1The beginning of the Good News of Jesus Christ, the Son of God.
1Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2As it is written in the prophets, “Behold, I send my messenger before your face, who will prepare your way before you. Malachi 3:1
2Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3The voice of one crying in the wilderness, ‘Make ready the way of the Lord! Make his paths straight!’” Isaiah 40:3
3Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake."
4John came baptizing or, immersing in the wilderness and preaching the baptism of repentance for forgiveness of sins.
4Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5All the country of Judea and all those of Jerusalem went out to him. They were baptized by him in the Jordan river, confessing their sins.
5Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6John was clothed with camel’s hair and a leather belt around his waist. He ate locusts and wild honey.
6Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7He preached, saying, “After me comes he who is mightier than I, the thong of whose sandals I am not worthy to stoop down and loosen.
7Naye alihubiri akisema, "Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8I baptized you in The Greek word (en) translated here as “in” could also be translated as “with” in some contexts. water, but he will baptize you in the Holy Spirit.”
8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu."
9It happened in those days, that Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John in the Jordan.
9Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10Immediately coming up from the water, he saw the heavens parting, and the Spirit descending on him like a dove.
10Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11A voice came out of the sky, “You are my beloved Son, in whom I am well pleased.”
11Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
12Immediately the Spirit drove him out into the wilderness.
12Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13He was there in the wilderness forty days tempted by Satan. He was with the wild animals; and the angels were serving him.
13akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14Now after John was taken into custody, Jesus came into Galilee, preaching the Good News of the Kingdom of God,
14Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15and saying, “The time is fulfilled, and the Kingdom of God is at hand! Repent, and believe in the Good News.”
15"Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!"
16Passing along by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew the brother of Simon casting a net into the sea, for they were fishermen.
16Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17Jesus said to them, “Come after me, and I will make you into fishers for men.”
17Yesu akawaambia, "Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
18Immediately they left their nets, and followed him.
18Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19Going on a little further from there, he saw James the son of Zebedee, and John, his brother, who were also in the boat mending the nets.
19Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20Immediately he called them, and they left their father, Zebedee, in the boat with the hired servants, and went after him.
20Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21They went into Capernaum, and immediately on the Sabbath day he entered into the synagogue and taught.
21Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22They were astonished at his teaching, for he taught them as having authority, and not as the scribes.
22Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23Immediately there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he cried out,
23Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24saying, “Ha! What do we have to do with you, Jesus, you Nazarene? Have you come to destroy us? I know you who you are: the Holy One of God!”
24akapaaza sauti, "Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!"
25Jesus rebuked him, saying, “Be quiet, and come out of him!”
25Yesu akamkemea, "Nyamaza! Mtoke mtu huyu."
26The unclean spirit, convulsing him and crying with a loud voice, came out of him.
26Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27They were all amazed, so that they questioned among themselves, saying, “What is this? A new teaching? For with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him!”
27Watu wote wakashangaa, wakaulizana, "Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!"
28The report of him went out immediately everywhere into all the region of Galilee and its surrounding area.
28Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29Immediately, when they had come out of the synagogue, they came into the house of Simon and Andrew, with James and John.
29Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30Now Simon’s wife’s mother lay sick with a fever, and immediately they told him about her.
30Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31He came and took her by the hand, and raised her up. The fever left her, and she served them.
31Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32At evening, when the sun had set, they brought to him all who were sick, and those who were possessed by demons.
32Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33All the city was gathered together at the door.
33Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34He healed many who were sick with various diseases, and cast out many demons. He didn’t allow the demons to speak, because they knew him.
34Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35Early in the morning, while it was still dark, he rose up and went out, and departed into a deserted place, and prayed there.
35Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36Simon and those who were with him followed after him;
36Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37and they found him, and told him, “Everyone is looking for you.”
37Walipomwona wakamwambia, "Kila mtu anakutafuta."
38He said to them, “Let’s go elsewhere into the next towns, that I may preach there also, because I came out for this reason.”
38Yesu akawaambia, "Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo."
39He went into their synagogues throughout all Galilee, preaching and casting out demons.
39Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40A leper came to him, begging him, kneeling down to him, and saying to him, “If you want to, you can make me clean.”
40Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, "Ukitaka, waweza kunitakasa!"
41Being moved with compassion, he stretched out his hand, and touched him, and said to him, “I want to. Be made clean.”
41Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, "Nataka, takasika!"
42When he had said this, immediately the leprosy departed from him, and he was made clean.
42Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43He strictly warned him, and immediately sent him out,
43Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44and said to him, “See you say nothing to anybody, but go show yourself to the priest, and offer for your cleansing the things which Moses commanded, for a testimony to them.”
44"Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
45But he went out, and began to proclaim it much, and to spread about the matter, so that Jesus could no more openly enter into a city, but was outside in desert places: and they came to him from everywhere.
45Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.