World English Bible

Swahili: New Testament

John

4

1Therefore when the Lord knew that the Pharisees had heard that Jesus was making and baptizing more disciples than John
1Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2(although Jesus himself didn’t baptize, but his disciples),
2(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3he left Judea, and departed into Galilee.
3Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4He needed to pass through Samaria.
4na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5So he came to a city of Samaria, called Sychar, near the parcel of ground that Jacob gave to his son, Joseph.
5Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6Jacob’s well was there. Jesus therefore, being tired from his journey, sat down by the well. It was about the sixth hour .
6Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7A woman of Samaria came to draw water. Jesus said to her, “Give me a drink.”
7Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."
8For his disciples had gone away into the city to buy food.
8(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9The Samaritan woman therefore said to him, “How is it that you, being a Jew, ask for a drink from me, a Samaritan woman?” (For Jews have no dealings with Samaritans.)
9Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10Jesus answered her, “If you knew the gift of God, and who it is who says to you, ‘Give me a drink,’ you would have asked him, and he would have given you living water.”
10Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."
11The woman said to him, “Sir, you have nothing to draw with, and the well is deep. From where then have you that living water?
11Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12Are you greater than our father, Jacob, who gave us the well, and drank of it himself, as did his children, and his livestock?”
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."
13Jesus answered her, “Everyone who drinks of this water will thirst again,
13Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but whoever drinks of the water that I will give him will never thirst again; but the water that I will give him will become in him a well of water springing up to eternal life.”
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."
15The woman said to him, “Sir, give me this water, so that I don’t get thirsty, neither come all the way here to draw.”
15Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."
16Jesus said to her, “Go, call your husband, and come here.”
16Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."
17The woman answered, “I have no husband.” Jesus said to her, “You said well, ‘I have no husband,’
17Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 for you have had five husbands; and he whom you now have is not your husband. This you have said truly.”
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."
19The woman said to him, “Sir, I perceive that you are a prophet.
19Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20Our fathers worshiped in this mountain, and you Jews say that in Jerusalem is the place where people ought to worship.”
20Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."
21Jesus said to her, “Woman, believe me, the hour comes, when neither in this mountain, nor in Jerusalem, will you worship the Father.
21Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 You worship that which you don’t know. We worship that which we know; for salvation is from the Jews.
22Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But the hour comes, and now is, when the true worshippers will worship the Father in spirit and truth, for the Father seeks such to be his worshippers.
23Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God is spirit, and those who worship him must worship in spirit and truth.”
24Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."
25The woman said to him, “I know that Messiah comes,” (he who is called Christ). “When he has come, he will declare to us all things.”
25Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."
26Jesus said to her, “I am he, the one who speaks to you.”
26Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."
27At this, his disciples came. They marveled that he was speaking with a woman; yet no one said, “What are you looking for?” or, “Why do you speak with her?”
27Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"
28So the woman left her water pot, and went away into the city, and said to the people,
28Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29“Come, see a man who told me everything that I did. Can this be the Christ?”
29"Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"
30They went out of the city, and were coming to him.
30Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31In the meanwhile, the disciples urged him, saying, “Rabbi, eat.”
31Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."
32But he said to them, “I have food to eat that you don’t know about.”
32Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."
33The disciples therefore said one to another, “Has anyone brought him something to eat?”
33Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"
34Jesus said to them, “My food is to do the will of him who sent me, and to accomplish his work.
34Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Don’t you say, ‘There are yet four months until the harvest?’ Behold, I tell you, lift up your eyes, and look at the fields, that they are white for harvest already.
35Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 He who reaps receives wages, and gathers fruit to eternal life; that both he who sows and he who reaps may rejoice together.
36Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
37 For in this the saying is true, ‘One sows, and another reaps.’
37Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 I sent you to reap that for which you haven’t labored. Others have labored, and you have entered into their labor.”
38Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."
39From that city many of the Samaritans believed in him because of the word of the woman, who testified, “He told me everything that I did.”
39Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."
40So when the Samaritans came to him, they begged him to stay with them. He stayed there two days.
40Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41Many more believed because of his word.
41Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42They said to the woman, “Now we believe, not because of your speaking; for we have heard for ourselves, and know that this is indeed the Christ, the Savior of the world.”
42Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."
43After the two days he went out from there and went into Galilee.
43Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44For Jesus himself testified that a prophet has no honor in his own country.
44Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."
45So when he came into Galilee, the Galileans received him, having seen all the things that he did in Jerusalem at the feast, for they also went to the feast.
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46Jesus came therefore again to Cana of Galilee, where he made the water into wine. There was a certain nobleman whose son was sick at Capernaum.
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47When he heard that Jesus had come out of Judea into Galilee, he went to him, and begged him that he would come down and heal his son, for he was at the point of death.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48Jesus therefore said to him, “Unless you see signs and wonders, you will in no way believe.”
48Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
49The nobleman said to him, “Sir, come down before my child dies.”
49Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."
50Jesus said to him, “Go your way. Your son lives.” The man believed the word that Jesus spoke to him, and he went his way.
50Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51As he was now going down, his servants met him and reported, saying “Your child lives!”
51Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52So he inquired of them the hour when he began to get better. They said therefore to him, “Yesterday at the seventh hour, the fever left him.”
52Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."
53So the father knew that it was at that hour in which Jesus said to him, “Your son lives.” He believed, as did his whole house.
53Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54This is again the second sign that Jesus did, having come out of Judea into Galilee.
54Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.