himself for our sins, that he might deliver us out of this present evil age, according to the will of our God and Father—
4Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa.
5to whom be the glory forever and ever. Amen.
5Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina.
6I marvel that you are so quickly deserting him who called you in the grace of Christ to a different “good news”;
6Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
7and there isn’t another “good news.” Only there are some who trouble you, and want to pervert the Good News of Christ.
7Lakini hakuna "Habari Njema" nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
8But even though we, or an angel from heaven, should preach to you any “good news” other than that which we preached to you, let him be cursed.
8Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
9As we have said before, so I now say again: if any man preaches to you any “good news” other than that which you received, let him be cursed.
9Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
10For am I now seeking the favor of men, or of God? Or am I striving to please men? For if I were still pleasing men, I wouldn’t be a servant of Christ.
10Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
11But I make known to you, brothers, concerning the Good News which was preached by me, that it is not according to man.
11Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
12For neither did I receive it from man, nor was I taught it, but it came to me through revelation of Jesus Christ.
12Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
13For you have heard of my way of living in time past in the Jews’ religion, how that beyond measure I persecuted the assembly of God, and ravaged it.
13Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
14I advanced in the Jews’ religion beyond many of my own age among my countrymen, being more exceedingly zealous for the traditions of my fathers.
14Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
15But when it was the good pleasure of God, who separated me from my mother’s womb, and called me through his grace,
15Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
16to reveal his Son in me, that I might preach him among the Gentiles, I didn’t immediately confer with flesh and blood,
16Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
17nor did I go up to Jerusalem to those who were apostles before me, but I went away into Arabia. Then I returned to Damascus.
17na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
18Then after three years I went up to Jerusalem to visit Peter, and stayed with him fifteen days.
18Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
19But of the other apostles I saw no one, except James, the Lord’s brother.
19Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20Now about the things which I write to you, behold, before God, I’m not lying.
20Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
21Then I came to the regions of Syria and Cilicia.
21Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
22I was still unknown by face to the assemblies of Judea which were in Christ,
22Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
23but they only heard: “He who once persecuted us now preaches the faith that he once tried to destroy.”
23Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: "Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza."
24And they glorified God in me.
24Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.